Tuesday, March 29, 2011

UINGEREZA 1 GHANA 1: ASAMOAH GYAN AIBEBA GHANA DAKIKA ZA MWISHO.

Wachezaji wa timu ya Taifa ya Ghana wakishangilia mara baada ya mshambuliaji wa timu hiyo Asamoah Gyan kuisawazishia timu yake bao dhidi ya Uingereza na kupelekea timu hizo kwenda sare ya bao 1-1 katika mchezo wa kimataifa wa kirafiki uliochezwa katika Uwanja wa Wembley, London, Uingereza usiku huu.

Mshambuliaji wa timu ya Taifa ya Uingereza Andy Carroll akishangilia mara baada ya kuifungia timu yake bao la kuongoza dhidi wakati timu hizo zilipocheza usiku huu. 

Carroll akiachia shuti kali la mguu wa kushoto lililompita kipa wa Ghana Richard Kingston na kutinga wavuni.

Mashabiki wa Ghana wapatao 18,000 waliohudhuria mchezo huo kuishangilia timu yao usiku huu.

Golikipa wa Uingereza Joe Hart akiokoa hatari langoni mwake katika mchezo huo.

Winga wa Uingereza Ashley Young akipiga shuti kali huku beki wa Ghana akijaribu kumzuia, shuti hilo la  mchezaji liliokolewa na golikipa Kingston.

Mchezaji wa Ghana Derek Boateng na mchezaji wa Uingereza Joleon Lescott wakichimbana mikwara katika mchezo baina ya timu hizo jana usiku.


Matokeo ya michezo mingine ya kimataifa ya kirafiki:

Belarus 0-1 Canada

China PR 3-0 Honduras

Colombia 0-2 Chile

Cyprus 0-1 Bulgaria

Ecuador 0-0 Peru

England 1-1 Ghana

France 0-0 Croatia

Germany 1-2 Australia

Greece 0-0 Poland

Portugal 2-0 Finland

Qatar 1-1 Russia

Rep of Ireland 2-3 Uruguay

Slovakia 1-2 Denmark

Ukraine 0-2 Italy


No comments:

Post a Comment