DAR ES SALAAM, Tanzania
KIKOSI kamili cha timu ya TP Mazembe kutoka DRC kinatarajiwa kutua nchini Ijumaa April 1 mwaka huu kwa ajili ya mchezo wao wa marudiano ya michuano ya Klabu Bingwa ya Afrika dhidi ya timu ya Simba katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Ofisa Habari wa Simba, Clinford Ndimbo alisema maandalizi kwa ajili ya mchezo huo unaotarajiwa kuchezwa Jumapili Aprili 3 yapo katika hatua za mwisho.
Alisema uongozi wa timu Mazembe umesema kuwa timu itawasili Ijumaa lakini hawakutaja muda wala mahali watapofikia ingawa tayari Simba wameshawaandalia mahala pa kufukia kama wenyeji wao.
Alisema viingilio katika mchezo huo vitakuwa kama ifuatavyo ambapo VIP "A" kiingilio kitakuwa shs. 40,000, VIP "B" shs. 20,000, VIP "C" shs. 10,000, Blue Mzunguko shs. 7,000 na Kijani mzunguko shs. 5,000.
No comments:
Post a Comment