Tuesday, March 29, 2011

KUNDI LA TAIFA STARS LAZIDI KUWA GUMU.

ALGERS, Algeria
MSIMAMO wa kundi D la michuano ya fainali za mataifa ya bara la Afrika iliyo katika hatua ya kufuzu umeendelea kuziweka timu za kundi hilo kwenye wakati mgumu baada ya timu ya taifa ya Algeria kupata ushindi dhidi ya timu ya taifa ya Morocco hapo jana.

Algeria wakicheza nyumbani walifanikiwa kupata ushindi wa bao moja kwa sifuri lililofungwa kwa njia ya mkwaju wa penati na Hassan Yebda katika dakika ya tano ya mchezo hali ambayo inaifanya timu hiyo kufikisha point nne sawa na timu nyingine.

Kufuatia hatua hiyo timu ya taifa ya Jamhuri ya Afrika ya kati inaongoza kwa tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa ambapo mpaka sasa imeshakufungwa mabao mawili na kufunga mabao matatu, huku Tanzania ikishika nafasi ya pili kwa kuwa na point nne huku ikiwa imefunga mabao matatu na kufungwa matatu.

Timu ya taifa ya Morocco inakamata nafasi ya tatu kwa kufikisha point nne, imefunga bao moja na kufungwa bao moja na timu ya taifa ya Algeria inakamata nafasi ya nne kwa kuwa na point nne, mabao mawili ya kufunga na mabao matatu ya kufungwa.

Michezo inayofuata ya kundi hilo itachezwa kati ya June 3-5 ambapo Tanzania watafanya ziara huko Barthelemy Boganda Stadium, mjini Bangui kwa kucheza na Jamuhuri ya Afrika ya kati na Algeria watasafiri hadi mjini Rabat kwenye uwanja wa Moulay Abdellah kucheza na timu ya taifa ya Morocco.

Wakati huo huo michezo ya kuwania kufuzu kucheza fainali za mataifa ya Afrika za mwaka 2012 iliendelea jana ambapo:

Msumbiji 0 - 2 Zambia
Congo Brazzaville 0 - 3 Ghana
DR Congo 3 - 0 Mauritius
Madagascar 1 - 1 Guinea
Niger 3 - 1 Sierra Leone
Sudan 3 - 0 Swaziland
Ivory Coast 2 - 1 Benin
Nigeria 4 - 0 Ethiopia

No comments:

Post a Comment