Tuesday, October 5, 2010

TORRES NJE KIKOSI CHA HISPANIA.

MADRID, Hispania
MSHAMBULIAJI, Fernando Torres ametemwa timu ya taifa ya Hispania inayojiandaa na mchezo wa kufuzu fainali za Kombe la Ulaya 2012 dhidi ya Lithunia na Scotland.
 
Torres, mfungaji mabao wa Liverpool amekuwa akiandwa na majeraha ya mguu tangu msimu uliopita. Katika mchezo uliopita, Torres alitoka dakika 10 wakati mchezo ukiendelea ambapo timu hiyo ilipochapwa mabao 2-1 na kibonde Blackpool Jumapili iliyopita.
 
Baada ya kutoka, Torres alikwenda moja kwa moja kwenye vyumba vya kuvalia nguo kabla ya kufuatwa na kocha, Roy Hodgson huku akionekana kuugulia maumivu ya korodani.
 
" Ana maumivu ya korodani, lakini sifahamu ana maumivu kiasi gani. Madaktari wanaendelea kumfanyia uchunguzi wa kina ili kubaini ukubwa wa tatizo lake, tatizo lake lilitushangaza wengi kwasababu lilimtokea mapema kabisa ya mchezo" alisema Hodgson.
 
Kocha huyo alidokeza kuwa awali hawakufahamu kama mchezaji huyo anakabiliwa na maumivu ya korodani na hajui nini kilitokea kwa madai Torres alikuwa na kiwango bora kabla ya kuanza mchezo huo. Mshambuliaji huyo alifanyiwa vipimo vya mionzi kubaini ukubwa wa tatizo.

No comments:

Post a Comment