Tuesday, October 5, 2010

"WAAMUZI LAZIMA WATULINDE," - NASRI.

LONDON, England
MUDA mfupi baada ya Hatem Ben Arfa wa Newcastle United kuvujika mguu, kiungo wa Arsenal, Samir Nasri amewajia waamuzi wa mchezo wa soka England kuwapa ulinzi mkali.
 
Arfa alivunjika mguu baada ya kuchezewa rafu mbaya na mchezaji wa Manchester City, Mholanzi, Nigel de Jong mchezo walioshinda mabao 2-1 Jumapili iliyopita, lakini mwamuzi Martin Atkinson hakumpa adhabu.
 
Mchezaji huyo alitolewa nje kwa machela na hatacheza mechi zilizobaki msimu huu. Nasri alisema De Jong alidhamiria kumchezea rafu Arfa na kuonya kuwa endapo hatua kali hazitachukuliwa mchezo wa soka utaingia dosari nchini humo.
 
Katika hatua nyingine, kocha wa timu ya taifa ya Uholanzi, Bert van Marwijk, amemtema de Jong katika kikosi chake katika mechi ya kufuzu Kombe la Ulaya 2012.
 
Kocha huyo alisema amechukua uamuzi huo kwa madai mchezaji huyo alicheza rafu ya makusudi. " Muda mfupi baada ya rafu ile nilizungumza naye, nilimwambia umecheza mbaya ya makusudi, hakuwa na sababu ya kufanya vile," alisema Marwijk.
 
Mchezaji huyo anakumbukwa na mashabiki wa soka baada ya kumrukia mguu wa kifua kiungo wa Hispania, Xabi Alonso katika mechi ya fainali ya Kombe la Dunia 2010. Hispania ilishinda bao 1-0.

No comments:

Post a Comment