LONDON, England
KLABU ya Liverpool imekumbwa na mpasuko mkubwa baada ya bodi ya wakurugenzi kutofautiana kuhusu ofa iliyowekwa mezani na mmiliki wa timu ya 'baseball' Boston Sox, John Henry.
Mkanganyiko huo ulitokea juzi usiku baada ya wamiliki wa Liverpool, Tom Hicks na George Gillett kujarabu kutaka kuwafukuza kazi Mkurugenzi Mtendaji, Christian Purslow na Mkurugenzi wa Fedha, Ian Ayre na nafasi zao kutaka kujazwa na raia wa Wamerakani.
Mzozo huo ulitokea muda mfupi baada ya ofa kuwekwa mezani, mbali ya Henry, bilionea mwingine kutoka Asia alijitokeza kutaka kuinunua klabu hiyo lakini siyo Kenny Huang raia wa China aliyejitoa mapema.
Mwenyekiti, Martin Broughton alitumia kura ya veto kuwalinda, Purslow na Ayre ambao walitakiwa kuondoka Anfield na nafasi zao kuchukuliwa na Mack Hicks, mtoto wa Tom Hicks na Lori Kay McCutcheon.
Purslow na Broughton wanapinga Hicks na Gillett kuwa wasemaji wa mwisho wa kutoa uamuzi kwenye bodi ya wakurugenzi kuhusu mchakato wa malipo katika benki ya Royal Bank ya Scotland ambapo wamekopa. Vigogo hao wanataka uamuzi wa mwisho ufanywe na wakurugenzi watano.
Hicks na Gillett walitangaza kuiuza Liverpool pauni milioni 800 kabla ya kupunguza bei hadi kufikia pauni milioni 600. Mzozo huo, umeibuka wakati klabu hiyo inadaiwa pauni milioni 237 na benki ya Royal ya Scotland. Matukio hayo, yamekuja siku chake baada ya Liverpool kutupwa nje na timu ya daraja la pili Northampton katika michuano ya Kombe la Carling.
Jumapili iliyopita, Liverpool ilichapwa mabao 2-1 na timu iliyopanda daraja la pili na kusababisha mashabiki wenye hasira kutaka Roy Hodgson atimuliwe na nafasi yake kujazwa na kocha wa zamani wa kikosi hicho, Kenny Dalglish.
No comments:
Post a Comment