MSHAMBULIAJI wa klabu ya Manchester city ambae kwa sasa anaitumikia klabu ya Real Madrid ya nchini Hispania kwa mkopo Emmanuel Adebayor amekanusha taarifa za yeye kuwa mbioni kurejea kwenye timu ya taifa ya Togo ambayo mwishoni mwa juma hili itaendelea na kampeni ya kusaka nafasi ya kushiriki fainali za mataifa ya Afrika za mwaka 2012 kwa kucheza na timu ya taifa ya Malawi.
Adebayor amekanusha taarifa hizo baada ya Raisi wa Shirikisho la Soka nchini Togo Gabriel Ameyi kueleza wazi kwamba mshambuliaji huyo atajiunga na kikosi cha timu ya taifa kufuatia kumaliza dhamira yake ya kustahafu soka la kimataifa.
Adebayor alisema hakuwahi kubadili msimamo wake wa kutokuichezea timu ya taifa ya Togo na ameshangazwa na kitendo cha Kocha Mkuu Stephen Keshi kumjumuisha kwenye kikosi chake kitakachoshuka uwanjani mwishoni mwa juma hili.
Ameyi alivieleza vyombo vya habari kwamba mshambuliaji huyo alibadili msimamo baada ya kukutana nae mjini Madrid na kufanya mazungumzo ya muda.
Adebayor alitangaza kustahafu soka la kimataifa baada ya timu ya taifa ya Togo kushambuliwa na waasi wa mji wa kabinda nchini Angola mwanzoni mwa mwaka jana wakati timu hiyo ilipokua safarini kushiriki fainali za mataifa ya Afrika za mwaka 2010.
No comments:
Post a Comment