Monday, March 28, 2011

FIFA KUTUMIA TEKNOLIGIA YA VIDEO KOMBE LA DUNIA 2014.

ZURICH, Switzerland
RAIS wa Shirikisho la Soka Duniani (FIFA), Sepp Blatter amethibitisha kuwa teknologia ya video itaweza kutumika katika fainali za Kombe la Dunia 2014 nchini Brazil, akiongezea kuwa taratibu kwajili ya mfumo utakuwa umekamilika katika kipindi cha mashindano hayo.

Kwa kawaida katika mchezo wa soka huwa hakutakiwi kuwa na matumizi ya teknologia, Lakini Blatter alikiri kuwa kuna mabaliko inabidi yafanyike.

Uingereza ndio walikuwa wahanga katika Kombe la Dunia lililofanyika mwaka uliopita Afrika ya Kusini walipokataliwa bao ambalo lilionekana kabisa kuingia nyavuni tukio ambalo kama teknologia ya video ingetumika basi lingekuwa bao.

Akihojiwa Blatter alisema kwamba anafikiri ifikapo mwaka 2012 mfumo huo utakuwa tayari kutambua kama bao litakuwa limefungwa au la kabla ya kuanza kutumia katika fainali za Kombe la Dunia 2014, Brazil.

"Ni muhimu kufungua mjadala mpya kuhusu hili ili kuepusha Waingereza kuendelea kukosa haki yao." alimalizia kwa utani Blatter.

No comments:

Post a Comment