KOCHA wa Real Madrid Jose Mourinho amethibisha kuwa yalikuwa yamebaki masaa machache kukubali kukinoa kikosi cha timu ya Taifa ya Uingereza kabla moyo wake haujasita kufanya hivyo katika dakika za mwisho.
Kocha huyo anayejulikana kwa jina la "The Special One" ailikiri kuwa alikuwa tayari kukubali ofa ya kuifundisha England, baada ya kuondoka Chelsea.
Kocha huyo raia wa Ureno ambaye aliondoka Chelsea Septemba 2007, miezi miwili kabla kocha wa Uingereza kwa kipindi hicho Steve McClaren hajatimuliwa na nafasi yake kuchukuliwa na Fabio Capello, alifafanua kuwa aliamua dakika za mwisho kuwa bado anapendelea kuwa kocha wa vilabu.
Akihojiwa na gazeti moja la Ufaransa alisema kuwa ilikuwa imebaki saa moja kabla sijaingia mkataba na Uingereza.
Aliendelea kusema kuwa katika dakika za mwisho alianza kuifikiria kazi yake mpya hiyo ya kufundisha timu ya taifa, ambapo atakuwa na mechi moja katika mwezi muda wote atakuwa akiutumia ofisini au kufuatilia mechi zingine halafu atasubiria mpaka yatakuja mashindano kama ya Ulaya au Kombe la Dunia nikaona hii kazi hainifai.
No comments:
Post a Comment