LONDON, England
MSHAMBULIAJI wa Chelsea Fernando Torres ameweka wazi kuwa kiungo wa Arsenal Cesc Fabregas atakuwa ni chaguo zuri kwa Barcelona kama wakiamua kumsajili ingawa hadhani kuwa timu hiyo inahitaji kusajili kiungo kwa sasa.
"Sijui kama Barcelona wanamhitaji mchezaji kama Fabregas. Hiyo ni juu ya Kocha pep Guardiola kuamua. Sifuatilii kwa karibu Ligi ya Hispania. Ni vigumu kuiweka sawa timu kama Barcelona na nani atatoka kama wakimsajili Fabregas," alisema torres akihojiwa na gazeti moja la Hispania.
"Ni mchezaji wa kweli wa timu hiyo hatahivyo na chaguo zuri kama akisajiliwa. Cesc anaheshimika zaidi Uingereza kuliko Hispania, kwasababu hajawahi kucheza Hispania. watu hapa Uingereza wamhesabu kama mmoja wa wachezaji watatu bora Uingereza.
No comments:
Post a Comment