Monday, March 28, 2011

NIGERIA, ARGENTINA USO KWA USO JUNE MOSI.

ABUJA, Nigeria
TIMU ya taifa ya Nigeria itacheza mchezo wa kimataifa wa kirafiki dhidi ya mabingwa wa zamani wa dunia timu ya taifa ya Argentina June mosi mwaka huu.

Rais wa Shirikisho la Soka nchini humo Aminu Maigari alisema taratibu za kuchezwa kwa mchezo huo tayari zimeshakamilika na wana imani Argentina itawaongezea kasi katika harakati za kusaka nafasi ya kushiriki fainali za mataifa ya bara la Afrika kwa mwaka 2012 ambapo Super Eagles watarejea tena uwanjani June 4/5 kucheza na timu ya taifa ya Ethiopia.

Alisema mchezo huo utachezwa mjini Abuja katika Uwanja wa taifa na watauchukulia kama sehemu ya kutaka kulipiza kisasi cha kufungwa bao moja kwa sifuri kwenye fainali za kombe la dunia ambapo Nigeria walipangwa katika kundi moja na Argentina.

No comments:

Post a Comment