Tuesday, March 29, 2011

BARRY KUKIONGOZA KIKOSI CHA ENGLAND DHIDI YA GHANA LEO.

LONDON, England
KOCHA Mkuu wa timu ya taifa Uingereza Fabio Capello amemteua kiungo wa klabu ya Manchester City Gareth Barry kuwa nahodha wa kikosi chake ambacho leo kitarejea uwanjani kucheza mchezo wa kimataifa wa kirafiki dhidi ya timu ya taifa ya Ghana.

Capello amefanya mabadiliko hayo ya baada ya kumuondoa kikosini John Terry pamoja na Frank Lampard kufuatia sababu za kuwa majeruhi baada ya kucheza mchezo wa kimataifa wa mwishoni mwa juma lililopita dhidi ya timu ya taifa ya Wales.

Sababu nyingine ilipelekea kocha huyo wa kimataifa toka nchini Italia kumteua Barry kuwa nahodha ni kutokana na kurejea mapema kwa Wayne Rooney, kwenye klabu yake ya Manchester united ambayo inajukumu zito la kuhakikisha inashinda michezo yote ya ligi iliyosalia kwa ajili ya kujihakikishia nafasi ya kutwaa ubingwa wa ligi msimu huu.

Barry mwenye umri wa miaka 30, atapata nafasi ya kuwa kiongozi wa kikosi cha timu ya taifa ya Uingereza ambacho kesho atakitumikia kwa mara ya 46 na kumbu kumbu zaonyesha kwamba mchezaji huyo alishawahi kuwa nahodha mwezi uliopita pindi The Three Lion walipocheza na timu ya taifa ya Denmark.

Barry amesema kuteuliwa kwake kuwa nahodha wa timu ya taifa ya Uingereza amekuchukulia kama sehemu ya kuboresha historia ya sola lake lakini bado akaanisha wazi kwamba kila mmoja ndani ya kikosi chao ni kiongozi.

Katika hatua nyingine Capello amesema kesho kikosi chake kitakua na mabadiliko makubwa huku akitarajia kumuanzisha mshambuliaji wa klabu ya Liverpool Andy Carroll.

Katika safu ya ulinzi atakuwepo Gary Cahill, Phil Jagielka pamoja na Leighton Baines, huku kipa Joe Hart pamoja na Scott Parker wakitegemea kuendelea kuwepo kikosini kama kawaida.

No comments:

Post a Comment