NAHODHA na kiungo wa klabu ya Liverpool Steven Gerrard amesema usajili uliofanywa na meneja wa klabu hiyo Kenny Dalglish katika msimu wa dirisha dogo umeziba nafasi ya mshambuliaji alieondoka klabuni hapo na kujiunga na klabu ya Chelsea Fernando Torres.
Gerrard amesema ujio wa Andy Carroll pamoja na Luis Suárez umebadilisha mtazamo wa kikosi cha Liverpool ambacho mwanzoni mwa msimu huu kilidhaurika na kila mmoja kufuatia matokeo mambovu yaliyokua yakiwaandama.
Alisema bado Torres ni mchezaji mzuri na anaekidhi viwango vya kuongoza safu ya ushambuliaji lakini ukweli ni kwamba bado wana haki ya kujivunia usajili wa wachezaji hao wawili uliofanywa mwezi januari.
Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 30 pia amesisitizia suala la meneja wao kwa sasa Dalglish ambapo amesema anastahili kuendelea kusali kikosini kutokana na kazi nzuri aliyoifanya tangu alipokichukua kikosi kutoka mikononi mwa Roy Hodgson mwishoni mwa mwaka jana.
Alisema Dalglish anapendwa na kila mmoja klabuni hapo na katu hatojisikia vyema endapo meneja huyo wa kimataifa toka nchini Scotland ataondoka mwishoni mwa msimu huu kama mkataba wake unavyoeleza.
Gerrard ameeleza wazi kwamba wakati Rafael Benitez akitimuliwa kazi mwishoni mwa msimu uliopita klabuni hapo nao walikua katika wakati mgumu wa kufikiria nani atakuwa mbadala wa meneja huyo toka nchini Hispania ambapo majina mengi yalisikika toka kwenye vyombo mbali mbali vya habari.
No comments:
Post a Comment