SHIRIKISHO la Soka la Japan (JFA) limesema kwamba litapeleka timu katika michuano ya Copa Amerika inayotarajiwa kufanyika Argentina pamoja na nchi kuwa katika majonzi ya kukumbwa na tetemeko la ardhi la chini ya bahari hivi karibuni ambapo watu zaidi ya 10,000 wanahofiwa kupoteza maisha.
Katibu Mkuu wa JFA Kozo Toshima alithibitisha ushiriki wa timu hiyo katika mashindano hayo, pamoja na kukabiliwa na wakati huo mgumu.
Kwa kusimamisha Ligi Kuu ya nchi hiyo maarufu kama J-league hiyo mpaka mwezi April, hiyo inamaanisha ligi hiyo ya nyumbani itaendelea wakati wa michuano ya Copa Amerika.
Kocha wa Japan Alberto Zaccheroni ataweza kulazimika kuita nyota wa timu hiyo waliopo Ulaya ili kuinusuru J-League kuwakosa nyota wake.
No comments:
Post a Comment