Wednesday, April 27, 2011

CHAMPIONS LEAGUE: REAL MADRID YAPIGWA 2-0 NA BARCELONA.



Baadhi ya wachezaji wa Barcelona wakijaribu kuzia vurugu zilikuwa zikitokea wakati wa kwenda mapumziko, ambapo katika vurugu hizo golikipa wa akiba wa Barcelona aliyekuwa benchi alipewa kadi nyekundu.

Mchezo ulikuwa ukisimama mara kwa mara kutoka faulo za hapa na pale zilizokuwa zikichezo kama inavyoonekana pichani.

Mwamuzi wa mchezo akimuonyesha kadi nyekundu mchezaji wa Madrid mapema katika kipindi cha pili baada ya kumchezea vibaya Marcherano.

Vijimambo vya mchezoni: mshabiki wa Madrid akiwa amemmulika kipa Barcelona Victor Valdes katika mchezo huo.

Kocha wa Madrid Jose Mourinho akiwa upande wa mashabiki mara baada ya mwamuzi wa mchezo kumuamuru kuondoka katika benchi la ufundi kufuatia kutoa lugha chafu kwa mwamuzi huyo baada ya kumpa Pepe kadi nyekundu.

Messi akifunga bao la pili katika mchezo huo.

Mourinho akisalimiana na Kocha wa Barcelona Pep Guardiola kabla ya kuanza kwa mchezo huo.

No comments:

Post a Comment