BEKI wa kimataifa toka nchini Romania Stefan Radu hatoonekana tena uwanjani akiwa na kikosi cha klabu yake ya Lazio kwa kipindi cha msimu kilichosalia kufuatia majeraha yanayomkabili.
Stefan Radu analazimika kuwa nje ya uwanjaa kufuatia maumivu makali ya mgongo yanayomsumbua hivyo ameshauriwa kupumzika kwa muda wa mwezi mmoja ama zaidi ili aweze kurejea katika hali yake ya kawaida.
Beki huyo mwenye umri wa miaka 24, ameripotiwa kuwa na maumivu makali ya mgongo ambayo huenda yakawa yamesababishwa na mpasuko mdogo katika pingili za mfupa wa uti wa mgongo ulioonekana katika picha za X Ray.
No comments:
Post a Comment