MILAN, Italia
KOCHA wa zamani wa AC Milan Leonardo ameajiriwa kama kocha mpya wa Inter Milan.
Mabingwa hao wa Ulaya na Italia walimtaja kocha huyo katika mtandao wake Ijumaa, siku baada ya mkataba wa Rafa Banitez haujasitishwa.
Mkataba wa Leonardo unaanza Jumatano na unafikia tamati June 2012.
Benitez ameingoza Inter kunyakuwa ubingwa wa Klabu Bingwa ya Dunia wiki iliyopita, lakini timu inashikilia nafasi ya saba katika ligi, wakiwa pointi 13 nyuma ya mahasimu wao AC Milan wanaongoza ligi hiyo. Kocha huyo wa Hispania amedumu katika klabu hiyo kwa muda wa miezi sita baada ya kuchukua mikoba iliyoachwa na Jeso Mourihno, aliyeondoka kuelekea Real Madrid msimu huu.
Wednesday, December 29, 2010
AJALI YA PIKIPIKI YAMUONDOA DUNIANI MCHEZAJI WA ZAMANI WA LIVERPOOL.
MCHEZAJI wa kimataifa wa zamani wa Israel na Liverpool Avi Cohen amefariki dunia kufuatia majeraha makubwa aliyopata kichwani baada ya kupata ajali ya pikipiki.
Mtoto wa kiume wa mchezaji huyo Tamir Cohen anayechezea klabu ya Bolton Wanderers katika ligi kuu ya Uingereza amesema baba yake alitangazwa kufariki na madaktari katika hospitali ya Ichilov mjini Tel Aviv.
Avi Cohen aliyekuwa akicheza nafasi ya ulinzi alikuwa mchezaji wa kwanza wa Israel kucheza katika ligi kubwa ya Uingereza wakati alipojiunga na klabu ya Liverpool mwaka 1970.
Baada ya kustaafu kucheza soka Avi Cohen aliyefariki akiwa na umri wa miaka 54, alikuwa mwenyekiti wa chama cha wachezaji wa kulipwa cha Israel kwa zaidi ya miaka mitano hadi wakati mauti yalipomkuta.
Mtoto wa kiume wa mchezaji huyo Tamir Cohen anayechezea klabu ya Bolton Wanderers katika ligi kuu ya Uingereza amesema baba yake alitangazwa kufariki na madaktari katika hospitali ya Ichilov mjini Tel Aviv.
Avi Cohen aliyekuwa akicheza nafasi ya ulinzi alikuwa mchezaji wa kwanza wa Israel kucheza katika ligi kubwa ya Uingereza wakati alipojiunga na klabu ya Liverpool mwaka 1970.
Baada ya kustaafu kucheza soka Avi Cohen aliyefariki akiwa na umri wa miaka 54, alikuwa mwenyekiti wa chama cha wachezaji wa kulipwa cha Israel kwa zaidi ya miaka mitano hadi wakati mauti yalipomkuta.
Tuesday, December 28, 2010
WALCOTT: TULISTAHILI KUSHINDA.
LONDON, England
WINGA machachari wa Arsenal Theo Walcott kuwa ana furaha kubwa mara baada ya kuwafunga Chelsea katika Uwanja wa Emirates na kuifanya timu ikwee mpka akatika nafasi ya pili katika msimamo wa Ligi Kuu ya England kwa tofauti ya magoli mbele ya Manchester City.
Alex Song ndio aliyefunga bao la kuongoza katika kipindi cha kwanza kabla ya mabao kutoka kwa Walcott na Cesc Fabrigas na kuifanya timu kuongoza mabao 3-0. Branislav Ivanovic alifunga bao la kufutia machozi la Chelsea.
Akiongea na Sky Sports baada ya mchezo Walcott alisema timu yake ilionyesha uwezo mkubwa katika kuzuia lakini aliwaonya wachezaji wenzake kuendelea kucheza kiwango hichohicho katika mchezo wao dhidi ya Wigan Athletic Jumatano usiku.
WINGA machachari wa Arsenal Theo Walcott kuwa ana furaha kubwa mara baada ya kuwafunga Chelsea katika Uwanja wa Emirates na kuifanya timu ikwee mpka akatika nafasi ya pili katika msimamo wa Ligi Kuu ya England kwa tofauti ya magoli mbele ya Manchester City.
Alex Song ndio aliyefunga bao la kuongoza katika kipindi cha kwanza kabla ya mabao kutoka kwa Walcott na Cesc Fabrigas na kuifanya timu kuongoza mabao 3-0. Branislav Ivanovic alifunga bao la kufutia machozi la Chelsea.
Akiongea na Sky Sports baada ya mchezo Walcott alisema timu yake ilionyesha uwezo mkubwa katika kuzuia lakini aliwaonya wachezaji wenzake kuendelea kucheza kiwango hichohicho katika mchezo wao dhidi ya Wigan Athletic Jumatano usiku.
Saturday, December 25, 2010
MESSI AWAPIGIA CHAPUO XAVI NA INIESTA BALLON D'OR.
ARGENTINA
MSHAMBULIAJI wa Barcelona Lionel Messi amewasili Argentina ambako atasherekea sikukuu ya Xmas na familia yake.
Waandishi wa Habari walikuwapo katika Uwanja wa ndege wakati alipotua nchini kwao huko, na aliongea nao kuhusu mustakabali wa msimu huu wa ligi huko Hispania pamoja na tuzo zinazokuja za mchezaji bora wa dunia.
"Mwaka 2010 ulikuwa ni mwaka mzuri kwa mimi binafsi, lakini Kombe la Dunia halikwenda kama tulivyotaka," alisema Messi.
"Sasa nina majukumu ya kuhakikisha Argentina inashinda Copa America mwaka ujao, ikizingatiwa itakuwa ikichezwa hapa nyumbani.
Alipoulizwa kuhusu mawazo yake ya nani atashinda Ballon d'Or tuzo ambayo ndio nayoshikilia hivi sasa aliwapigia chapuo wachezaji wenzake wa Barcelona ambao wapo wote katika kinyang'anyiro hicho.
"Mwaka huu nafikiri mmoja kati ya wachezaji wenzangu, Xavi au Iniesta, mmoja wao anaweza kushinda," alisema.
Viungo hao wawili ni miongoni kati ya wachezaji watatuwanaogombea tuzo huyo, huku wa tatu akiwa ni Messi mwenyewe.
MSHAMBULIAJI wa Barcelona Lionel Messi amewasili Argentina ambako atasherekea sikukuu ya Xmas na familia yake.
Waandishi wa Habari walikuwapo katika Uwanja wa ndege wakati alipotua nchini kwao huko, na aliongea nao kuhusu mustakabali wa msimu huu wa ligi huko Hispania pamoja na tuzo zinazokuja za mchezaji bora wa dunia.
"Mwaka 2010 ulikuwa ni mwaka mzuri kwa mimi binafsi, lakini Kombe la Dunia halikwenda kama tulivyotaka," alisema Messi.
"Sasa nina majukumu ya kuhakikisha Argentina inashinda Copa America mwaka ujao, ikizingatiwa itakuwa ikichezwa hapa nyumbani.
Alipoulizwa kuhusu mawazo yake ya nani atashinda Ballon d'Or tuzo ambayo ndio nayoshikilia hivi sasa aliwapigia chapuo wachezaji wenzake wa Barcelona ambao wapo wote katika kinyang'anyiro hicho.
"Mwaka huu nafikiri mmoja kati ya wachezaji wenzangu, Xavi au Iniesta, mmoja wao anaweza kushinda," alisema.
Viungo hao wawili ni miongoni kati ya wachezaji watatuwanaogombea tuzo huyo, huku wa tatu akiwa ni Messi mwenyewe.
Friday, December 17, 2010
CHAMPIONS LEAGUE DRAW.
First Leg Feb. 15-16 and 22-23 • Arsenal vs. Barcelona• Copenhagen vs. Chelsea • Inter Milan vs. Bayern Munich • Lyon vs. Real Madrid • Marseille vs. Manchester United • AC Milan vs. Tottenham • AS Roma vs. Shakhtar Donetsk • Valencia vs. Schalke Second Leg March 8-9 and 15-16 • Barcelona vs. Arsenal• Bayern Munich vs. Inter Milan • Chelsea vs. Copenhagen • Manchester United vs. Marseille • Real Madrid vs. Lyon • Schalke vs. Valencia • Shakhtar Donetsk vs. AS Roma • Tottenham vs. AC Milan |
Wednesday, December 15, 2010
ETO'O AIVULIA KOFIA TP MAZEMBE.
ABU DHABI
MSHAMBULIAJI wa Inter Milan amesema kuwa anafuatilia kiwango cha wawakilishi wa Afrika TP Mazembe katika michuano ya Klabu Bingwa ya Dunia kwa kujivunia kwa kiasi kikubwa.
Nilifuatilia toka mechi yao ya kwanza nilipowasili Abu Dhabi," alisema nahodha huyo wa Cameroon akiongea na mtandao wa FIFA.com Jumatano.
Mchezo wao wa kwanza dhidi ya Pachuca ulivyoanza na tayari walikuwa wameshashinda. Waafrika katika timu yetu walianza kuwapa moyo, wakiwamini kuwa watashinda.
Nilifurahi na kujivunia kwa kuwa walishinda mchezo huo. Wanajivunia kuliwakilisha bara letu, baada ya ushindi katika mchezo wao wa pili dhidi Internacional kutoka Amerika Kusini na napenda kutuma salamu za pongezi kwao."
Inter nao walifanikiwa kuingia fainali Jumatano baada ya kuifunga klabu ya Seongnam kutoka Asia mabao 3-0. Sasa watakutana na TP Mazembe katika mchezo wa fainali Jumamosi usikose.
MSHAMBULIAJI wa Inter Milan amesema kuwa anafuatilia kiwango cha wawakilishi wa Afrika TP Mazembe katika michuano ya Klabu Bingwa ya Dunia kwa kujivunia kwa kiasi kikubwa.
Nilifuatilia toka mechi yao ya kwanza nilipowasili Abu Dhabi," alisema nahodha huyo wa Cameroon akiongea na mtandao wa FIFA.com Jumatano.
Mchezo wao wa kwanza dhidi ya Pachuca ulivyoanza na tayari walikuwa wameshashinda. Waafrika katika timu yetu walianza kuwapa moyo, wakiwamini kuwa watashinda.
Nilifurahi na kujivunia kwa kuwa walishinda mchezo huo. Wanajivunia kuliwakilisha bara letu, baada ya ushindi katika mchezo wao wa pili dhidi Internacional kutoka Amerika Kusini na napenda kutuma salamu za pongezi kwao."
Inter nao walifanikiwa kuingia fainali Jumatano baada ya kuifunga klabu ya Seongnam kutoka Asia mabao 3-0. Sasa watakutana na TP Mazembe katika mchezo wa fainali Jumamosi usikose.
HISPANIA YAFUNGA MWAKA WAKIWA VINARA WA SOKA DUNIANI.
ZURICH, Switzerland
HISPANIA ambayo imeshinda Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza mwaka huu inamaliza mwaka ikiwa inaongoza katika viwango vya Shirikisho la Soka Duniani (FIFA).
Uholanzi ambayo ilifungwa katika fainali za Kombe la Dunia na Hispania inashika nafsi ya pili wakati Ujerumani imepanda nafasi moja juu ya Brazil ambayo inashika nafasi ya nne toka mwezi uliopita. USA ndio inaongoza nchi za Amerika Kaskazini (CONCACAF), huku kwa upande wa viwango vya FIFA ikipanda kwa nafasi sita hadi nafasi ya 18.
Argentina na England zimebaki katika nafsi zao ya tano na sita. Hispania wameongoza katika orodha hiyo ya viwango vya FIFA kwa miaka mitatu mfululizo.
Nchi pekee ya Afrika iliyopo katika kumi bora Misri wao wamepanda nafsi moja hadi ya tisa, wakati Australia imeshuka kwa nafasi sita hadi ya 26 lakini bado inashikilia nafasi ya kwanza kwa nchi za Asia.
Urusi ambayo imeshinda nafasi ya kuandaa Kombe la Dunia 2018 mapema mwezi huu imebaki katika nafasi ya 13 wakati wenyeji wa fainali hizo 2022 Qatar wameanguka mpaka nafasi ya 114.
HISPANIA ambayo imeshinda Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza mwaka huu inamaliza mwaka ikiwa inaongoza katika viwango vya Shirikisho la Soka Duniani (FIFA).
Uholanzi ambayo ilifungwa katika fainali za Kombe la Dunia na Hispania inashika nafsi ya pili wakati Ujerumani imepanda nafasi moja juu ya Brazil ambayo inashika nafasi ya nne toka mwezi uliopita. USA ndio inaongoza nchi za Amerika Kaskazini (CONCACAF), huku kwa upande wa viwango vya FIFA ikipanda kwa nafasi sita hadi nafasi ya 18.
Argentina na England zimebaki katika nafsi zao ya tano na sita. Hispania wameongoza katika orodha hiyo ya viwango vya FIFA kwa miaka mitatu mfululizo.
Nchi pekee ya Afrika iliyopo katika kumi bora Misri wao wamepanda nafsi moja hadi ya tisa, wakati Australia imeshuka kwa nafasi sita hadi ya 26 lakini bado inashikilia nafasi ya kwanza kwa nchi za Asia.
Urusi ambayo imeshinda nafasi ya kuandaa Kombe la Dunia 2018 mapema mwezi huu imebaki katika nafasi ya 13 wakati wenyeji wa fainali hizo 2022 Qatar wameanguka mpaka nafasi ya 114.
Tuesday, December 14, 2010
TP MAZEMBE YAENDELEA KUANDIKA HISTORIA, KOCHA N'DIAYE AJIVUNIA KIKOSI CHAKE.
ABU DHABI.
KOCHA wa TP Mazembe Lamine N'Diaye ameonyesha kufurahishwa kwake baada ya ushindi walioupata wa mabao 2-0 dhidi ya Internacional katika mchezo wa nusu fainali ya Kombe la Klbu Bingwa ya Dunia ulichezwa usiku huu.
Ni mara ya kwanza kwa timu ya Afrika kufika katika hatua hiyo katika mashindano hayo na N'Diaye anajivunia kwa kiasi kikubwa uwezo walionyesha wachezaji wake.
"Ni kitu muhimu kwetu," alisema N'Diaye akiuambia mtandao wa Fifa.com. Tupo hapa kuiwakilisha Afrika, na Afrika nzima itajivunia kazi yetu.
"Tunajiamini, tuna uhakika na unaweza kuona kuona hilo wakati tukianza kushambulia, haswa mwanzoni mwa kipindi cha pili. Tuna bahati pia, na usisahau golikipa wetu ni mzuri ni kama mchawi vile!
"Tumefanikiwa kuonyesha kwamba wachezaji wetu ni wa kiwango cha juu. Tumepata ushindi mzuri. Ni ushindi mzuri kwa timu na watu wa DRC, na kila mwafrika anapaswa kujivunia timu hii."
Mazembe sasa anasubiri kukutana na mshindi katika fainali kwenye mchezo mwingine wa nusu fainali kati ya aidha Inter Milan au Seongnam IIhwa Chunma mchezo utakachezwa leo.
KOCHA wa TP Mazembe Lamine N'Diaye ameonyesha kufurahishwa kwake baada ya ushindi walioupata wa mabao 2-0 dhidi ya Internacional katika mchezo wa nusu fainali ya Kombe la Klbu Bingwa ya Dunia ulichezwa usiku huu.
Ni mara ya kwanza kwa timu ya Afrika kufika katika hatua hiyo katika mashindano hayo na N'Diaye anajivunia kwa kiasi kikubwa uwezo walionyesha wachezaji wake.
"Ni kitu muhimu kwetu," alisema N'Diaye akiuambia mtandao wa Fifa.com. Tupo hapa kuiwakilisha Afrika, na Afrika nzima itajivunia kazi yetu.
"Tunajiamini, tuna uhakika na unaweza kuona kuona hilo wakati tukianza kushambulia, haswa mwanzoni mwa kipindi cha pili. Tuna bahati pia, na usisahau golikipa wetu ni mzuri ni kama mchawi vile!
"Tumefanikiwa kuonyesha kwamba wachezaji wetu ni wa kiwango cha juu. Tumepata ushindi mzuri. Ni ushindi mzuri kwa timu na watu wa DRC, na kila mwafrika anapaswa kujivunia timu hii."
Mazembe sasa anasubiri kukutana na mshindi katika fainali kwenye mchezo mwingine wa nusu fainali kati ya aidha Inter Milan au Seongnam IIhwa Chunma mchezo utakachezwa leo.
MASHOGA WAMJIA JUU BLATTER.
LONDON, England
KIKUNDI cha Kimataifa cha kutetea haki za mashoga kimemtaka Rais wa Shirikisho la Soka Duniani (FIFA), Sepp Blatter kuwaomba radhi kufuatia kauli yake aliyoitoa hivi karibuni kuhusiana na mashoga watakaosafiri kwenda Qatar kushuhudia fainali za Kombe la Dunia 2022.
Blatter alizungumza Jumatatu kuwa mashabiki ambao ni mashoga "inabidi wajizuie kufanya mambo yao ya kishoga" wakati wa Kombe la Dunia Qatar, ambapo huko vitendo vya kishoga ni haramu.
Mkurugenzi wa mawasiliano wa tawi la Ulaya la kikundi hicho Juris Lavrikovs, alisema kauli hiyo imewashangaza na imewakwaza sana.
"Nafikiri wangetoa ripoti kamili inayoeleweka na sio kuzungumza juu juu," alisema Lavrikovs akiwaambia waandishi wa habari. "Tunaongelea suala la haki za msingi za binadamu ambayo inakiukwa."
Blatter alitoa kauli hiyo Jumatatu Afrika Kusini wakati wa chakula cha mchana. aliulizwa kama naona kutakuwa na tatizo lolote la kiutamaduni wakati mashindano hayo yatapofanyika Qatar.
"Naweza kusema inabidi wajizuie kufanya vitendo vyao vya kishoga wakati wakiwa huko," alisema Blatter huku akitabasamu.
"Huu si utani ni suala la kufa na kupona," alisema Lavrikovs. "Qatar na zaidi ya nchi 70 duniani bado wanapingana na masuala ya ushoga na nchi zingine zinafikia hatua ya kumnyonga yoyote atakayebainika anafanya vitendo hivyo.
"Inasikitisha kuona taasisi ambayo inasimamia michezo, na huwa inapingana na aina yoyote ya ukandamizaji, ikitoa kauli kama hiyo." alimalizia Lavrikovs.
KIKUNDI cha Kimataifa cha kutetea haki za mashoga kimemtaka Rais wa Shirikisho la Soka Duniani (FIFA), Sepp Blatter kuwaomba radhi kufuatia kauli yake aliyoitoa hivi karibuni kuhusiana na mashoga watakaosafiri kwenda Qatar kushuhudia fainali za Kombe la Dunia 2022.
Blatter alizungumza Jumatatu kuwa mashabiki ambao ni mashoga "inabidi wajizuie kufanya mambo yao ya kishoga" wakati wa Kombe la Dunia Qatar, ambapo huko vitendo vya kishoga ni haramu.
Mkurugenzi wa mawasiliano wa tawi la Ulaya la kikundi hicho Juris Lavrikovs, alisema kauli hiyo imewashangaza na imewakwaza sana.
"Nafikiri wangetoa ripoti kamili inayoeleweka na sio kuzungumza juu juu," alisema Lavrikovs akiwaambia waandishi wa habari. "Tunaongelea suala la haki za msingi za binadamu ambayo inakiukwa."
Blatter alitoa kauli hiyo Jumatatu Afrika Kusini wakati wa chakula cha mchana. aliulizwa kama naona kutakuwa na tatizo lolote la kiutamaduni wakati mashindano hayo yatapofanyika Qatar.
"Naweza kusema inabidi wajizuie kufanya vitendo vyao vya kishoga wakati wakiwa huko," alisema Blatter huku akitabasamu.
"Huu si utani ni suala la kufa na kupona," alisema Lavrikovs. "Qatar na zaidi ya nchi 70 duniani bado wanapingana na masuala ya ushoga na nchi zingine zinafikia hatua ya kumnyonga yoyote atakayebainika anafanya vitendo hivyo.
"Inasikitisha kuona taasisi ambayo inasimamia michezo, na huwa inapingana na aina yoyote ya ukandamizaji, ikitoa kauli kama hiyo." alimalizia Lavrikovs.
Monday, December 13, 2010
MANCHESTER UNITED 1 ARSENAL 0
MCHEZAJI wa Park Ji-Sung wa Manchester United akishangilia bao wakati timu hiyo ilipokuwa ikimenyana na Arsenal usiku huu katika Uwanja wa Old Traford, bao ambalo ndilo pekee lilifungwa katika mchezo huo limeiwezesha United kushikilia usukani katika msimamo wa Ligi Kuu ya Uingereza kwa pointi mbili zaidi ya Arsenal na Chelsea zinazofuatia katika msimamo wa ligi hiyo huku wakiwa na mchezo mmoja mkononi.
Saturday, December 11, 2010
WENGER: EVRA FUNGA DOMO LAKO.
LONDON, England
KOCHA wa Arsenal Arsene Wenger amechukizwa na kauli aliyoitoa beki wa Manchester United Patrice Evra.
Timu hizo zikitarajiwa kukutana Jumatatu usiku katika Ligi Kuu ya Uingereza, Evra aliwatania wapinzania wao hao wakati akihojiwa na katika luninga moja ya Ufaransa akisema kuwa wakicheza na Arsenal ni kama sehemu ya mazoezi na kuongeza kuwa timu kukosa vikombe kwa kipindi kirefu kuwa ni ujinga.
Akiongea na waandishi wa habari Ijumaa, Wenger alijitahidi kuzuia vita ya maneno na Mfaransa mwenzake huyo. Badala yake alifafanua kuwa timu yake haiwezi kubabaishwa na maneno ya kejeli ili kuongeza presha ya mchezo.
"Tunaongozwa na aina ya jinsi tunavyotaka kucheza mpira na sio kwa maneno ya mtu yoyote ambaye tunacheza naye. alisema Wenger. "Binafsi, naamini kwamba mchezaji mkubwa yoyote huwa anamuheshimu mpinzania wake na hicho ndicho tunachojaribu kufanya."
Arsenal ina rekodi nzuri ya michezo ya ugenini katika Ligi Kuu msimu huu na wanasafiri kwenda Old Traford kukutana na United ambao nao wana rekodi nzuri ya kushinda mechi za nyumbani.
Monday, December 6, 2010
KINYANG'ANYIRO CHA BALLON D'Or NI KATI YA MESSI, XAVI NA INIESTA.
PARIS, Ufaransa
WACHEZAJI wa Barcelona Andres Iniesta, Xavi Hernandez na Lionel Messi ndio majina ya wachezaji watatu waliteuliwa na Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) kugombea tuzo ya Mchezaji Bora wa Dunia maarufu kama "Ballon d'Or".
Viungo Iniesta na Xavi wameteuliwa kutokana na mchango wao mkubwa uliopelekea timu ya Taifa ya Hispania kunyakua Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza, wakati mshambuliaji Muagentina Messi yeye ametoa mchango mkubwa kwa timu yake ya Barcelona kuhakikisha inatetea taji lake la Ligi ya Hispania.
Messi alishinda mwaka uliopita wakati magazeti ya michezo ya Ufaransa walipotoa tuzo hiyo kwa mchezaji bora wa Ulaya. Wameungana mwaka huu na waandaaji wa tuzo ya mchezaji bora wa FIFA na kuunda tuzo moja.
Kocha wa zamani wa Inter Milan Jose Mourinho, Kocha wa timu ya Taifa ya Hispania Vicente del Bosque na Kocha wa Barcelona ndio majina matatu ya makocha walioteliwa kugombea tuzo ya kocha bora wa dunia kwa mwaka huu.
Mshindi atatangazwa January, 2011.
WACHEZAJI wa Barcelona Andres Iniesta, Xavi Hernandez na Lionel Messi ndio majina ya wachezaji watatu waliteuliwa na Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) kugombea tuzo ya Mchezaji Bora wa Dunia maarufu kama "Ballon d'Or".
Viungo Iniesta na Xavi wameteuliwa kutokana na mchango wao mkubwa uliopelekea timu ya Taifa ya Hispania kunyakua Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza, wakati mshambuliaji Muagentina Messi yeye ametoa mchango mkubwa kwa timu yake ya Barcelona kuhakikisha inatetea taji lake la Ligi ya Hispania.
Messi alishinda mwaka uliopita wakati magazeti ya michezo ya Ufaransa walipotoa tuzo hiyo kwa mchezaji bora wa Ulaya. Wameungana mwaka huu na waandaaji wa tuzo ya mchezaji bora wa FIFA na kuunda tuzo moja.
Kocha wa zamani wa Inter Milan Jose Mourinho, Kocha wa timu ya Taifa ya Hispania Vicente del Bosque na Kocha wa Barcelona ndio majina matatu ya makocha walioteliwa kugombea tuzo ya kocha bora wa dunia kwa mwaka huu.
Mshindi atatangazwa January, 2011.
Thursday, December 2, 2010
URUSI KUANDAA KOMBE LA DUNIA 2018, QATAR 2022.
ZURICH, Switzerland
SHIRIKISHO la Soka la Dunia (FIFA) imefikia uamuzi na kuwapa kibali Urusi kuwa wenyeji wa KOmbe la Dunia 2018. Urusi walikuwa wanakabiliwa na upinzani mkubwa kutoka Uingereza, lakini Kamati ya Utendaji ya FIFA iliamua kuipa nafasi hiyo Urusi.
Kura zilipigwa na Kamati ya Utendaji ya Shirikisho hilo lenye wajumbe 24, na hiyo itakuwa ni mara ya kwanza kwa nchi hiyo kuandaa michuano hiyo mikubwa na muhimu duniani.
Wakati huohuo FIFA limeiteua nchi ya Qatar kuandaa fainali za Kombe la Dunia 2022. Katika kinyang'anyiro hicho Qatar ilikuwa ikikabiliwa na upinzani mkubwa kutoka kwa USA, lakini Kamati ya Utendaji iliamua kuipa nafasi hiyo Qatar.
Katika kinyang'aro hicho nchi zingine ambazo zilikuwa zikitaka nafsi hiyo ni pamoja na South Korea, Japan, Australia na USA, lakini zote hizo hazikufanikiwa.
Baada ya Kombe la Dunia 2002 liliandaliwa bara la Asia hii itakuwa ni mara ya pili kwa bara hilo kupata nafasi ya kuwa mwenyeji.
Ifuatayo chini ni orodha ya nchi ambazo zimeshawahi kuandaa michuano hiyo, washindi, idadi ya mabao pamoja na washindi wa pili.
SHIRIKISHO la Soka la Dunia (FIFA) imefikia uamuzi na kuwapa kibali Urusi kuwa wenyeji wa KOmbe la Dunia 2018. Urusi walikuwa wanakabiliwa na upinzani mkubwa kutoka Uingereza, lakini Kamati ya Utendaji ya FIFA iliamua kuipa nafasi hiyo Urusi.
Kura zilipigwa na Kamati ya Utendaji ya Shirikisho hilo lenye wajumbe 24, na hiyo itakuwa ni mara ya kwanza kwa nchi hiyo kuandaa michuano hiyo mikubwa na muhimu duniani.
Wakati huohuo FIFA limeiteua nchi ya Qatar kuandaa fainali za Kombe la Dunia 2022. Katika kinyang'anyiro hicho Qatar ilikuwa ikikabiliwa na upinzani mkubwa kutoka kwa USA, lakini Kamati ya Utendaji iliamua kuipa nafasi hiyo Qatar.
Katika kinyang'aro hicho nchi zingine ambazo zilikuwa zikitaka nafsi hiyo ni pamoja na South Korea, Japan, Australia na USA, lakini zote hizo hazikufanikiwa.
Baada ya Kombe la Dunia 2002 liliandaliwa bara la Asia hii itakuwa ni mara ya pili kwa bara hilo kupata nafasi ya kuwa mwenyeji.
Ifuatayo chini ni orodha ya nchi ambazo zimeshawahi kuandaa michuano hiyo, washindi, idadi ya mabao pamoja na washindi wa pili.
Subscribe to:
Posts (Atom)