Friday, April 29, 2011

HAMMAM KUZIWEZESHA NCHI ZA AFRIKA.

Blatter (Kulia) akiwa na mpinzani wake Hamman (kushoto).

NCHI za bara la Afrika huenda zikafaidia zaidi katika utaratibu wa kuhakikisha soka la barani humo linakua endapo wajumbe wa Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) watamchagua Mohamed Bin Hammam kuwa Rais wa shirikisho hilo katika uchaguzi utakaofanyika June mosi mjini Zurich, Uswiz.

Mohamed Bin Hammam amepania kuendeleza kasumba ya kufanya mapinduzi ya maendeleo ya soka barani Afrika huku akiahidi kuongeza fedha ambazo hutumwa kila mwaka katika nchi za bara hilo kutoa dola za kimarekani 250,000 hadi 500,000.

Mpinzani huyo wa Rais wa sasa wa FIFA Sepp Blatter ametoa ahadi ya kuongeza fedha hizo alipofanya ziara barani Afrika katika nchi za Equatorial Guinea, Chad, Jamhuri ya Afrika kati, Rwanda, Gabon pamoja na Cameroon.

Mohamed Bin Hammam ambae pia ni Rais wa Shirikisho la Soka Barani Asia ameahidi kuongeza fedha za mradi wa GOAL ambao husimamiwa na FIFA kutoa dola za kimarekani 400,000 hadi dola za kimarekani million moja.

Baada ya kumaliza ziara ya kufanya kampeni barani Afrika Mohamed Bin Hammam hii leo alikua barani ulaya katika nchi Uingereza kwa ajili ya harakati hizo za kuomba kura na ameelezea furaha yake ya kukutana na viongozi wa soka wa nchi hiyo.

Baada ya kuzulu nchini Uingereza Mohamed Bin Hammam anatarajia kufunga safari hadi katika barala la Amerika ya kusini ambapo huko atahudhuria mkutano mkuu wa shirikisho la soka la ukanda huo utakaofanyika nchini Paraguay.

BARCELONA YAFIKIRIA KUMSHTAKI MOURINHO.

BARCELONA, Hispania
UONGOZI wa klabu ya FC Barcelona unajipanga kumshitaki meneja wa klabu ya Real Madrid José  Mourinho kufuatia maneno yake makali aliyoyatoa mbele ya vyombo vya habari mara baada ya mchezo wa usiku wa kuamkia hii leo kumalizika huko Estadio Stantiago Bernabeu.

Uongozi wa klabu hiyo unafikiria hatua hiyo baada ya kukiri kuchomwa na maneno makali ambayo wamedai hayapaswi kuzungumza na mtu kama Mourinho aliedumu katika ramani ya soka kwa vigezo vyenye sifa kubwa duniani.

Katika mkutano na waandishi wa habari Mourinho alionyeshwa kuchukizwa na namna ya matokeo ya mchezo wa jana yalivyopatikana ambapo alifikia hatua ya kudai kwamba ni vigumu kwa upande wake kupata ushindi anapocheza na klabu ya Barcelona.

Alisema hafahamu kama klabu hiyo inajidaia jina la UNICEF lililopo katika jezi zao ambapo ameeleza wazi kwamba huenda jina hilo linafanyiwa tangazo kwa namna yoyote ile kwa kuhakikisha wanashinda ili ujumbe ufike kwa wahusika salama wa salamini.

Pia Mourinho akaendelea kuishambulia klabu hiyo kwa kueleza kwamba huenda ukaharibu uliopo kati yao na Rais wa Shirikisho la Soka nchini Hispania Angel Maria ambae pia ni mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Soka barani Ulaya (UEFA) ukawa unachangia kwa klabu hiyo ya Catalan kupata ushindi kirahisi.

Hata hivyo ameomba aelezwe wazi kwamba kulikua na uhalali gani kwa Pepe kuonyweshwa kadi nyekundu na muamuzi Wolfgang Stark kutoka nchini Ujerumani ili hali tayari ilikua imeshaonekana wazi kwamba mchezaji huyo pamoja na Daniel Alves walikua katika harakati za kuuwani mpira.

Pia akahoji adhabu aliyopewa ya kuondolewa kwenye benchi na kutakiwa kukaa jukwaani ili hali alikua akitetea maslahi ya kikosi chake lakini akaendelea kuuliza kwa nini beki wake Sergio Ramos alionyeshwa kadi ya njano ambayo inamfanya aukose mchezo wa merejeano utakaochezwa Camp Nou juma lijalo.

Katika hatua nyingine Mourinho akamgeukiwa kocha wa Barcelona Pep Guardiola Isala kwa kumsifia kuwa ni kocha mzuri lakini amekua akichafuliwa na sifa ya kutwaa ubingwa wa barani Ulaya kwa kashfa za kikosi chake kupendelewa katika michezo muhimu.


Akitolea mfano wa mwaka 2009 meneja huyo wa kimataifa toka nchini Ureno ametanabaisha kwamba katika mwaka huo, Barcelona walibebwa wazi wazi na muamuzi kutoka nchini Norway Tom Ovrebo ambae aliwanyima Chelsea haki ya kutinga hatua ya fainali kufautia matokeo ya sare ya bao moja kwa moja yaliyopatikana katika mchezo huo.

Alisema mara baada ya mchezo huo wachezaji wa Chelsea wakiongozwa na Didier Drogba walimlalamikia muamuzi huyo kutokana na maamuzi mabovu aliyoyatoa dhidi yao lakini mshambuliaji huyo alijikuta akiambulia adhabu huku Barcelona wakisonga mbele katika hatua ya fainali na kufanikiwa kutwaa ubingwa mbele ya Man Utd.

Lakini pamoja na kusema yote hayo Jose Mourinho akaendelea kutamba kikosi chake huku akisema kwamba wao ndio vinara wa kutwaa ubingwa wa barani Ulaya hivyo watakwenda mjini Barcelona kushindana na anaamini nafasi yao ya kusonga mbele bado ipo.


Guardiola alipozungumza na waandishi wa habari hakugusia lolote juu ya tuhuma hizo zaidi ya kusifia ushindi uliopatikana ugenini ambao anaamini ulichangiwa na changamoto ya wachezaji vijana kumi na mbili aliosafiri nao toka mjini Barcelona hadi mjini Madrid.

TEVEZ, ETHERINGTON KUIWAHI FAINALI FA.

LONDON, England
WINGA wa kimataifa toka nchini Uingereza pamoja na klabu ya Stoke City Matthew Etherington ameripotiwa huenda akauwahi mchezo wa hatua ya fainali ya kombe la chama cha soka nchini humo FA dhidi ya Man city utakaochezwa katika uwanja wa Wembley May 14 mwaka huu.

Kocha wa klabu Stoke City Tony Pulis alisema Matthew Etheringto, amefanyiwa vipimo na imeonekana amaumia sehemu ya nyama za paja zinazoshikilia nyuma ya goti hivyo madaktari wamemuahidi kufanya kila linalowezekana ili kuweza kuuwahi mchezo huo dhidi ya Man City.

Winga huyo mwenye umri wa miaka 29, alipatwa na maumivu hayo ya nyama za paja katika mchezo wa ligi uliochezwa usiku wa kuamkia jana dhidi ya Walves ambao walikubalia kisago cha mabao matatu kwa sifuri.

Wakati huo huo mshambuliaji wa kimataifa toka nchini Argentina pamoja na klabu ya Man City Carlos Tevez nae ameripotiwa huenda akauwahi mchezo huo wa hatua ya fainali kutokana na kuendelea kupata matibabu mazuri.

Carlos Tevez alipatwa na maumivu ya nyama za paja katika mchezo wa ligi dhidi ya Liverpool ambapo katika mchezo huo majogoo wa jiji waliibuka na ushindi wa mabao matatu kwa sifuri.

VERMAELEN KUREJEA DIMBANI.

LONDON, England
BEKI  wa kimataifa kutoka nchini Ubelgiji Thomas Vermaelen hii leo anarajea uwanjani kucheza mchezo wa wachezaji wa akiba kati ya Arsenal dhidi ya Manchester United.

Vermaelen anarejea uwanjani hii leo baada ya kupona maumivu ya kisigino yaliyomsumbua kwa muda wa miezi minane iliyopita hatua ambayo ilipelekea kufanyiwa upasuaji mwezi januari mwaka huu.

Hata hivyo kurejea kwa beki huyo mwenye umri wa miaka 25 katika mchezo wa wachezaji wa akiba, bado kunahisiwa huenda kukamfanya meneja wa klabu ya Arsenal Arsene Wenger kupata ushawishi wa kumtumia kwenye michezo ya ligi kabla ya msimu huu kumalizika.

Thursday, April 28, 2011

"SI MESSI WALA RONALDO ALIYEFIKIA KIWANGO CHANGU." PELE.

NEWYORK, Marekani
MSHAMBULIAJI nguli wa zamani kutoka Brazil Pele anaamini kuwa bado yeye ndio mchezaji bora aliyepata kutokea pamoja na ujio wa wachezaji wa sasa Lionel Messi na Cristiano Ronaldo.

Mchezaji huyo wa zamani wa Santos aliweka rekodi ya kipekee ya kufunga mabao 1,281 katika michezo 1363 aliyocheza katika kipindi cha miaka 23 aliyocheza soka.

Pele alishinda Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza akiwa na Brazil mwaka 1958 akiwa na umri wa miaka 17, na aliendelea kuchukua makombe mengine ya dunia mawili akiwa na timu hiyo ya Amerika Kusini.

Katika miaka ya karibuni Messi na Ronaldo wameonekana kuiteka dunia kwa vipaji walivyonavyo wanapokuwa uwanjani lakini Pele anaamini hakuna hata mmoja aliyemfikia.

"Kwangu mimi Pele bado ni bora. Hakuna yoyote aliyefanya zaidi ya Pele. Ni mchezaji pekee aliyeshinda ubingwa wa dunia akiwa na miaka 17, kushinda vikombe vitatu vya Kombe la Dunia na kufunga zaidi ya magoli 1,208," alikaririwa Pele akiongea na Mwandishi mmoja wa Marekani.

Wednesday, April 27, 2011

CHAMPIONS LEAGUE: REAL MADRID YAPIGWA 2-0 NA BARCELONA.



Baadhi ya wachezaji wa Barcelona wakijaribu kuzia vurugu zilikuwa zikitokea wakati wa kwenda mapumziko, ambapo katika vurugu hizo golikipa wa akiba wa Barcelona aliyekuwa benchi alipewa kadi nyekundu.

Mchezo ulikuwa ukisimama mara kwa mara kutoka faulo za hapa na pale zilizokuwa zikichezo kama inavyoonekana pichani.

Mwamuzi wa mchezo akimuonyesha kadi nyekundu mchezaji wa Madrid mapema katika kipindi cha pili baada ya kumchezea vibaya Marcherano.

Vijimambo vya mchezoni: mshabiki wa Madrid akiwa amemmulika kipa Barcelona Victor Valdes katika mchezo huo.

Kocha wa Madrid Jose Mourinho akiwa upande wa mashabiki mara baada ya mwamuzi wa mchezo kumuamuru kuondoka katika benchi la ufundi kufuatia kutoa lugha chafu kwa mwamuzi huyo baada ya kumpa Pepe kadi nyekundu.

Messi akifunga bao la pili katika mchezo huo.

Mourinho akisalimiana na Kocha wa Barcelona Pep Guardiola kabla ya kuanza kwa mchezo huo.

BREAKING NEWS: BAFANA BAFANA KUJIPIMA NGUVU NA TAIFA STARS.

Wachezaji wa Bafana Bafana wakiwa katika mazoezi.

JOHANESBURG, South Afrika
SHIRIKISHO la Soka la Afrika Kusini (Safa) na wawakilishi kutoka Tanzania wamefikia mkubaliano jioni hii juu ya mchezo wa kimataifa wa kirafiki baina ya timu za mataifa hayo utakaochezwa katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam Mei 14 mwaka huu.

Kocha Mkuu wa timu ya Taifa ya Afrika Kusini (Bafana Bafana) Pitso Mosimane alithibitisha kuwa ameletewa taarifa kutoka Safa kuhusiana na mchezo huo ambapo atatangaza kikosi kitakachoivaa timu ya taifa ya Tanzania (Taifa Stars) katika tarehe hiyo waliyokubaliana.

"Naishukuru Safa na PSL kwa ushikiriano wanaompa kuhusu mipango yetu," alisema Mosimane. "Tuna mchezo mgumu dhidi ya Misri katika kutafuta tiketi ya kucheza michuano ya Mataifa ya Afrika Juni 3, hivyo mchezo huu utakuwa ni mzuri kwa sisi kujipima nguvu.

"Naweza kusema kuwa kama tukishinda mchezo huu tutakuwa tumejiweka katika nafasi nzuri ya kukata tiketi ya kucheza michuano ya Mataifa ya Afrika 2012, Equatorial na Gabon. Hivyo mchezo huu tutakaocheza Tanzania utakuwa ni muhimu kwa maandalizi ya mchezo wetu huko Misri na nitateua kikosi imara kwa ajili ya mchezo huo."

Nae wakala anayetambulika na Shirikisho la Soka Duniani (FIFA), Damas Ndumbaro alithibisha kuwa tayari wamefikia makubaliano na wote Rais wa Shirikisho la Soka la Tanzania (TFF) Leodgar Tenga na Safa CEO Pinky Lehoko kwa ajili ya mchezo huo kwa tarehe iliyotajwa hapo juu na tayari wamepeleka taarifa FIFA.

Rais wa Safa Kirsten Nematandani pia alithibisha juu ya kuwapo kwa mchezo huo kwa tarehe hiyo. Ingawa sio tarehe ya FIFA, lakini Ligi Kuu nchini itakuwa imesimama kufuatia mchezo wa nusu fainali wa Kombe la Nedbank hivyo wameona ni wakati muafaka kwa timu ya Taifa kupata mchezo wa kujipima nguvu.

Tuesday, April 26, 2011

TFF YATANGAZA VIINGILIO VYA U-23 BAINA YA UGANDA NA TANZANIA.

DAR ES SALAAM, Tanzania
SHIRIKISHO la Soka nchini (TFF) limetangaza viingilio vya mchezo wa Kimataifa kati ya timu Taifa ya Tanzania (U23) na timu ya Taifa ya Uganda chini ya miaka 23 (The Kobs) kutafuta tiketi ya kucheza michuano ya Olimpiki  2012, London, Uingereza mchezo utakaocheza katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Akizungumza Dar es Salaam, Ofisa Habari wa TFF, Boniface Wambura alisema maandalizi katika mchezo huo muhimu yako katika hatyua za mwisho.

Alisema viingilio katika mchezo huo vitakuwa kama ifuatavyo; ambapo Jukwaa Kuu (VIP A) kiingilio kitakuwa shs. 10,000, VIP B&C 5,000, Jukwaa la rangi ya kijani, Bluu na viti vya Rangi ya Chungwa vinavyotizamana na VIP na nyuma ya magoli kiingilio kitakuwa shilingi 1,000.

Wambura alisema tiketi zinatarajiwa kuuzwa siku moja kabla ya mchezo katika vituo vya Premier Betting (Kariakoo- Mtaa wa Sukuma, Buguruni Sokoni, Manzese Midizini, JM Mall na Tandale kwa Mtogole), Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, Steers (Mtaa wa Ohio na Samora), Big Bon Msimbazi (Kariakoo) na Uwanja wa Uhuru.


The Kobs inatarajia kuwasili nchini Alhamisi Aprili 28 mwaka huu saa 10.30 jioni kwa ndege ya Uganda Air na kurejea nyumbani Jumapili Mei 1 saa 11.50 kwa ndege hiyo hiyo.

Msafara wa timu hiyo utaongozwa na Ofisa wa Shirikisho la Soka nchini Uganda (FUFA) Sam Lwere na utafikia hoteli ya Durban iliyoko Barabara ya Uhuru, Dar es Salaam.

CHAMPIONS LEAGUE: SCHALKE 04 0 MANCHESTER UNITED 2








"NASTAHILI KULAUMIWA." WENGER.

LONDON, Uingereza
BAADA ya kupoteza matumaini ya kumaliza ukame wa kutwaa vikombe kwa muda wa miaka sita iliyopita kufuatia kisago cha mabao 2-1 kilichotolewa huko Reebok Stadium, Kocha Mkuu wa klabu ya Arsenal Arsene Wenger amesema anastahili kualaumi yeye binafsi na si wachezaji wake.

Wenger alisema kijumla wachezaji wake wamejituma kikamilfu kwa muda wa msimu mzima hivyo hakuna haja ya kulaumiwa zaidi yake yeye ambae ndie mwenye jukumu la kuhakikisha ukame wa vikombe unamalizwa huko Emitrates.

Alisema kila shabiki anaeipenda Arsenal ulimwenguni atakua amechukizwa na matokeo yaliyopatikana jana hali amabyo inapelekea kuwalaumu wachezaji lakini bado ameendelea kusisitiza kuwa lawama za kushindwa kufikia melengo waliyojiwekea zinastahili kutupwa kwake.

Hata hivyo mzee huyo ameendelea kuwa na msimamo wake wa kutobadilisha mfumo wa kuwatumia vijana huku akidai kwamba bado anaamini mfumo huo ni mzuri na ipo siku utaleta mafanikio chini ya utawala wake.

Alisema ni vigumu kufanya maamuzi ya kubadilisha mfumo kutokana na matakwa ya mashabiki na kama atashawishiwa na yoyote yule anaeupinga mfumo wake kwa vielelezo sahihi atakua tayari kuubadili.

Kauli hiyo ya Arsene Wenger imepingwa vikali na beki wa zamani wa klabu ya Arsenal, Lee Michael Dixon ambapo amesema iwe isiwe ni lazima meneja huyo wa kifaransa akubalia kubadilika na kinyume na hapo ataendelea kuambulia patupu kila unapofika mwisho wa msimu.

Lee Michael Dixon amesema mfumo wa kuwategemea vijana unaotumiwa klabuni hapo tayari umeshajidhihirisha wazi hauwezi kuipa mafanikio Arsenal hivyo hakuna haja ya kuendelea kutumiwa zaidi ya kufanya usajili wa wachezaji waliokomaa.

Alisema ujio wa muwekezaji ndani ya klabu ya Arsenal unatakiwa kuchukuliwa kama faraja ya kumfanya Arsene Wenger kuiweka kando sera yake ya vijana.

Wakati huo huo Lee Michael Dixon ameikubali kauli iliyotolewa na nahodha wa klabu ya Arsenal Cesc Fabregas siku moja kabla ya mchezo wa ligi dhidi ya Spurs ambayo ilikaririwa na vyombo vya habari vya nchini kwao Hispania ikieleza kwamba ni wakati wa Arsenal kufanya maamuzi ya kutwaa vikombe ama kuendeleza makinda kama ilivyo sasa.

Lee Michael Dixon amesema kauli hiyo ina uzito wa aina yake na inajidhihirisha wazi kwamba ni vipi nahodha huyo alivyochoshwa na mwenendo uliopo klabuni hapo lakini pia akaeleza kwamba Fabregas hakustahili kulisema hilo hadharani kufuatia nafasi aliyonayo ndani ya kikosi.

Kufungwa katika mchezo wa jana mabao mawili kwa moja na Bolton Wanderers, kunadhihirisha wazi kwamba Man Utd wapo mbele kwa tofauti ya point 9 dhidi Arsenal ambao kwa sasa wanakamata nafasi ya tatu huku nafasi ya pili ikishikiliwa na Chelsea.

Saturday, April 23, 2011

WENGER AWAJIA JUU WAANDISHI WA HABARI.

LONDON, England
KOCHA wa klabu ya Arsenal Arsene Wenger amelaani kitendo cha baadhi ya waandishi wa habari kukuza maneno yanayo zungumzwa juu ya klabu hiyo ya kaskazini mwa jiji la London ambayo ipo katika harakati za kutaka kumaliza ukame wa kutwaa vikombe kwa kipindi cha miaka sita sasa.

Wenger amelaani kitendo hicho kufuatia moja ya vyombo vya habari nchini Hispania kuripoti kwamba nahodha na kiungo wa klabu ya Arsenal Cesc Fabregas alizungumza kauli inayoenda kinyume na sera za mzee huyo wa kifaransa mapema jana kabla ya mchezo wa ligi ya Uingereza dhidi ya Tottenham Hotspurs.

Alisema kila mmoja ana uhuru wa kuzungumza na kuandika la kwake lakini isizidi uwezo wa kuikandamiza Arsenal kwa utashi wa mtu ama watu binafsi kwa kupitia mianya ya wachezaji wake ambao amekiri anawatambua tabia zao.

Katika chombo hicho cha habari Cesc Fabregas alinukuliwa akisema kwamba ni wakati wa klabu ya Arsenal kufikiria kutwaa vikombe la kuachana na kasumba ya kukuza vijana, taarifa ambayo Arsene Wenger amedai haiingii akilini kama imesemwa na mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23.

Katika hatua nyingine Arsene Wenger ameendelea kusisitiza jambo la kuhakikisha anapigana hadi tone la mwisho katika harakati za kusaka ubingwa msimu huu licha ya matokeo ya sare ya mabao matatu kwa matatu yaliyopatikana jana huko White Hart Lane.

Alisema ubingwa bado upo wazi na haoni sababu ya kukiondoa kikosi chake katika harakati za kuuwani ubingwa ambao kwa sasa unawaniwa na klabu yake, Man Utd pamoja na Chelsea ambao wanakamata nafasi ya pili kwa tofauti ya mabao dhidi ya washika bunduki wa Ashburton Grove.

Alisema katika mchezo wa jana asilimia kubwa ya wachezaji wake walishindwa kwenda sambamba katika kipindi cha pili hali ambayo ilipelekea Spurs kusawazisha bao la tatu kupitia mkwaju wa penati.

Nae meneja wa klabu ya Tottenham Hotspurs Harry Redknapp amesema kuiujumla wachezaji wake walicheza kwa kujituma tena bila kuvunjika moyo baada ya kuwa nyuma kwa idadi ya mabao matatu na kwa bahati nzuri juhudi zao binafsi ziliwaokoa kujinusuru nyumbani.

Hata hivyo amedai kwamba Arsenal walicheza vizuri sana katika kipindi cha kwanza hatua ambayo ilipelekea kupata mabao matatu ya kuongoza.

ZAMALEK WALA KIBANO CHA CAF.

CAIRO, Misri
MABINGWA wa soka nchini Misri Zamalek FC sasa watalazimika kucheza michezi miwili ya kimataifa iliyo chini ya Shirikisho la soka Barani Afrika (CAF) bila ya kuwa na mashabiki uwanjani pamoja na kulipa faini ya dola za kimarekani 80,000.

Maamuzi ya klabu hiyo kongwe barani Afrika ya kucheza bila ya kuwa na mashabiki katika uwanja wa nyumbani yamefikiwa katika mkutano wa Kamati ya Nidhamu CAF kwa ajili ya kupitia matatizo ya kinidhamu yaliyojitokeza kwenye michuano ya kimataifa barani humo.

Zamalek wamefikwa na dhoruba hilo baada ya mashabiki wake kuingia uwanjani wakati wa mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya mabingwa wa nchini Tunisia Club Africain uliochezwa mapema mwezi wa tatu.

Club Africain pia wametozwa faini ya dola za kimarekani 10,000 kufuatia kosa la baadhi ya mashabiki wao kuingia uwanjani wakati wa mchezo wa kwanza uliochezwa nchini Tunisia dhidi ya Zamalek.

Kamati ya nidhamu ya CAF pia aimewaadhibu mabingwa wa zamani wa barani Afrika Enyimba ya nchini Nigeria kwa kuwatoza faini ya dola za kimarekani 20,000 kufuatia malumbano yaliyojitokeza kati ya wachezaji wa klabu hiyo dhidi ya klabu ya US Bitam ya nchini Gabon hali ambayo ilipelekea askari polisi kuingia katika sehemu yua kuchezea.

Enyimba pia wamepewa onyo kali na kamati hiyo ya nidhamu na endapo watashindwa kutii amri hiyo huenda wakafungiwa kucheza katika uwanjani wao wa nyumbani wa uliopo mjini Aba.

Klabu ya Mouloudia Alger ya nchini Algeria nayo imetozwa faini ya dola za kimarekani 5,000 kufuati mashabiki kuingia uwanjani wakati wa mchezo wa kombe la shirikisho dhidi ya Dynamos ya nchini Zimbabwe pamoja na klabu ya AS Aviacao ya nchini Angola nayo imeguswa na faini hiyo.

Klabu ya Deportivo Maxaquene, ya nchini Msumbiji, Kano Pillars ya nchini Nigeria pamoja na As Vita ya jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo zote kwa pamoja zimetozwa faini ya dola za kimarekani 5000 kwa kosa la mashabiki kuingia uwanjani.

Shirikisho la soka nchini Senegal nalo limeangukiwa na adhabu ya kutakiwa kulipa faini ya dola za kimarekani 5,000 kufuatia mashabiki kuingia uwanjani mara baada ya mchezo wa kuwania nafasi ya kucheza fainali za mataifa ya bara la Afrika kumalizika kati ya timu ya taifa ya nchi hiyo dhidi ya Cameroon walioibuka na ushindi wa bao moja kwa sifuri.

RAMOS ALIDONDOSHA KOMBE LA MFALME.

MADRID, Hispania
KUFUATIA furaha iliyopitiliza beki wa pembeni wa klabu ya Real Madrid Sergio Ramos alijikuta akiangusha kombe la ubingwa wa michuano ya Mfalme ambayo jana ilifikia tamati mjini Valencia kwa The Merengues kuibuka kidedea dhidi ya mabingwa wa soka nchini Hispania Fc Barcelona.

Sergio Ramos alijikuta akiangusha kombe la ubingwa wa michuano hiyo wakati kikosi cha Real Madrid kilipokua kikipita katika mitaa ya mji wa Valencia kikiwa juu ya gari maalum ambalo huwawezesha mashabiki kuwaona wachezaji kiurahisi.

Hata hivyo imeelezwa kwamba kombe hilo lenye uzito wa kilogram nane na urefu wa sentimita 78 limeripotiwa kuwa katika hali ya usalama licha kuingia sehemu ya chini ya gari walilokua wamepanda wachezaji.

Real Madrid wametawazwa kuwa mabingwa wa kombe la Mfalme baada ya miaka 18 iliyopita kufuatia ushindi wa bao moja kwa sifuri lililofungwa na Cristiano Ronaldo katika dakika ya 103.

José Mourinho alieweka historia ya kutwaa ubingwa wa kombe la Mfalme ambao pia ni ubingwa wake wa kwanza toka alipojiunga na klabu hiyo ya Stantiago Bernabeu alisema haikuwa kazi rahisi kukamilisha shughuli ya ushindi walioupata lakini kikubwa amefurahishwa na mafanikio yaliyopatikana.

Alisema hatua inayomfariji ni kumaliza mchezo huo akiwa na mawazo chanya ambayo ana hakika yatamsaidia katika mchezo ujao ambao utamkutanisha na Barcelona kwenye michuano ya ligi ya mabingwa barani Ulaya.

AFYA YA HOULLIER MATATANI.

LONDON, England
KOCHA wa klabu ya Aston Villa Gerard Houllier usiku wa kuamkia hii leo alilazimika kukimbizwa hospitalini huko mjini Birmingham kufuatia hali yake ya kiafya kutokua nzuri.

Uongozi wa klabu ya Aston Villa uliowakilishwa na mtendaji mkuu Paul Faulkner mbele ya vyombo vya habari umetoa taarifa hizo huku ukisisitiza kwamba hali ya meneja huyo wa kimataifa toka nchini Ufaransa ni shwari na wala hakuna shaka na hii ni kwa mujibu wa madaktari wanao mshughulikia.

Paul Faulkner alisema mapema hii leo alikwenda hospitali kumjulia hali Gerard Houllier ambapo amemkuta katika hali nzuri na yenye kuridhisha hivyo wanamichezo pamoja na mashabiki wa klabu ya Aston Villa wametakiwa kuwa watulivu.

Hata hivyo Paul Faulkner amesema bado meneja huyo mwenye umri wa miaka 63 ataendelea kupatia matibabu kwa siku kadhaa hatua ambayo itamkosesha mchezo wa mwishoni mwa juma hili ambapo kikosi chake kitakua nyumbani Villa Park kikiwakaribisha Stoke City.

Kutokana na hali hiyo meneja msaidizi Gary McAllister, amepewa jukumu la kukisimamia kikosi cha Aston Villa ambacho atakiongoza katika mchezo wa mwishoni mwa juma hili akiwa kama mkuu wa benchi la ufundi.

RADU NJE MSIMU WOTE ULIOSALIA.

LAZIO, Italia
BEKI wa kimataifa toka nchini Romania Stefan Radu hatoonekana tena uwanjani akiwa na kikosi cha klabu yake ya Lazio kwa kipindi cha msimu kilichosalia kufuatia majeraha yanayomkabili.

Stefan Radu analazimika kuwa nje ya uwanjaa kufuatia maumivu makali ya mgongo yanayomsumbua hivyo ameshauriwa kupumzika kwa muda wa mwezi mmoja ama zaidi ili aweze kurejea katika hali yake ya kawaida.

Beki huyo mwenye umri wa miaka 24, ameripotiwa kuwa na maumivu makali ya mgongo ambayo huenda yakawa yamesababishwa na mpasuko mdogo katika pingili za mfupa wa uti wa mgongo ulioonekana katika picha za X Ray.

"SIJAZUNGUMZA NA MANCINI." MAROTTA.

TURIN, Italia
MKURUGENZI Mkuu wa klabu ya Juventus Giuseppe Marotta amekana kufanya mazungumzo na meneja wa klabu ya Manchester City Roberto Mancini.

Giuseppe Marotta amekana taarifa hizo kufuatia uvumi unaoendelea katika vyombo mbali mbali vya habari ambao unadai kwamba Roberto Mancini ambae kwa sasa ana ndoto ya kuizawadia ubingwa wa FA Man City huenda akarejea nyumbani kuinoa Juventus yenye maskani yake makuu mjini Turine.

Kiongozi huyo alisema kwamba kwa sasa bado wana mkataba na meneja wao Luigi Del Neri na katu hawezi kuzungumza lolote hadi msimu huu wa ligi utakapomalizika huko nchini Italia.

Hata hivyo wakala wa Roberto Mancini, Giorgio De Giorgis amezikana taarifa hizo huku akidai kwamba mtu wake bado ana mkataba na klabu ya Man city na yeye amekua akizisikia taarifa hizo katika vyombo vya habari.

Katika hatua nyingine Giuseppe Marotta amekanusha uvumi mwingine wa kumnyemelea meneja wa klabu ya Napoli Walter Mazzarri ambae amekiwezesha kikosi chake kuwa miongoni mwa vilabu vinavyofikiriwa kucheza ligi ya mabingwa barani Ulaya msimu ujao.

NEUER KUIKIMBIA SCHALKE 04 MWISHONI MWA MSIMU.

MUNICH, Ujerumani
MLINDA mlango wa kimataifa toka nchini Ujerumani pamoja na klabu ya Schalke 04 Manuel Neuer ameonyesha nia ya kutaka kuihama klabu hiyo baada ya kugoma kusaini mkataba mpya pindi alipotakiwa kufanya hivyo.

Manuel Neuer amekataa kufanya hivyo huku ikitambulika wazi kwamba mkataba wake wa sasa utafikia kikomo mara baada ya msimu ujao kumalizika mwezi Mei mwaka 2012 hivyo ikitakua jukumu la uongozi wa klabu ya Schalke 04 kumuuza kwa kuhofia huenda akaondoka akiwa kama mchezaji huru.

Tayari mabingwa wa zamani wa nchini Ujerumani Bayern Munich wameshatangaza nia ya kutaka kumsajili kipa huyo ambae huenda akawagharimu kiasi cha paund million 20 kama ada ya uhamisho wake kutoka huko Veltins-Arena, mjini Gelsenkirchen.

Mbali na mabingwa hao wa zamani wa nchini Ujerumani pia imearifiwa kwamba mashetani wekundu kutoka nchini Uingereza Man Utd wanamuwania kipa huyo kwa udi na uvumba kwa ajili ya kutaka kuziba nafasi ya kipa wao wa sasa Edwin van der Sar ambae tayari ameshatangaza kustahafu soka mwishoni mwa msimu huu.

Monday, April 18, 2011

USHAURI WA BURE KWA SCHOLES.


LONDON, Egland
Just look at this picture and you will see why it was the correct decision by Mike Dean to dismiss Paul Scholes.
It was an awful tackle, with his stud marks clearly seen along the legs of Pablo Zabaleta in Graham Chadwick’s photograph.
It is the 10th red card of his career — a frightening statistic for a gifted and cultured playmaker, who even the great Xavi considers one of the finest he has seen.
Cutting edge: Paul Scholes challenge left Pablo Zabaletta with painful injuries
Cutting edge: Paul Scholes challenge left Pablo Zabaletta with painful injuries
The challenge was made at pace and with some venom, perhaps in retaliation for a Zabaleta foul on the Manchester United player 10 minutes earlier.
From my experience, Scholes was always a very personable player who approached me respectfully. However, he is now in reach of the 12 red cards collected by Vinnie Jones.
I’m sure that is not how he wants to be compared. I hope the red card and subsequent ban do not hasten Scholes’ retirement this summer.
We want to see more of his clever passing, even if his tackling can often be spiteful and nasty.

Friday, April 15, 2011

All the FA Cup and Premier League team news ahead of the latest fixtures



Just champion: Chelsea celebrated after finishing last season top of the pile
Just champion: Chelsea celebrated after finishing last season top of the pile

SATURDAY

FA CUP
Man City v Man United (5.15pm Wembley)
PREMIER LEAGUE
Birmingham v Sunderland (3pm)
Blackpool v Wigan (3pm)
Everton v Blackburn (3pm)
West Bromwich v Chelsea (3pm)
West Ham v Aston Villa (3pm)

SUNDAY

FA CUP
Bolton v Stoke (4pm Wembley)
PREMIER LEAGUE
Arsenal v Liverpool (4pm)

Saturday, April 9, 2011

ZANZIBAR YANYANG'ANYWA UENYEJI WA KOMBE LA KAGAME.

DAR ES SALAAM, Tanzania
BARAZA la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) hii limetoa taarifa rasmi ya kuyahamisha mashindano ya Kombe la Kagame kutoka Zanzibar kama ilivyotangazwa mara ya kwanza na kuyapeleka Sudan.

Taarifa hiyo iliyosainiwa na Katibu Mkuu wa CECAFA Nicholas Musonye imesema mashindano hayo wameamua kuyapeleka Sudan baada ya Zanzibar kushindwa kukidhi vigezo vya kuandaa huku sababu kubwa ikitajwa kuwa ni mapungufu ya fedha.

Alisema baada ya kufanya mabadiliklo hayo ratiba na makundi ya michuano hiyo itapangwa mjini Khartoum, Sudan Jumanne Aprili 12 kabla ya kuanza rasmi kwa michuano hiyo June 21 hadi July 5 mwaka huu.

Alisema kubwa lililopelekea kuyahamisha mashindano hayo kutoka visiwani Zanzibar nchini Tanzania hadi nchini Sudan ni ushawishi uliotolewa na viongozi wa chama cha soka nchini humo ambao wamekubali kuubeba mzigo huo sambamba na kusaka wafadhili.

Friday, April 1, 2011

MESSI FITI KUIVAA VILLAREAL.

BARCELONA, Hispania
JOPO la madaktari wa klabu ya Barcelona hii leo limekua na kazi nzito ya kumshughulikia kiungo wa kimataifa toka nchini Argentina Lionel Messi kwa lengo la kumuwezesha kucheza mchezo wa ligi wa mwishoni mwa juma hili.

Jopo la madakrtari huko mjini Catalan limefanya shughuli hiyo ikiwa ni sehemu ya kuongeza chachu ya kusaka ubingwa wa ligi kuu ya soka nchini Hispania ambapo Barcelona mpaka hii leo bado wapo kileleni kwa tofauti ya point tano dhidi ya Real Madrid ambao wana malengo ya kumaliza ukame wa kutwaa taji la nchini humo.

Baada ya kufanyiwa vipimo Messi amebainika kwamba hana tatizo linalomsumbua kama ilivyoripotiwa hapo awali zaidi ya kupata mshtuko wa misulu ya paja alipokua kwenye maandalizi ya mchezo wa kimataifa wa kirafiki kati ya timu y taifa ya Argentina dhIdi ya timu ya taifa ya Costa Rica.

Hata hivyo bado kiungo huyo mwenye umri wa miaka 23 ataendelea kufanyiwa uchunguzi akiwa mazoezini na wenzake ili kufahamu mustakabali wa hali yake itamruhusu kujumuishwa kikosini mwishioni mwa juma hili pale FC Barcelona watakapowakabili dhidi ya Villarreal.

Mapema hii leo taarifa zilieleza kwamba Messi alikua kwenye mashaka makubwa ya kuukosa mchezo huo wa ligi wa mwishoni mwa juma hili sambamba na mchezo wa ligi ya mabingwa barani Ulaya utakaochezwa kati kati ya juma lijalo dhidi ya Shakhtar Donetsk kutoka nchini Ukraine.

"BADO NIPONIPO SANA HAPA." RAUL

SCHALKE, Ujerumani
MSHAMBULIAJI wa kimataifa toka nchini Hispania Raúl González amesema hana mpango wowote wa kuikacha klabu yake ya sasa ya Schalke 04 ya nchini Ujerumani na badala yake atakuwepo klabuni hapo kama mkataba wake unavyoeleza.

Raúl amelazimika kupasua ukweli huo kufuatia taarifa zinazomuandama kwa sasa ambapo inadaiwa kwamba anajipanga kuondoka huko Veltins-Arena, (Gelsenkirchen) baada ya kukasirishwa na utaratibu uliochukuliwa na viongozi wa ngazi za juu wa kumtimua kazi aliekua meneja Wolfgang-Felix Magath, ambae kwa sasa amerejea kwenye klabu yake ya zamani ya Wolfsburg.

Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 33 alisema yeye binafsi alisaini mkataba wa kuitumikia klabu ya Shalke 04 hadi mwaka 2012 na hakujiunga na klabu hiyo kwa ajili ya Wolfgang-Felix Magath, ambae amelazimika kuondoka baada ya matokeo mabovu kuendelea kumuandama katika michezo ya ligi ya nchini ujerumani.

Hata hivyo Raúl amedai bado ana nafasi ya kusaidiana na wachezaji wengine klabuni hapo kwa ajili ya kuizawadia Shalke 04 ubingwa wa soka wa kombe la nchini Ujerumani mwishoni mwa msimu huu baada ya kufanikiwa kutinga kwenye hatua ya fainali ya michuano hiyo dhidi ya klabu inayoshiriki ligi daraja la pili nchini humo ya Duisburg.

Mbali na kuwa na ndoto za kuizawadia ubingwa klabu hiyo bado Raúl ana matumaini mengine ya kuhakikisha wanafika mbali katika michuano ya ligi ya mabingwa barani Ulaya baada ya kufanikiwa kutinga kwenye hatua ya robo fainali ambapo watakutana na mabingwa watetezi wa michuano hiyo Inter Milan.

LUCAS AONGEZEWA MKATABA LIVERPOOL.

LONDON, England
KOCHA wa klabu ya Liverpool Kenny Dalglish anaendelea kulifuma zaidi jeshi lake baada ya jana jioni kufanikiwa kumsainisha mkataba mpya kiungo wa kimataifa toka nchini Brazil Lucas Leiva.

Dalglish amefanisha utaratibu huo baada ya kuvutiwa na uchezaji wa kiungo huyo aliejiunga na klabu ya Liverpool mwaka 2007 akitokea nyumbani kwao kwenye klabu ya Gremio kwa uhamisho wa paund million 5.

Kocha huyo wa kimataifa toka nchini Scotland alisema Lucas ni mchezaji mwenye kubadilika kimtazamo chanya tangu alipoanza kukinoa kikosi cha klabu ya Liverpool hivyo anaamini mchezaji huyo ni hazina kubwa kwa hivi sasa pamoja na miaka ijayo.

Kwa upande wake Lucas Leiva alisema hatua ya kusaini mkataba mpya imemuweka katika mazingira mazuri klabuni hapo na kujihisi anathaminiwa kufuatia mchango wake mkubwa anaoutoa akiwa nje na ndani ya uwanja akitetea Liverpool.

Ameahidi kuendelea kufanya kazi kwa kujituma zaidi tena kwa kushirikiana na wachezaji wengine ili kuweza kutimiza malengo yaliyowekwa na uongozi wa ngazi za juu ya kuhakikisha wanarejea kwenye michuano ya ligi ya mabingwa barani Ulaya msimu ujao baada ya kukosa nafasi hiyo msimu huu.

Lucas alianza kupewa nafasi katika kikosi cha kwanza cha Liverpool baada ya kuondoka kwa kiungo wa kimataifa toka nchini Hispania Xabi Alonso pamoja na kiungo wa kimataifa toka nchini Argentina Javier Mascherano.

katika hatua nyingine Dalglish amethibitisha taarifa za kurejea mazoezini kwa kiungo na nahodha wa kikosi chake Steven Garrard ambae alikua nje ya uwanja kwa majuma kadhaa baada ya kufanyiwa upasuaji kufuatia matatizo ya ngiri yaliyokua yakimsumbua.

Alisema kurejea mazoezini kwa kiungo huyo mwenye umri wa miaka 30 kunatoa nafasi ya asilimia 50 kwa 50 ya kumchezesha katika mchezo wa ligi wa mwishoni mwa juma hili ambapo Liverpool watakua ugenini wakikabiliana na West Bromwich Albion.

Wakati huo huo meneja wa klabu ya West Bromwich Albion ambae alitimuliwa kazi ya kukinoa kikosi cha Liverpool mwishoni mwa mwaka jana Roy Hodgson amesema mchezo huo hatouchukulia kama sehemu ya kulipiza kisasi zaidi ya kuwahimiza wachezaji wake kucheza kwa kujituma kwa minajili ya kuepukana na janga la kurejea kwenye shimo la kushuka daraja msimu huu.