KOCHA wa timu ya Taifa ya Tanzania Mdenmark Jan Poulsen ametangaza kikosi cha wachezaji 23 itakayocheza na timu ya Taifa ya Morocco kuwania kufuzu michuano ya Mataifa ya Afrika itakayofanyika 2012.
Katika kikosi hicho kutakuwa na walinda mlango Juma Kaseja, Shaban Hassan Kado na Said Mohamed.
Walinzi wa kati Aggrey Morris, Erasto Nyoni na Nadir Haroub Cannavaro huku walinzi wa pembeni wakiwa Shadrack Nsajigwa, Haruna Moshi, Salmin Kiss na Stephano Mwasika.
Viungo walioitwa ni Henry Joseph, Shaban Nditi, Nurdin Bakari, Jabir Aziz, Nizer Khalfan, Seleman Kassim, Idrissa Rajabu na Salum Machaku.
Kwa upande wa washambuliaji wamo Danny Mrwanda, Mohamed Banka, Mrisho Ngasa, John Bocco na Mussa Hassan Mgosi.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Poulsen alisema wachezaji hao wanatarajia kuingia kambini hii leo huku mazoezi rasmi yakitarajiwa kuanza hapo kesho.
Stars inatarajia kucheza na Morocco Octoba 9 mwaka huu katika Uwanja wa Taifa, Dar es salaam, ukiwa na mchezo wa pili kwa timu hiyo katika kampeni hizo za kuwania kufuzu fainali za mataifa ya Africa baada ya kutoka sare ya mabao 1-1 dhidi ya Algeria katika mchezo wa kwanza.
"Mchezo dhidi ya Morocco utakuwa mgumu kama ule tuliocheza na Algeria, na katika mchezo huu unaofuata tutakuwa tukishambulia zaidi na kukaba tofauti na mchezo wa kwanza ambao tulikuwa tukikaba tu."
Wednesday, September 29, 2010
AFRIKA KUSINI YAJITOSA KINYANG'ANYIRO CHA KUANDAA AFCON 2015.
JOHANNESBURG, Afrika Kusini
KWA mujibu wa gazeti la Sowetan la Afrika Kusini , Shirikisho la Soka la nchi (SAFA) hiyo tayari limeshatuma barua Shirikisho la Soka Afrika (CAF) kuhusu nia yao ya kuandaa fainali za Mataifa ya Afrika 2015.
Mara ya mwisho nchi kuandaa michuano hiyo ilikuwa ni mwaka 1996, ambapo Bafana Bafana walichukua ubingwa wa michuano hiyo baada ya kuifunga Tunisia katika mchezo wa fainali.
Taarifa hiyo ilisema Rais wa SAFA Kirsten Nematandani alituma maombi hayo CAF Jumanne baada ya kuamuliwa katika kikao cha menejimenti kilichokaa Johannesburg kitu ambacho kilichangiwa kwa kiasi kikubwa na mafanikio waliyopata katika Kombe la Dunia.
"Bado tunafurahia mafanikio tuliyopata katika Kombe la Dunia na tunategemea itatusaidia katika kushinda mchakato wa kuandaa Kombe la Mataifa ya Afrika. Kutakuwa hakuna maswali kuhusu miundo mbunu kwa kuwa tayari ipo hapa, malazi yapo. Kutakuwa hakuna maswali kuhusu usafiri kwa sababu upo, viwanja bora pia vipo hapa. Tuna kila kitu. Tutaongea na serikali kuhusu wazo letu hili," alikaririwa akisema Nematandani.
Michuano inayofuata itaandaliwa kwa pamoja na Gabon pamoja na Equatorial Guinea 2012 na mwaka utakaofuatia wakati mashindano hayo yatakapobalidilishwa na kuwekwa katika miaka isiyogawanyika itafanyika Libya.
KWA mujibu wa gazeti la Sowetan la Afrika Kusini , Shirikisho la Soka la nchi (SAFA) hiyo tayari limeshatuma barua Shirikisho la Soka Afrika (CAF) kuhusu nia yao ya kuandaa fainali za Mataifa ya Afrika 2015.
Mara ya mwisho nchi kuandaa michuano hiyo ilikuwa ni mwaka 1996, ambapo Bafana Bafana walichukua ubingwa wa michuano hiyo baada ya kuifunga Tunisia katika mchezo wa fainali.
Taarifa hiyo ilisema Rais wa SAFA Kirsten Nematandani alituma maombi hayo CAF Jumanne baada ya kuamuliwa katika kikao cha menejimenti kilichokaa Johannesburg kitu ambacho kilichangiwa kwa kiasi kikubwa na mafanikio waliyopata katika Kombe la Dunia.
"Bado tunafurahia mafanikio tuliyopata katika Kombe la Dunia na tunategemea itatusaidia katika kushinda mchakato wa kuandaa Kombe la Mataifa ya Afrika. Kutakuwa hakuna maswali kuhusu miundo mbunu kwa kuwa tayari ipo hapa, malazi yapo. Kutakuwa hakuna maswali kuhusu usafiri kwa sababu upo, viwanja bora pia vipo hapa. Tuna kila kitu. Tutaongea na serikali kuhusu wazo letu hili," alikaririwa akisema Nematandani.
Michuano inayofuata itaandaliwa kwa pamoja na Gabon pamoja na Equatorial Guinea 2012 na mwaka utakaofuatia wakati mashindano hayo yatakapobalidilishwa na kuwekwa katika miaka isiyogawanyika itafanyika Libya.
"MCHEZO WETU DHIDI YA ARSENAL UTAKUWA MGUMU." MALOUDA.
LONDON, England
MCHEZAJI wa Chelsea Florent Malouda amesisitiza kuwa Arsenal watawapa upinzani mkubwa wakati timu hizo zitapokutana mwishoni mwa wiki hii lakini anategemea timu hiyo itawapa nafasi zaidi tofauti na ilivyokuwa kwa Manchester City.
Mabingwa hao wa Uingereza walifungwa mchezo wao wa kwanza toka ligi hiyo ianze baada ya kukubali kipigo cha bao 1-0 dhidi ya kikosi cha Robert Mancin kilichokuwa kikicheza kwa staili ya Counter Attack nyumba kwa City.
Malouda anategemea mchezo wa wazi zaidi dhidi ya Arsenal kutokana na aina ya uchezaji wao katika Uwanja wa Stamford Bridge Jumapili.
"Kila mtu anajua mchezo wa pasi wanaocheza Arsenal," alisema Malouda. "Wako vizuri. Tumeona mara nyingi timu zinapokuja hapa wanajaribu kucheza mchezo wa kuzuia na itategemea kama utafunga mapema katika mchezo lakini nafikiri Arsenal siku zote wamekuwa wakicheza mchezo wao uleule wa kupiga pasi nyingi na wamejaribu kufanya hivyo wakipambana na timu yoyote ile.
"Manchester City ni timu ngumu na ndio mchezo wetu wa kwanza kufungwa. Nitazungumza jinsi tunavyoona. Lazima tutegemee kitu kizuri mbele ya mashabiki wetu. Tulipoteza dhidi ya City na sasa tuna nafasi kwa mchezo huu tunaocheza nyumbani kurudisha ari yetu ya ushindi.
"Itakuwa ngumu kwetu kuishinda moja wapo ya kubwa nne katika Ligi Kuu (Big Four). Mchezo wa Chelsea na Arsenal siku zote umekuwa na umuhimu wake kwasababu wako nyuma yetu na tunataka kuongeza pengo ili wasitufikie kwa urahisi.
Haitakuwa rahisi kwasababu hakuna mchezo rahisi kwa Chelsea lakini huu ni muda kujiandaa na baadae tutakuwa na muda wa kufirikiri kuhusu Arsenal."
MCHEZAJI wa Chelsea Florent Malouda amesisitiza kuwa Arsenal watawapa upinzani mkubwa wakati timu hizo zitapokutana mwishoni mwa wiki hii lakini anategemea timu hiyo itawapa nafasi zaidi tofauti na ilivyokuwa kwa Manchester City.
Mabingwa hao wa Uingereza walifungwa mchezo wao wa kwanza toka ligi hiyo ianze baada ya kukubali kipigo cha bao 1-0 dhidi ya kikosi cha Robert Mancin kilichokuwa kikicheza kwa staili ya Counter Attack nyumba kwa City.
Malouda anategemea mchezo wa wazi zaidi dhidi ya Arsenal kutokana na aina ya uchezaji wao katika Uwanja wa Stamford Bridge Jumapili.
"Kila mtu anajua mchezo wa pasi wanaocheza Arsenal," alisema Malouda. "Wako vizuri. Tumeona mara nyingi timu zinapokuja hapa wanajaribu kucheza mchezo wa kuzuia na itategemea kama utafunga mapema katika mchezo lakini nafikiri Arsenal siku zote wamekuwa wakicheza mchezo wao uleule wa kupiga pasi nyingi na wamejaribu kufanya hivyo wakipambana na timu yoyote ile.
"Manchester City ni timu ngumu na ndio mchezo wetu wa kwanza kufungwa. Nitazungumza jinsi tunavyoona. Lazima tutegemee kitu kizuri mbele ya mashabiki wetu. Tulipoteza dhidi ya City na sasa tuna nafasi kwa mchezo huu tunaocheza nyumbani kurudisha ari yetu ya ushindi.
"Itakuwa ngumu kwetu kuishinda moja wapo ya kubwa nne katika Ligi Kuu (Big Four). Mchezo wa Chelsea na Arsenal siku zote umekuwa na umuhimu wake kwasababu wako nyuma yetu na tunataka kuongeza pengo ili wasitufikie kwa urahisi.
Haitakuwa rahisi kwasababu hakuna mchezo rahisi kwa Chelsea lakini huu ni muda kujiandaa na baadae tutakuwa na muda wa kufirikiri kuhusu Arsenal."
"MOURINHO ANAHITAJI MUDA ZAIDI WA KUIFANYA MADRID KUWA BORA." - FERNANDEZ.
AUXERRE, Ufaransa
KOCHA wa Auxerre Jean Fernandez anaamini kuwa kocha wa Real Madrid Jose Mourinho anahitaji muda zaidi wa kuifanya Madrid timu bora duniani.
Mshambuliaji anayecheza kwa mkopo Angel di Maria aliwahakikishia vijana wa Mourinho ushindi katika mchezo uliochezwa katika Uwanja wa Stade de 1'Abbe, Deschamps na Fernandez walivutiwa na mabeki wa timu hiyo ambao wanacheza kwa kuelewana lakini wanaona kuwa bado matatizo katika safu ya ushambuliaji.
"Unatakiwa umpe muda kidogo Mourinho kwa kuitengeneza Madrid kuwa tishio," alisema Fernandez.
"Hatahivyo, Nafikiri kuwa Madrid watapigania taji la ligi na Barcelona na pia lazima wapiganie taji la Ligi ya Mabingwa. Wanaonekana wanazuia vizuri.
"Timu yangu ilicheza vizuri, tulijipanga kujilinda na tunaweza kusema hawakutupa shida sana kwasababu hawakupata nafasi nyingi."
KOCHA wa Auxerre Jean Fernandez anaamini kuwa kocha wa Real Madrid Jose Mourinho anahitaji muda zaidi wa kuifanya Madrid timu bora duniani.
Mshambuliaji anayecheza kwa mkopo Angel di Maria aliwahakikishia vijana wa Mourinho ushindi katika mchezo uliochezwa katika Uwanja wa Stade de 1'Abbe, Deschamps na Fernandez walivutiwa na mabeki wa timu hiyo ambao wanacheza kwa kuelewana lakini wanaona kuwa bado matatizo katika safu ya ushambuliaji.
"Unatakiwa umpe muda kidogo Mourinho kwa kuitengeneza Madrid kuwa tishio," alisema Fernandez.
"Hatahivyo, Nafikiri kuwa Madrid watapigania taji la ligi na Barcelona na pia lazima wapiganie taji la Ligi ya Mabingwa. Wanaonekana wanazuia vizuri.
"Timu yangu ilicheza vizuri, tulijipanga kujilinda na tunaweza kusema hawakutupa shida sana kwasababu hawakupata nafasi nyingi."
JUVE, TOTTENHAM WAANZA KUMMEZEA MATE PIENAAR.
LONDON, England
KLABU ya soka ya Juventus inatarajiwa kuingia katika kinyang'anyiro na klabu ya Tottenham Hotspurs kuwania kumnyakuwa kiungo wa Everton Steven Pienaar katika kipindi cha dirisha dogo la usajili, kwa mujibu wa gazeti ya Daily Mail la Uingereza.
Klabu hiyo ya Italia imemtamani kwa muda mrefu mchezaji huyo wa kimataifa kutoka Afrika Kusini ambaye mkataba unaisha mwaka ujao na kumfanya kuwa huru kufanya mazungumzo na klabu nyingine kuanzia January.
Juventus wanataka kuongeza nguvu katika kikosi chake baada kuanza vibaya ligi msimu huu na wamesema kuwa kiungo huyo ndio chaguo lao katika usajili wa dirisha dogo.
Kuondoka katika klabu hiyo kwa kiungo Mauro Camoranesi na Diego kumeacha pengo kubwa katika nafasi ya kiungo mshambuliaji.
Lakini wakongwe hao kutoka mji wa Turin itabidi wapambane na Spurs kwa ajili ya huduma ya kijana huyo mwenye umri wa miaka 28, baada ya kocha wa Spurs Harry Redknapp kushindwa kusajili mchezaji yoyote katika kipindi cha majira kiangazi.
KLABU ya soka ya Juventus inatarajiwa kuingia katika kinyang'anyiro na klabu ya Tottenham Hotspurs kuwania kumnyakuwa kiungo wa Everton Steven Pienaar katika kipindi cha dirisha dogo la usajili, kwa mujibu wa gazeti ya Daily Mail la Uingereza.
Klabu hiyo ya Italia imemtamani kwa muda mrefu mchezaji huyo wa kimataifa kutoka Afrika Kusini ambaye mkataba unaisha mwaka ujao na kumfanya kuwa huru kufanya mazungumzo na klabu nyingine kuanzia January.
Juventus wanataka kuongeza nguvu katika kikosi chake baada kuanza vibaya ligi msimu huu na wamesema kuwa kiungo huyo ndio chaguo lao katika usajili wa dirisha dogo.
Kuondoka katika klabu hiyo kwa kiungo Mauro Camoranesi na Diego kumeacha pengo kubwa katika nafasi ya kiungo mshambuliaji.
Lakini wakongwe hao kutoka mji wa Turin itabidi wapambane na Spurs kwa ajili ya huduma ya kijana huyo mwenye umri wa miaka 28, baada ya kocha wa Spurs Harry Redknapp kushindwa kusajili mchezaji yoyote katika kipindi cha majira kiangazi.
ARSENAL, CHELSEA ZAENDELEZA UBABE LIGI YA MABINGWA.
ARSENAL jana imelinda rekodi yake ya ushindi wa asilimia mia moja katika kundi H baada kushinda mabao 3-1 dhidi ya timu ngumu ya Partizan Belgrade ya Serbia, huku golikipa Lukasz Fabianski akiokoa mkwaju wa penati dakika za mwisho.
Arsenal walianza kupata bao ushindi kupitia kwa mchezaji Andrei Arshavin ambaye baadae alikosa penati, mabao mengine ya Arsenal yalifungwa na Marouane Chamakh na Sebastian Squillaci huku bao la kufutia machozi la Belgrade likifungwa na Cleo.
Kabla ya mchezo kuanza, kulitokea matatizo ya kiufundi katika baadhi ya taa za pembeni kushindwa kuwaka kitu ambacho kilitishia mchezo huo kuahirishwa, lakini mwishoni mwamuzi alipokea iliyomruhusu kuendelea na mchezo huo mkwa wakati.
wakati huohuo Chelsea jana walishika usukani wa kundi F baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 katika Uwanja wa Stamford Bridge. Pamoja na kumkosa mshambuliaji wake tegemeo Didier Drogba na Frank Lampard, vijana wa Carlo Ancelotti waliweza kuwashinda mabingwa hao wa Ufaransa kwa mabao yaliyofungwa na John Terry na Nicolas Anelka.
Katika mkutano na waandishi wa habari kabla ya mchezo huo, Ancelotti aliwasihi wachezaji wake kusahau mchezo wa ligi walioupoteza dhidi ya Manchester City mwishoni mwa wiki. Ambapo Terry alimjibu kocha wake huyo kwa kuunganisha kwa kichwa mpira wa kona uliopigwa na Florent Malouda dakika saba toka mchezo huo uanze, kabla ya Anelka kuongeza la pili kwa mkwaju wa penati baada ya Stephane M'Bia kuunawa mpira uliopigwa na Michael Essien katika eneo la hatari.
Angel Di Maria aliipatia timu yake ya Real Madrid ushindi katika dakika za mwisho dhidi ya Auxerre na kufanya timu kuongoza kundi G.
Mara ya mwisho Madrid kushinda kombe la Klabu Bingwa ilikuwa ni mwaka 2002 wakati Zinedine Zidane alifunga bao kwa staili ya kipekee dhidi ya Bayer Leverkusen katika Uwanja wa Hampden Park, Glasgow. Wamewekeza kwa kiasi kikubwa kuhakikisha kuwa wanafanya vizuri katika ligi hiyo pamoja na Ligi Kuu ya nyumbani, na mchezaji ambaye walimsajili kutoka Benfica msimu huu ndiye aliyewaokoa huko Ufaransa, kwa kuukwamisha mpira wavuni kwa ufundi mkubwa baada ya mchezaji mwenzake ambaye naye amesajiliwa msimu huu Mesut Ozil kumpatia pasi safi kwenye dakika ya 81 na kuibuka kwa ushindi huo mwembamba wa bao 1-0.
AC Milan ambao walifunga Auxerre katika mchezo wa kwanza, walijikuta wakivutwa shati na Ajax ya Uholanzi kwa kutoka nao sare ya bao 1-1. Mounir El Hamdaoui ndiye aliyefunga bao la kuongoza Ajax dakika ya 23 akimalizia kazi nzuri iliyofanywa na Luis Suarez, lakini shujaa wa zamani wa Ajax Zlatan Ibrahimovic alisawazisha bao hilo dakika 15 baadae kwa kusaidiana vyema na aliyekuwa kipenzi cha mashabiki wa Uholanzi Clarence Seedorf.
AS Roma walituliza maumivu ya kufungwa na Bayern Munich katika mchezo wa kwanza wa kundi E kwa kuwafunga CFR Cluj mabao 2-1. Mabao hayakupatikana mpaka katikati ya kipindi cha pili, ambapo beki Philipe Mexes aliipatia timu yake bao la kuongoza kwa shuti kali dakika ya 69 na Marco Borriello aliongeza la pili dakika mbili baadae. Cluj walijibu mapigo dakika saba baadae wakati Ionut Rada alipotumbukiza nyavuni mpira wa kichwa na kupata bao lakufutia machozi.
Bayern walilikuja kutoka nyuma na kushinda mabao 2-1 dhidi ya Basel, ambao walianza kuongoza katika dakika ya 17 kwa bao lilifungwa na alexander Frei. Bayern walirudisha bao hilo kwa njia ya penati iliyofungwa na Bastian Schweinsteiger katika dakika ya 56, baada ya Thomas Muller kufanyiwa madhambi na Benjamin Huggel, na dakika moja kabla ya mpira kumalizika Schweinsteiger aliipatia timu yake bao la kuongoza.
Katika michezo mingine iliyochezwa jana Shakhtar Donetsk waliifunga Braga mabao 3-0 huku Spartak Moscow nao wakishinda mabao 3-0 dhidi ya Zilina.
Arsenal walianza kupata bao ushindi kupitia kwa mchezaji Andrei Arshavin ambaye baadae alikosa penati, mabao mengine ya Arsenal yalifungwa na Marouane Chamakh na Sebastian Squillaci huku bao la kufutia machozi la Belgrade likifungwa na Cleo.
Kabla ya mchezo kuanza, kulitokea matatizo ya kiufundi katika baadhi ya taa za pembeni kushindwa kuwaka kitu ambacho kilitishia mchezo huo kuahirishwa, lakini mwishoni mwamuzi alipokea iliyomruhusu kuendelea na mchezo huo mkwa wakati.
wakati huohuo Chelsea jana walishika usukani wa kundi F baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 katika Uwanja wa Stamford Bridge. Pamoja na kumkosa mshambuliaji wake tegemeo Didier Drogba na Frank Lampard, vijana wa Carlo Ancelotti waliweza kuwashinda mabingwa hao wa Ufaransa kwa mabao yaliyofungwa na John Terry na Nicolas Anelka.
Katika mkutano na waandishi wa habari kabla ya mchezo huo, Ancelotti aliwasihi wachezaji wake kusahau mchezo wa ligi walioupoteza dhidi ya Manchester City mwishoni mwa wiki. Ambapo Terry alimjibu kocha wake huyo kwa kuunganisha kwa kichwa mpira wa kona uliopigwa na Florent Malouda dakika saba toka mchezo huo uanze, kabla ya Anelka kuongeza la pili kwa mkwaju wa penati baada ya Stephane M'Bia kuunawa mpira uliopigwa na Michael Essien katika eneo la hatari.
Angel Di Maria aliipatia timu yake ya Real Madrid ushindi katika dakika za mwisho dhidi ya Auxerre na kufanya timu kuongoza kundi G.
Mara ya mwisho Madrid kushinda kombe la Klabu Bingwa ilikuwa ni mwaka 2002 wakati Zinedine Zidane alifunga bao kwa staili ya kipekee dhidi ya Bayer Leverkusen katika Uwanja wa Hampden Park, Glasgow. Wamewekeza kwa kiasi kikubwa kuhakikisha kuwa wanafanya vizuri katika ligi hiyo pamoja na Ligi Kuu ya nyumbani, na mchezaji ambaye walimsajili kutoka Benfica msimu huu ndiye aliyewaokoa huko Ufaransa, kwa kuukwamisha mpira wavuni kwa ufundi mkubwa baada ya mchezaji mwenzake ambaye naye amesajiliwa msimu huu Mesut Ozil kumpatia pasi safi kwenye dakika ya 81 na kuibuka kwa ushindi huo mwembamba wa bao 1-0.
AC Milan ambao walifunga Auxerre katika mchezo wa kwanza, walijikuta wakivutwa shati na Ajax ya Uholanzi kwa kutoka nao sare ya bao 1-1. Mounir El Hamdaoui ndiye aliyefunga bao la kuongoza Ajax dakika ya 23 akimalizia kazi nzuri iliyofanywa na Luis Suarez, lakini shujaa wa zamani wa Ajax Zlatan Ibrahimovic alisawazisha bao hilo dakika 15 baadae kwa kusaidiana vyema na aliyekuwa kipenzi cha mashabiki wa Uholanzi Clarence Seedorf.
AS Roma walituliza maumivu ya kufungwa na Bayern Munich katika mchezo wa kwanza wa kundi E kwa kuwafunga CFR Cluj mabao 2-1. Mabao hayakupatikana mpaka katikati ya kipindi cha pili, ambapo beki Philipe Mexes aliipatia timu yake bao la kuongoza kwa shuti kali dakika ya 69 na Marco Borriello aliongeza la pili dakika mbili baadae. Cluj walijibu mapigo dakika saba baadae wakati Ionut Rada alipotumbukiza nyavuni mpira wa kichwa na kupata bao lakufutia machozi.
Bayern walilikuja kutoka nyuma na kushinda mabao 2-1 dhidi ya Basel, ambao walianza kuongoza katika dakika ya 17 kwa bao lilifungwa na alexander Frei. Bayern walirudisha bao hilo kwa njia ya penati iliyofungwa na Bastian Schweinsteiger katika dakika ya 56, baada ya Thomas Muller kufanyiwa madhambi na Benjamin Huggel, na dakika moja kabla ya mpira kumalizika Schweinsteiger aliipatia timu yake bao la kuongoza.
Katika michezo mingine iliyochezwa jana Shakhtar Donetsk waliifunga Braga mabao 3-0 huku Spartak Moscow nao wakishinda mabao 3-0 dhidi ya Zilina.
Tuesday, September 28, 2010
GUARDIOLA AMTOA KAFARA MESSI.
MADRID, Hispania
MAJERUHI Lionel Messi ametajwa katika kikosi cha Barcelona kitakachokwenda Russia kuvaana na Rubin Karzan kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya uliopangwa kuchezwa leo.
Kocha wa Barcelona Pep Guardiola amebeba dhamana ya mwanasoka huyo bora wa dunia 2009, ambaye alitakuwa kukaa nje ya uwanja wiki mbili baada ya kuumia kifundo cha mguu.
Mshambuliaji huyo wa Argentina alitolewa nje kwa machela baada ya kuchezewa rafu mbaya na beki wa Atletico Madrid, Tomasz Ujfalusi raia wa Jamhuri ya Czech Septemba 19. Messi, tayari amekosa michezo miwili ya ligi.
Messi alianza mazoezi mepesi Ijumaa iliyopita lakini hakujumuishwa na wachezaji wenzake kabla ya kutangazwa mmoja wa wachezaji 19 watakaokwenda Russia. Guardiola atasafiri na beki wa Ufaransa, Eric Abidal aliyekosa mechi tatu kutokana na matatizo binafsi.
Barcelona inaongoza kundi D baada ya kupata ushindi mnono wa mabao 5-1 iliyopata katika mchezo wa kwanza ilipovaana na timu ya Ugiriki Panathinaikos 5-1 kwenye Uwanja wa Camp Nou. Mwaka jana, Barcelona ilikiona cha moto baada ya kunyukwa mabao 2-1 na Rubin Karzan.
MAJERUHI Lionel Messi ametajwa katika kikosi cha Barcelona kitakachokwenda Russia kuvaana na Rubin Karzan kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya uliopangwa kuchezwa leo.
Kocha wa Barcelona Pep Guardiola amebeba dhamana ya mwanasoka huyo bora wa dunia 2009, ambaye alitakuwa kukaa nje ya uwanja wiki mbili baada ya kuumia kifundo cha mguu.
Mshambuliaji huyo wa Argentina alitolewa nje kwa machela baada ya kuchezewa rafu mbaya na beki wa Atletico Madrid, Tomasz Ujfalusi raia wa Jamhuri ya Czech Septemba 19. Messi, tayari amekosa michezo miwili ya ligi.
Messi alianza mazoezi mepesi Ijumaa iliyopita lakini hakujumuishwa na wachezaji wenzake kabla ya kutangazwa mmoja wa wachezaji 19 watakaokwenda Russia. Guardiola atasafiri na beki wa Ufaransa, Eric Abidal aliyekosa mechi tatu kutokana na matatizo binafsi.
Barcelona inaongoza kundi D baada ya kupata ushindi mnono wa mabao 5-1 iliyopata katika mchezo wa kwanza ilipovaana na timu ya Ugiriki Panathinaikos 5-1 kwenye Uwanja wa Camp Nou. Mwaka jana, Barcelona ilikiona cha moto baada ya kunyukwa mabao 2-1 na Rubin Karzan.
ROONEY KUIKOSA VALENCIA.
LONDON, England
MANCHESTER United imepata pigo baada ya kuripotiwa taarifa kuwa mshambuliaji nguli Wayne Rooney atakosa mchezo muhimu wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Valencia uliopangwa kuchezwa leo nchini Hispania.
Rooney atalazimika kuangalia mchezo huo akiwa nyumbani na hatakwenda Hispania na kikosi hicho baada ya kuumia kifundo cha mguu katika mchezo walilazimisha sare mabao 2-2 na Bolton kwenye Uwanja wa Reebok.
Nguli huyo wa England, alitoka dakika 61 kupatiwa matibabu ya dharura baada ya kuumia. Mfungaji mabao huyo wa England ameshindwa kurejea katika kiwango chake tangu alipoumia katika mchezo wa ligi ya mabingwa Ulaya msimu uliopita katika mchezo dhidi ya Bayern Munich.
Mshambuliaji huyo alitoka baada ya kupata majeraha lakini kocha Sir Alex Ferguson alisema ana imani Rooney atacheza mchezo huo kwa madai hakupata maumivu makubwa kabla ya jana kuripotiwa taarifa hatacheza pambano hilo kwenye Uwanja wa Mestalla unaotumiwa na Valencia.
"Rooney hatakwenda Hispania wiki hii, meneja amegundua ana maumivu makali hivyo hatakuwa mmoja wa wachezaji watakaocheza dhidi ya Valencia, amepanga kumpumzisha ili kuangalia afya yake," kilisema chanzo cha habari ndani ya klabu hiyo.
Ferguson atalazimika kumtumia mshambuliaji mkongwe, Michael Owen kucheza 'pacha' na Dimitar Berbatov safu ya ushambuliaji. Nyota wamerejea katika viwango bora tangu kuanza msimu huu. Berbatov, alifunga mabao yote matatu katika mchezo ambao United ilishinda mabao 3-2 dhidi ya mahasimu wao Liverpool.
MANCHESTER United imepata pigo baada ya kuripotiwa taarifa kuwa mshambuliaji nguli Wayne Rooney atakosa mchezo muhimu wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Valencia uliopangwa kuchezwa leo nchini Hispania.
Rooney atalazimika kuangalia mchezo huo akiwa nyumbani na hatakwenda Hispania na kikosi hicho baada ya kuumia kifundo cha mguu katika mchezo walilazimisha sare mabao 2-2 na Bolton kwenye Uwanja wa Reebok.
Nguli huyo wa England, alitoka dakika 61 kupatiwa matibabu ya dharura baada ya kuumia. Mfungaji mabao huyo wa England ameshindwa kurejea katika kiwango chake tangu alipoumia katika mchezo wa ligi ya mabingwa Ulaya msimu uliopita katika mchezo dhidi ya Bayern Munich.
Mshambuliaji huyo alitoka baada ya kupata majeraha lakini kocha Sir Alex Ferguson alisema ana imani Rooney atacheza mchezo huo kwa madai hakupata maumivu makubwa kabla ya jana kuripotiwa taarifa hatacheza pambano hilo kwenye Uwanja wa Mestalla unaotumiwa na Valencia.
"Rooney hatakwenda Hispania wiki hii, meneja amegundua ana maumivu makali hivyo hatakuwa mmoja wa wachezaji watakaocheza dhidi ya Valencia, amepanga kumpumzisha ili kuangalia afya yake," kilisema chanzo cha habari ndani ya klabu hiyo.
Ferguson atalazimika kumtumia mshambuliaji mkongwe, Michael Owen kucheza 'pacha' na Dimitar Berbatov safu ya ushambuliaji. Nyota wamerejea katika viwango bora tangu kuanza msimu huu. Berbatov, alifunga mabao yote matatu katika mchezo ambao United ilishinda mabao 3-2 dhidi ya mahasimu wao Liverpool.
VAN GAAL AONGEZA MKATABA BAYERN.
BERLIN, Ujerumani
KOCHA wa Bayern Munich, Louis van Gaal ameongeza mkataba wa mwaka mmoja ambapo mkataba wake sasa utafikia ukingoni Juni 30, 2012.
Kocha huyo raia wa Uholanzi alitia saini mkataba huo juzi Basel, Uswis mji ambao Bayern Munich ilicheza mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya na FC Bassel.
Awali, kulikuwa na taarifa zisizo rasmi kuwa kocha huyo mkongwe, alikuwa kwenye hatihati ya kuongeza mkataba mpya baada ya Bayern Munich kuchapwa mabao 2-1 na Mainz Jumamosi iliyopita.
"Hatuwezi kubadili mwelekeo licha ya kufungwa, tuna imani kubwa na kocha Louis van Gaal. Amefanya kazi kubwa katika timu yetu ni mtu muhimu Bayern Munich," alisema mwenyekiti wa klabu hiyo Karl-Heinz Rummenigge.
Van Gaal mwenye miaka 59, aliipa Bayern Munich ubingwa wa Ligi Kuu Ujerumani mara mbili na Kombe la Ujerumani. Moja ya mafanikio makubwa aliyopata katika rekodi zake ni kuifikisha timu hiyo katika fainali za ligi ya mabingwa Ulaya ambapo timu ilichapwa mabao 2-0 dhidi ya Inter Milan.
KOCHA wa Bayern Munich, Louis van Gaal ameongeza mkataba wa mwaka mmoja ambapo mkataba wake sasa utafikia ukingoni Juni 30, 2012.
Kocha huyo raia wa Uholanzi alitia saini mkataba huo juzi Basel, Uswis mji ambao Bayern Munich ilicheza mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya na FC Bassel.
Awali, kulikuwa na taarifa zisizo rasmi kuwa kocha huyo mkongwe, alikuwa kwenye hatihati ya kuongeza mkataba mpya baada ya Bayern Munich kuchapwa mabao 2-1 na Mainz Jumamosi iliyopita.
"Hatuwezi kubadili mwelekeo licha ya kufungwa, tuna imani kubwa na kocha Louis van Gaal. Amefanya kazi kubwa katika timu yetu ni mtu muhimu Bayern Munich," alisema mwenyekiti wa klabu hiyo Karl-Heinz Rummenigge.
Van Gaal mwenye miaka 59, aliipa Bayern Munich ubingwa wa Ligi Kuu Ujerumani mara mbili na Kombe la Ujerumani. Moja ya mafanikio makubwa aliyopata katika rekodi zake ni kuifikisha timu hiyo katika fainali za ligi ya mabingwa Ulaya ambapo timu ilichapwa mabao 2-0 dhidi ya Inter Milan.
RADEBE AJIPIGIA DEBE KUINOA BAFANA BAFANA.
JOHANNESBURG, Afrika Kusini.
NAHODHA wa zamani wa Afrika Kusini, 'Bafana Bafana' amesema ana kiu ya kufundisha timu ya taifa ya nchi hiyo baada ya kucheza kwa kiwango bora Ulaya kabla ya kustaafu soka.
Beki huyo wa kati, alikuwa nahodha wa kwanza mweusi kuongoza klabu ya Leeds United iliyokuwa ligi kuu England na alikuwa mmoja wa mabeki hodari waliong'ara miaka ya 1990.
Radebe alisema ndoto yake ni kuinoa Leeds au Bafana Bafana. Mchezaji huyo aliyecheza mechi 200 za ligi akiwa na klabu yake alidai ni jambo la kufurahisha kurejea uwanjani baada ya kuwa nje ya mchezo muda mrefu akifanya shughuli zake nje ya mchezo wa soka.
"Niliwahi kutamka kwamba baada ya kustaafu soka sikuwahi kufundisha timu yoyote, lakini endapo nitaamua kurejea uwanjani msimamo wangu ni kuinoa Leeds United pekee. Nyingine itakuwa timu ya taifa ya Afrika Kusini," alisema Radebe.
Mchezaji huyo alidokeza ana mapenzi na Leeds iliyompa umaarufu katika mchezo wa soka duniani na Bafana Bafana kwa kuwa ni timu ya taifa lake. Radebe alikuwa miongoni mwa watu zaidi ya 37000 waliojitokeza makao makuu Elland Road, alisema atakuwa radhi kuzinoa kwa hisani ikiwa ni sehemu ya mchango wake.
NAHODHA wa zamani wa Afrika Kusini, 'Bafana Bafana' amesema ana kiu ya kufundisha timu ya taifa ya nchi hiyo baada ya kucheza kwa kiwango bora Ulaya kabla ya kustaafu soka.
Beki huyo wa kati, alikuwa nahodha wa kwanza mweusi kuongoza klabu ya Leeds United iliyokuwa ligi kuu England na alikuwa mmoja wa mabeki hodari waliong'ara miaka ya 1990.
Radebe alisema ndoto yake ni kuinoa Leeds au Bafana Bafana. Mchezaji huyo aliyecheza mechi 200 za ligi akiwa na klabu yake alidai ni jambo la kufurahisha kurejea uwanjani baada ya kuwa nje ya mchezo muda mrefu akifanya shughuli zake nje ya mchezo wa soka.
"Niliwahi kutamka kwamba baada ya kustaafu soka sikuwahi kufundisha timu yoyote, lakini endapo nitaamua kurejea uwanjani msimamo wangu ni kuinoa Leeds United pekee. Nyingine itakuwa timu ya taifa ya Afrika Kusini," alisema Radebe.
Mchezaji huyo alidokeza ana mapenzi na Leeds iliyompa umaarufu katika mchezo wa soka duniani na Bafana Bafana kwa kuwa ni timu ya taifa lake. Radebe alikuwa miongoni mwa watu zaidi ya 37000 waliojitokeza makao makuu Elland Road, alisema atakuwa radhi kuzinoa kwa hisani ikiwa ni sehemu ya mchango wake.
Monday, September 27, 2010
ALMUNIA KUKOSA MECHI YA LIGI YA MABINGWA ULAYA.
KOCHA wa Arsenal Arsene Wenger amesema kuwa mlinda mlango wake namba moja katika kikosi hicho Manuel Almunia ni majeruhi na hatakuwemo katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya huko FK Partizan wiki hii.
Mlinda mlango huyo kutoka Hispania aliumia kisukusuku au kipepsi Jumamosi wakati timu hiyo ilipokubali kichapo dhidi ya timu ya West Bromwich Albion, na nafasi yake inaweza kuzibwa na Lukasz Fabianski.
"Tutamkosa Almunia. Ana matatizo ya kisukusuku. Aliyapata wakati akidaka penati Jumamosi," alisema Wenger. "Pia Kieran Gibbs atafanyiwa majaribio katika mazoezi leo."
Almunia amekuwa akilaumiwa kutokana na mchezo wa Jumamosi ambapo anatuhumiwa kufanya makosa mawili ambayo yaliigharimu timu katika kipindi cha pili lakini Wenger amekanusha uvumi huo akisema angemchagua katika kikosi chake kama asingekuwa ameumia.
"Hapana," alijibu Wenger alipoulizwa kama alimuacha Almunia kutokana na makosa aliyofanya.
"Siku zote wakati timu inaposhindwa wa kwanza kulaumiwa anakuwa golikipa. Lakini huwa tunashinda pamoja na kushindwa pamoja hata kama watu wanakiri alifanya makosa tulipofungwa bao la pili." alimalizia Wenger.
Mlinda mlango huyo kutoka Hispania aliumia kisukusuku au kipepsi Jumamosi wakati timu hiyo ilipokubali kichapo dhidi ya timu ya West Bromwich Albion, na nafasi yake inaweza kuzibwa na Lukasz Fabianski.
"Tutamkosa Almunia. Ana matatizo ya kisukusuku. Aliyapata wakati akidaka penati Jumamosi," alisema Wenger. "Pia Kieran Gibbs atafanyiwa majaribio katika mazoezi leo."
Almunia amekuwa akilaumiwa kutokana na mchezo wa Jumamosi ambapo anatuhumiwa kufanya makosa mawili ambayo yaliigharimu timu katika kipindi cha pili lakini Wenger amekanusha uvumi huo akisema angemchagua katika kikosi chake kama asingekuwa ameumia.
"Hapana," alijibu Wenger alipoulizwa kama alimuacha Almunia kutokana na makosa aliyofanya.
"Siku zote wakati timu inaposhindwa wa kwanza kulaumiwa anakuwa golikipa. Lakini huwa tunashinda pamoja na kushindwa pamoja hata kama watu wanakiri alifanya makosa tulipofungwa bao la pili." alimalizia Wenger.
"NIMERIDHISHWA NA MATOKEO TULIYOPATA." FERGUSON.
KOCHA wa Manchester United Sir Alex Ferguson anaamini kuwa kikosi chake kilifanya vizuri katika mchezo ambao walitoka sare ya mabao 2-2 dhidi ya Bolton Wanderers Jumapili.
United walikuwa nyuma mara mbili ya kikosi cha Owen Coyle, lakini bao la Michael Owen dakika 16 kabla ya mpira kumalizika liliokoa na kuifanya timu hizo kugawana pointi.
Kiwango cha United wanapocheza michezo ya ugenini kimemuogopesha Ferguson. Ambapo wametoa sare michezo yao mitatu waliyocheza ugenini msimu huu, mabingwa hao zamani wanapata wakati mgumu kuwasogelea Chelsea katika hatua hizi za mwanzoni mwa msimu.
Baada ya kufungwa bao la dakika ya 10 toka mchezo ulivyoanza, United walisawazisha bao hilo kwa juhudi binafsi zilizofanywa na mchezaji Nani. Lakini United walijikuta tena wakiwa nyuma katika kipindi cha pili kabla ya Owen hajaokoa jahazi kwa bao la kichwa kufanya mchezo huo uishe kwa sare.
"Katika kipindi cha tulitakiwa kufanya vizuri zaidi," alisema Ferguson.
"Lakini tulitengeneza nafasi nzuri na tulicheza mchezo wa kuvutia.
"Bolton walimiliki mchezo, lakini tulicheza na pindi tulipomiliki mchezo tulitengeneza nafasi.
"Kuwa nyuma mara mbili katika mechi za ugenini ni ngumu, lakini tumeonyesha kwamba tunaweza. nafikiri ni matokeo ya kuridhisha."
Pamoja na kuwa na matokeo yasiyo ya kuridhisha wanapocheza ugenini, Ferguson naamini ligi inaanza kuwa ngumu na kikosi chake kitapata nafasi huko mbeleni ya kuwakamata Chelsea waoshilia usukani kwa sasa.
"Timu huwa inapoteza pointi usipotegemea," alisema Ferguson.
"Katika michezo ya ugenini tumeshinda mabao saba na tumepata pointi tatu tu, hiyo inaonyesha jinsi gani ligi ilivyo ngumu, lakini tumeonyesha kwamba tunaweza, kitu ambacho ni kizuri."
United walikuwa nyuma mara mbili ya kikosi cha Owen Coyle, lakini bao la Michael Owen dakika 16 kabla ya mpira kumalizika liliokoa na kuifanya timu hizo kugawana pointi.
Kiwango cha United wanapocheza michezo ya ugenini kimemuogopesha Ferguson. Ambapo wametoa sare michezo yao mitatu waliyocheza ugenini msimu huu, mabingwa hao zamani wanapata wakati mgumu kuwasogelea Chelsea katika hatua hizi za mwanzoni mwa msimu.
Baada ya kufungwa bao la dakika ya 10 toka mchezo ulivyoanza, United walisawazisha bao hilo kwa juhudi binafsi zilizofanywa na mchezaji Nani. Lakini United walijikuta tena wakiwa nyuma katika kipindi cha pili kabla ya Owen hajaokoa jahazi kwa bao la kichwa kufanya mchezo huo uishe kwa sare.
"Katika kipindi cha tulitakiwa kufanya vizuri zaidi," alisema Ferguson.
"Lakini tulitengeneza nafasi nzuri na tulicheza mchezo wa kuvutia.
"Bolton walimiliki mchezo, lakini tulicheza na pindi tulipomiliki mchezo tulitengeneza nafasi.
"Kuwa nyuma mara mbili katika mechi za ugenini ni ngumu, lakini tumeonyesha kwamba tunaweza. nafikiri ni matokeo ya kuridhisha."
Pamoja na kuwa na matokeo yasiyo ya kuridhisha wanapocheza ugenini, Ferguson naamini ligi inaanza kuwa ngumu na kikosi chake kitapata nafasi huko mbeleni ya kuwakamata Chelsea waoshilia usukani kwa sasa.
"Timu huwa inapoteza pointi usipotegemea," alisema Ferguson.
"Katika michezo ya ugenini tumeshinda mabao saba na tumepata pointi tatu tu, hiyo inaonyesha jinsi gani ligi ilivyo ngumu, lakini tumeonyesha kwamba tunaweza, kitu ambacho ni kizuri."
KOCHA WA SEVILLA ATUPIWA VIRAGO.
KLABU Sevilla imemtimua kocha wake Antonio Alvarez baada ya kuanza vibaya msimu wa Ligi Kuu ya Hispania kwa kupoteza mchezo mwingine dhidi ya Hercules kwa mabao 2-0, ambapo tayari timu hiyo imemteua Ramon Sanchez kushika nafasi hiyo kwa mujibu taarifa iliyotolewa na tovuti ya klabu hiyo.
Alvarez amekiongoza kikosi hicho kwa muda wa miezi sita tu toka alipochukua mikoba hiyo kutoka kwa Manolo Jimenez baada ya timu hiyo kutolewa katika ligi ya mabingwa na pia kupoteza michezo mingi katika ligi kuu ambapo katika michezo 14 walifanikiwa kushinda minne tu.
Pamoja na kutetea ubingwa wa kombe la mfalme msimu uliopita na kushika nafasi ya nne katika siku za mwisho mwishoni mwa msimu uliopita, Alvarez ameonyesha kushindwa kutafuta makali ya kikosi hicho msimu huu.
Nafasi yake inachukuliwa na Manzano kocha ambaye kidogo aitoe Sevilla katika Ligi ya Mabingwa msimu uliopita akiwa na Malorca ambapo aliachana na klabu hiyo kwa kushindwa kukubaliana baadhi ya mambo.
Kocha huyo mwenye umri wa miaka 54 anatarajiwa kuanza kukinoa kikosi hicho leo jioni.
Alvarez amekiongoza kikosi hicho kwa muda wa miezi sita tu toka alipochukua mikoba hiyo kutoka kwa Manolo Jimenez baada ya timu hiyo kutolewa katika ligi ya mabingwa na pia kupoteza michezo mingi katika ligi kuu ambapo katika michezo 14 walifanikiwa kushinda minne tu.
Pamoja na kutetea ubingwa wa kombe la mfalme msimu uliopita na kushika nafasi ya nne katika siku za mwisho mwishoni mwa msimu uliopita, Alvarez ameonyesha kushindwa kutafuta makali ya kikosi hicho msimu huu.
Nafasi yake inachukuliwa na Manzano kocha ambaye kidogo aitoe Sevilla katika Ligi ya Mabingwa msimu uliopita akiwa na Malorca ambapo aliachana na klabu hiyo kwa kushindwa kukubaliana baadhi ya mambo.
Kocha huyo mwenye umri wa miaka 54 anatarajiwa kuanza kukinoa kikosi hicho leo jioni.
MESSI KUWEMO KWENYE BENCHI LA AKIBA JUMATANO.
KUPONA haraka kwa mshambuliaji nyota wa Barcelona Lionel Messi aliyeumia wakati timu yake hiyo ilipocheza na Atletico Madrid kumewashangaza wengi, ambapo sasa shujaa huyo kutoka Argentina anatarajiwa kuwemo katika benchi la wachezaji wa akiba katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa dhidi ya Rubin Kazan, Jumatano.
Taarifa iliyotolewa na gazeti moja Hispania ilisema kuwa Messi hataanza katika kikosi cha kwanza huko Russia lakini atakuwa tayari kucheza pindi atakapohitajika katika mchezo huo.
Hata hivyo mchezaji huyo anategemewa kuanza katika kikosi cha kwanza katika mchezo wa Kombe la Ligi dhidi Mallorca mwishoni mwa wiki ijayo.
Messi pia ameitwa katika kikosi cha timu ya Taifa ya Argentina na kocha Sergio Batista wakati timu itapocheza mchezo wa kimataifa wa kirafiki dhidi ya Japan Octoba.
Taarifa iliyotolewa na gazeti moja Hispania ilisema kuwa Messi hataanza katika kikosi cha kwanza huko Russia lakini atakuwa tayari kucheza pindi atakapohitajika katika mchezo huo.
Hata hivyo mchezaji huyo anategemewa kuanza katika kikosi cha kwanza katika mchezo wa Kombe la Ligi dhidi Mallorca mwishoni mwa wiki ijayo.
Messi pia ameitwa katika kikosi cha timu ya Taifa ya Argentina na kocha Sergio Batista wakati timu itapocheza mchezo wa kimataifa wa kirafiki dhidi ya Japan Octoba.
Sunday, September 26, 2010
SAFU YA USHAMBULIAJI IMEKUWA BUTU.
BEKI wa Real Madrid Alvaro Arbeloa amesema timu yake inahitaji kuwa makini katika umaliziaji baada ya timu hiyo kutoka suluhu 0-0 na timu Lavante juzi usiku.
Pamoja na kazi kubwa iliyokuwa ikifanywa na Cristiano Ronaldo, timu hiyo ilishindwa kupata bao la ushindi na mwisho wa mchezo walilazimika kugawana pointi.
Beki huyo wa zamani wa Liverpool anaamini kuwa ukata wa mabao unaoikabili timu yake ndio umechangia kwa kiasi kikubwa kukosa pointi tatu katika mchezo huo.
"Tunahitaji kuongeza umakini na utulivu pindi tunapopata nafasi tunazotengeneza. Tulikuwa tukitarajia kwamba Levante watatupa mchezo mgumu lakini hatukuwa tumetulia vya kutosha kutafuta pointi tatu." alisema Arbeloa
"Tunahitaji kuwa na ngome imara. Na kitu muhimu zaidi ni kwamba timu ina ngome imara na tunahitaji kujitahidi katika ushambuliaji tu."
Pamoja na kazi kubwa iliyokuwa ikifanywa na Cristiano Ronaldo, timu hiyo ilishindwa kupata bao la ushindi na mwisho wa mchezo walilazimika kugawana pointi.
Beki huyo wa zamani wa Liverpool anaamini kuwa ukata wa mabao unaoikabili timu yake ndio umechangia kwa kiasi kikubwa kukosa pointi tatu katika mchezo huo.
"Tunahitaji kuongeza umakini na utulivu pindi tunapopata nafasi tunazotengeneza. Tulikuwa tukitarajia kwamba Levante watatupa mchezo mgumu lakini hatukuwa tumetulia vya kutosha kutafuta pointi tatu." alisema Arbeloa
"Tunahitaji kuwa na ngome imara. Na kitu muhimu zaidi ni kwamba timu ina ngome imara na tunahitaji kujitahidi katika ushambuliaji tu."
NIRIDHISHWA NA MATOKEO TULIOYOPATA.
KOCHA wa Barcelona Pep Guardiola ameridhishwa na kiwango kilichoonyeshwa na wachezaji wakati wa mchezo ambao timu hiyo ilishinda mabao 3-1 dhidi ya timu ya Athletic Bilbao.
Akiwa amewapanga, Seydou Keita, Xavi na Sergio Busquets ambao walifanya kazi nzuri kuhakikisha ushindi unapatikana na kuwafanya kujikita nafasi ya pili nyuma ya Valencia ambao ndio wanaongoza ligi kwa sasa.
Akizungumza na waandshi wa habari baada ya mchezo huo, Guardiola alikiri kuwa amefurahishwa kuondoka katika mji wa Basque akiwa na pointi zote tatu.
"Nafurahi nimeshinda katika sehemu ambayo ni ngumu kuja, ukitulinganisha na Real Madrid utaona hatulingani kwa ubora, huwa tunajitahidi kuhakikisha tunapata pointi na ndicho tunachojaribu kufanya." alisema Guardiola.
David Villa na Fernando Amorebeita walitolewa katika mchezo huo uliokuwa wa vuta ni kuvute, lakini Guardiola hajazungumzia lolote kuhusu hilo mwamuzi wa mchezo huo.
"Tukio lilitokea haraka sana na ningipenda kulitizama tena katika luninga." alisema Guardiola.
"Watu wanalipia tiketi na wana uhuru wa kuimba na kupiga makofi kwa ajili ya pesa zao. Mashabiki wa Hispania wana uelewa na mpira wa miguu." alimalizia Guardiola.
Akiwa amewapanga, Seydou Keita, Xavi na Sergio Busquets ambao walifanya kazi nzuri kuhakikisha ushindi unapatikana na kuwafanya kujikita nafasi ya pili nyuma ya Valencia ambao ndio wanaongoza ligi kwa sasa.
Akizungumza na waandshi wa habari baada ya mchezo huo, Guardiola alikiri kuwa amefurahishwa kuondoka katika mji wa Basque akiwa na pointi zote tatu.
"Nafurahi nimeshinda katika sehemu ambayo ni ngumu kuja, ukitulinganisha na Real Madrid utaona hatulingani kwa ubora, huwa tunajitahidi kuhakikisha tunapata pointi na ndicho tunachojaribu kufanya." alisema Guardiola.
David Villa na Fernando Amorebeita walitolewa katika mchezo huo uliokuwa wa vuta ni kuvute, lakini Guardiola hajazungumzia lolote kuhusu hilo mwamuzi wa mchezo huo.
"Tukio lilitokea haraka sana na ningipenda kulitizama tena katika luninga." alisema Guardiola.
"Watu wanalipia tiketi na wana uhuru wa kuimba na kupiga makofi kwa ajili ya pesa zao. Mashabiki wa Hispania wana uelewa na mpira wa miguu." alimalizia Guardiola.
Friday, September 24, 2010
NEYMAR, LUCIO, MAICON NJE BRAZIL.
REO DE JENEIRO, Brazil.
KOCHA wa Brazil Mano Menezes ametangaza kikosi cha wachezaji 23 kwa ajili mechi mbili za kimataifa zinazotarajiwa kufanyika Octoba 6 na 13 mwaka huu.
Kwa mshangao wa wengi Menezes amemuacha katika kikosi hicho mchezaji chipukizi machachari Neymar anayechezea klabu ya Santos kufuatia mshambuliaji huyo kutoonyesha kiwango cha kuvutia pamoja na matukio yake ya nje ya uwanja.
"Nataka kuwa makini katika kufikiri jinsi ninavyofanya kazi. Siku tumekuwa tukisema mchezaji ataitwa kwa sababu ya kiwango chake atakachokionyesha uwanjani. Neymar akicheza chini ya kiwango katika kipindi cha hivi karibuni na pia ana matatizo yake mengine nje ya uwanja," alisema Menezes.
"Tumeamua kuliacha tatizo hilo nje ya kikosi hiki ndio maana sikumwita. Tunafikiri kuwa tunafikisha ujumbe unaoeleweka ili kila mmoja ajue kitu gani kinaendelea katika akili zetu.
"Lakini wote tunakubaliana na kiwango bora alichoonyesha katika miezi ya karibuni kabla hajakumbwa na matatizo. Na kama akirudi katika kiwango hicho nitamrudisha katika kikosi changu."
Mshambuliaji wa AC Milan Ronaldinho, ambaye amekuwa akifanya juhudi kubwa ili arudi katika kikosi hicho naye ameachwa, wakati wachezaji kama Luis Fabiano wa Sevilla, mabeki wa Inter Maicon na Lucio, kiungo Felipe Melo na mchezaji wa Wolfburg Diego nao hawakujumuishwa katika kikosi hicho.
Kikosi kamili kitakuwa kama ifuatavyo na timu wanazotoka katuika mabano:-
Magolikipa: Victor (Gremio), Jefferson (Botafogo), Neto (Atletico Paranaense)
Mabeki: Daniel Alves (Barcelona), Mariano (Fluminense), Alex (Chelsea), Thiago Silva (Milan), David Luiz (Benfica), Andre Santos (Fenerbahce), Adriano (Barcelona)
Viungo: Wesley (Werder Bremen), Sandro (Tottenham), Ramires (Chelsea), Philippe Coutinho (Inter), Lucas (Liverpool), Giuliano (Internacional), Elias (Corinthians), Carlos Eduardo (Rubin Kazan)
Washambuliaji: Robinho (Milan), Alexandre Pato (Milan), Nilmar (Villarreal), Andre (Dynamo Kiev)
KOCHA wa Brazil Mano Menezes ametangaza kikosi cha wachezaji 23 kwa ajili mechi mbili za kimataifa zinazotarajiwa kufanyika Octoba 6 na 13 mwaka huu.
Kwa mshangao wa wengi Menezes amemuacha katika kikosi hicho mchezaji chipukizi machachari Neymar anayechezea klabu ya Santos kufuatia mshambuliaji huyo kutoonyesha kiwango cha kuvutia pamoja na matukio yake ya nje ya uwanja.
"Nataka kuwa makini katika kufikiri jinsi ninavyofanya kazi. Siku tumekuwa tukisema mchezaji ataitwa kwa sababu ya kiwango chake atakachokionyesha uwanjani. Neymar akicheza chini ya kiwango katika kipindi cha hivi karibuni na pia ana matatizo yake mengine nje ya uwanja," alisema Menezes.
"Tumeamua kuliacha tatizo hilo nje ya kikosi hiki ndio maana sikumwita. Tunafikiri kuwa tunafikisha ujumbe unaoeleweka ili kila mmoja ajue kitu gani kinaendelea katika akili zetu.
"Lakini wote tunakubaliana na kiwango bora alichoonyesha katika miezi ya karibuni kabla hajakumbwa na matatizo. Na kama akirudi katika kiwango hicho nitamrudisha katika kikosi changu."
Mshambuliaji wa AC Milan Ronaldinho, ambaye amekuwa akifanya juhudi kubwa ili arudi katika kikosi hicho naye ameachwa, wakati wachezaji kama Luis Fabiano wa Sevilla, mabeki wa Inter Maicon na Lucio, kiungo Felipe Melo na mchezaji wa Wolfburg Diego nao hawakujumuishwa katika kikosi hicho.
Kikosi kamili kitakuwa kama ifuatavyo na timu wanazotoka katuika mabano:-
Magolikipa: Victor (Gremio), Jefferson (Botafogo), Neto (Atletico Paranaense)
Mabeki: Daniel Alves (Barcelona), Mariano (Fluminense), Alex (Chelsea), Thiago Silva (Milan), David Luiz (Benfica), Andre Santos (Fenerbahce), Adriano (Barcelona)
Viungo: Wesley (Werder Bremen), Sandro (Tottenham), Ramires (Chelsea), Philippe Coutinho (Inter), Lucas (Liverpool), Giuliano (Internacional), Elias (Corinthians), Carlos Eduardo (Rubin Kazan)
Washambuliaji: Robinho (Milan), Alexandre Pato (Milan), Nilmar (Villarreal), Andre (Dynamo Kiev)
YANGA YALAANI KUPIGWA KWA PAPIC.
UONGOZI wa klabu ya Yanga umesikitishwa na kulaani vurugu zilizosababishwa na mmoja wa viongozi wa wa timu ya Kagera Sugar Mohamed Hussein katika mchezo baina yake na timu hiyo ulichezwa katika Uwanja wa Kaitaba, Kagera ambapo Yanga ilishinda mabao 2-0.
Kauli hiyo imekuja kufuatia Hussein kuonekana akimpiga kwa makusudi Kocha Mkuu wa Yanga Kostadin Papic mara baada ya mpambano wa ligi kuu baina ya timu hizo kumalizika.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Ofisa Habari wa Yanga, Luis Sendeu alisema kitendo kilichofanywa na kiongozi huyo hakikuwa cha kiungwana na kinafaa kulaaniwa na wapenda michezo wote hapa nchini.
Alisema Papic alipigwa wakati akimalizia kuwapongeza wachezaji na waamuzi mara baada ya mchezo huo kumalizika Hussein alipomrushia ngumi kocha huyo na kusababisha vurugu kwa mashabiki walikasirishwa na kitndo hicho.
Alisema uongozi wa klabu hiyo tayari umeliandikia barua Shirikisho la Soka nchini (TFF) juu ya vurugu zilizoanzishwa na kiongozi huyo kwani zingeweza kuleta maafa kwa mashabiki waliohudhuria pambano hilo na kuomba hatua kali za kinidhamu zichukuliwe.
Alisema sio mara ya kwanza kwa Hussein kufanya vurugu katika michezo ya Ligi Kuu kwani aliwahi kufanya vurugu katika miaka ya karibuni katika Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam hali iliyopekea kutolewa nje na FFU.
"Ni matumaini yetu TFF italichunguza tukio hilo kwa umakini na kuchukua hatua kali za kinidhamu kwa kiongozi huyo." alimalizia Sendeu.
Kauli hiyo imekuja kufuatia Hussein kuonekana akimpiga kwa makusudi Kocha Mkuu wa Yanga Kostadin Papic mara baada ya mpambano wa ligi kuu baina ya timu hizo kumalizika.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Ofisa Habari wa Yanga, Luis Sendeu alisema kitendo kilichofanywa na kiongozi huyo hakikuwa cha kiungwana na kinafaa kulaaniwa na wapenda michezo wote hapa nchini.
Alisema Papic alipigwa wakati akimalizia kuwapongeza wachezaji na waamuzi mara baada ya mchezo huo kumalizika Hussein alipomrushia ngumi kocha huyo na kusababisha vurugu kwa mashabiki walikasirishwa na kitndo hicho.
Alisema uongozi wa klabu hiyo tayari umeliandikia barua Shirikisho la Soka nchini (TFF) juu ya vurugu zilizoanzishwa na kiongozi huyo kwani zingeweza kuleta maafa kwa mashabiki waliohudhuria pambano hilo na kuomba hatua kali za kinidhamu zichukuliwe.
Alisema sio mara ya kwanza kwa Hussein kufanya vurugu katika michezo ya Ligi Kuu kwani aliwahi kufanya vurugu katika miaka ya karibuni katika Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam hali iliyopekea kutolewa nje na FFU.
"Ni matumaini yetu TFF italichunguza tukio hilo kwa umakini na kuchukua hatua kali za kinidhamu kwa kiongozi huyo." alimalizia Sendeu.
ARSENAL YATANGAZA KUPATA FAIDA.
LONDON, England.
KLABU ya soka ya Arsenal imetangaza kupata faida ya kiasi cha paundi
milioni 56 kwa mwaka ulioishia Mei 31, 2010.
Faida hiyo imekuja kutokana na vitga uchumi vya klabu hiyo, ambapo
klabu hiyo inayotokea Kaskazini mwa London imelipa deni la nyumba za
kupanga ilizojenga Highbury miezi sita kabla ya tarehe ya mwisho ya
kurudisha deni hilo.
Mwaka ulipita klabu hiyo ilitangaza faida ya kiasi cha paundi milioni 45,
ambayo ilikuwa kwa kiasi cha asilimia 24 kulinganisha na mwaka huo
uliopita. Mwaka huu klabu hiyo imetangaza faida ambayo imekuwa kwa
asilimia 18.6 ya kiasi hicho kilichopatikana.
Madeni ambayo kutokana na vitega uchumi vya biashara sio tu kwamba
wamelipa lakini pia vimetengeza faida. Nyumba za kupanga zilizopo
Highbury Square na nyingine zilizopo Queensland Road zimeingiza kiasi
kikubwa.
Klabu pia imepata faida kwa kuuza wachezaji, kiasi ambacho ni paundi
milioni 13.6 kutopkana na mauzo ya wachezaji Kolo Toure na Emmanuel
Adebayor kiasi ambacho kimeongezeka ikilinganishwa na mwaka uliopita
ambapo walipata paundi milioni 2.9.
KLABU ya soka ya Arsenal imetangaza kupata faida ya kiasi cha paundi
milioni 56 kwa mwaka ulioishia Mei 31, 2010.
Faida hiyo imekuja kutokana na vitga uchumi vya klabu hiyo, ambapo
klabu hiyo inayotokea Kaskazini mwa London imelipa deni la nyumba za
kupanga ilizojenga Highbury miezi sita kabla ya tarehe ya mwisho ya
kurudisha deni hilo.
Mwaka ulipita klabu hiyo ilitangaza faida ya kiasi cha paundi milioni 45,
ambayo ilikuwa kwa kiasi cha asilimia 24 kulinganisha na mwaka huo
uliopita. Mwaka huu klabu hiyo imetangaza faida ambayo imekuwa kwa
asilimia 18.6 ya kiasi hicho kilichopatikana.
Madeni ambayo kutokana na vitega uchumi vya biashara sio tu kwamba
wamelipa lakini pia vimetengeza faida. Nyumba za kupanga zilizopo
Highbury Square na nyingine zilizopo Queensland Road zimeingiza kiasi
kikubwa.
Klabu pia imepata faida kwa kuuza wachezaji, kiasi ambacho ni paundi
milioni 13.6 kutopkana na mauzo ya wachezaji Kolo Toure na Emmanuel
Adebayor kiasi ambacho kimeongezeka ikilinganishwa na mwaka uliopita
ambapo walipata paundi milioni 2.9.
KIKOSI CHA NIGERIA HIKI HAPA.
LAGOS, Nigeria
NIGERIA imemtema beki nguli Danny Shittu katika kikosi cha wachezaji 30 waliotangazwa kwa ajili ya mechi za kufuzu fainali za Kombe la Mataifa Afrika 2012 zilizopangwa kuchezwa nchini Equatorial Guinea na Gabon.
Beki huyo alikuwemo katika kikosi kilichocheza fainali za Kombe la Mataifa Afrika nchini Angola na Kombe la Dunia Afrika Kusini 2010, ametemwa muda mfupi kutokana na kutokuwa na timu ya kuitumikia. Shitttu alijiengua klabu ya Bolton Wanderers ya England.
Nigeria imeita nyota wake wengi waliokwenda Afrika Kusini ambao ni Taye Taiwo, Obinna Nsofor, Dele Adeleye, Yusuf Ayila na kiungo wa Fulham Dickson Etuhu ambaye alikosa mchezo wa kwanza timu hiyo ilipomenyana na Madagascar baada ya kuumia kifundo cha mguu.
Kikosi kamili, makipa Vincent Enyeama (Hapoel Tel Aviv/ISR), Dele Aiyenugba (Bnei-Yehuda/ISR), Bassey Akpan (Bayelsa United) na Chigozie Agbim wa Warri Wolves. Mabeki, Chidi Odiah (CSKA Moscow/RUS), Dele Adeleye (Metalurh Donetsk/UKR), Taye Taiwo (Olympique Marseille/FRA), Emmanuel Anyanwu, Emeka Anyanwu na Valentine Nwabili kutoka Enyimba.
Wengine ni beki mkongwe, Joseph Yobo (Fenerbache/TUR), Ugwu Uwadiegwu (Enugu Rangers), Ikechukwu ThankGod (Heartland), Chibuzor Okonkwo wa klabu ya Bayelsa United. Viungo, John Obi Mikel (Chelsea/ENG), Kalu Uche (Almeria/SPA), Otekpa Eneji (Enyimba), Dickson Etuhu (Fulham/ENG), Sunday Stephen (Valencia/SPA), Yusuf Ayila (Dynamo Kiev/UKR), Daddy Bazuaye (Enyimba), Ayo Saka (Ocean Boys) na John Nnam wa Enugu Rangers.
Washambuliaji, Obinna Nsofor (West Ham/ENG), Ahmed Musa (Kano Pillars), Obafemi Martins (Rubin Kazan/RUS), Osaze Odemwingie (West Bromwich Albion/ENG), Michael Eneramo (Esperance/TUN), John Owoeri (Heartland), Moses Bunde kutoka Lobi Stars.
NIGERIA imemtema beki nguli Danny Shittu katika kikosi cha wachezaji 30 waliotangazwa kwa ajili ya mechi za kufuzu fainali za Kombe la Mataifa Afrika 2012 zilizopangwa kuchezwa nchini Equatorial Guinea na Gabon.
Beki huyo alikuwemo katika kikosi kilichocheza fainali za Kombe la Mataifa Afrika nchini Angola na Kombe la Dunia Afrika Kusini 2010, ametemwa muda mfupi kutokana na kutokuwa na timu ya kuitumikia. Shitttu alijiengua klabu ya Bolton Wanderers ya England.
Nigeria imeita nyota wake wengi waliokwenda Afrika Kusini ambao ni Taye Taiwo, Obinna Nsofor, Dele Adeleye, Yusuf Ayila na kiungo wa Fulham Dickson Etuhu ambaye alikosa mchezo wa kwanza timu hiyo ilipomenyana na Madagascar baada ya kuumia kifundo cha mguu.
Kikosi kamili, makipa Vincent Enyeama (Hapoel Tel Aviv/ISR), Dele Aiyenugba (Bnei-Yehuda/ISR), Bassey Akpan (Bayelsa United) na Chigozie Agbim wa Warri Wolves. Mabeki, Chidi Odiah (CSKA Moscow/RUS), Dele Adeleye (Metalurh Donetsk/UKR), Taye Taiwo (Olympique Marseille/FRA), Emmanuel Anyanwu, Emeka Anyanwu na Valentine Nwabili kutoka Enyimba.
Wengine ni beki mkongwe, Joseph Yobo (Fenerbache/TUR), Ugwu Uwadiegwu (Enugu Rangers), Ikechukwu ThankGod (Heartland), Chibuzor Okonkwo wa klabu ya Bayelsa United. Viungo, John Obi Mikel (Chelsea/ENG), Kalu Uche (Almeria/SPA), Otekpa Eneji (Enyimba), Dickson Etuhu (Fulham/ENG), Sunday Stephen (Valencia/SPA), Yusuf Ayila (Dynamo Kiev/UKR), Daddy Bazuaye (Enyimba), Ayo Saka (Ocean Boys) na John Nnam wa Enugu Rangers.
Washambuliaji, Obinna Nsofor (West Ham/ENG), Ahmed Musa (Kano Pillars), Obafemi Martins (Rubin Kazan/RUS), Osaze Odemwingie (West Bromwich Albion/ENG), Michael Eneramo (Esperance/TUN), John Owoeri (Heartland), Moses Bunde kutoka Lobi Stars.
HATUWEZI KUTWAA UBINGWA WA ENGLAND.
LONDON, England
NAHODHA wa Liverpool, Steven Gerrard ametoa kauli nzito baada ya kukiri hawana ubavu wa kutwaa ubingwa wa England msimu huu na badala yake wanapigania nafasi moja kati ya nne za juu.
Kiungo huyo ametoa kauli hiyo muda mfupi baada ya Liverpool kutupwa nje katika mbio za kuwania Kombe la Carling kuchapwa mabao 4-2 na timu ya daraja la nne Northampton.
"Ukweli hatuna ubavu wa kutwaa kombe la England, tunapigania nafasi moja kati ya nne. Msimu uliopita tulimaliza tukiwa nafasi ya nne lakini mwaka huu tutajitahidi angalau tuingie nne bora," alisema Gerrard.
Nahodha huyo msaidizi wa England, alisema wamejifunza baada ya kuumbiliwa na timu ya daraja la nne. Gerrard atakuwepo uwanjani katika mchezo wa leo dhidi ya Sunderland baada ya Jumatano kupumzika. Kiungo huyo alifunga mabao yote mawili katika mechi na Manchester United waliochapwa mabao 3-2 Jumapili iliyopita.
NAHODHA wa Liverpool, Steven Gerrard ametoa kauli nzito baada ya kukiri hawana ubavu wa kutwaa ubingwa wa England msimu huu na badala yake wanapigania nafasi moja kati ya nne za juu.
Kiungo huyo ametoa kauli hiyo muda mfupi baada ya Liverpool kutupwa nje katika mbio za kuwania Kombe la Carling kuchapwa mabao 4-2 na timu ya daraja la nne Northampton.
"Ukweli hatuna ubavu wa kutwaa kombe la England, tunapigania nafasi moja kati ya nne. Msimu uliopita tulimaliza tukiwa nafasi ya nne lakini mwaka huu tutajitahidi angalau tuingie nne bora," alisema Gerrard.
Nahodha huyo msaidizi wa England, alisema wamejifunza baada ya kuumbiliwa na timu ya daraja la nne. Gerrard atakuwepo uwanjani katika mchezo wa leo dhidi ya Sunderland baada ya Jumatano kupumzika. Kiungo huyo alifunga mabao yote mawili katika mechi na Manchester United waliochapwa mabao 3-2 Jumapili iliyopita.
OWEN AMUOMBA FERGUSON AMPANGE
LONDON, England
MSHAMBULIAJI nguli wa Manchester United, Michael Owena amemwangukia Sir Alex Ferguson akimtaka ampange katika michezo ya Ligi Kuu England msimu huu.
Owen ametoa kauli hiyo muda mfupi baada ya kufunga mabao mawili na kuchangia ushindi wa mabao 5-2 iliyopata United katika mchezo wake wa Kombe la Carling ilipovaana na Scunthorpe.
Mchezaji huyo wa zamani wa England, amerejea katika kiwango bora baada ya kuwa nje ya uwanja muda mrefu kutokana na kukabiliwa na majeraha ya nyonga, amecheza mechi tatu akitokea benchi tangu kuanza msimu huu.
Lakini, Jumatano iliyopita Owen alikuwa nyota wa mchezo baada ya kucheza kwa kiwango bora dakika 90 ingawa Ferguson hakuwepo uwanjani na inadaiwa alikwenda Hispania kuipepeleza Valencia ambayo watakutana nayo wiki ijayo katika mchezo wa ligi ya mabingwa Ulaya.
Baada ya kung'ara katika mchezo huo, mshambuliaji huyo wa zamani wa klabu za Liverpool, Real Madrid na Newcastle United, ana imani ataonyesha soka ya kuvutia msimu huu baada ya kupona.
"Ilikuwa mechi nzuri kwangu dhidi ya Scunthorpe, nipo katika kipindi cha mpito kwenye michuano ijayo ya ligi ya mabingwa Ulaya na Kombe la Carling. Nina uhakika nitacheza mechi nyingi zaidi," alisema Owen mwenye miaka 30.
Mchezaji huyo anatakiwa kufanya kazi ya ziada kumshawishi Ferguson kumpa nafasi ya kikosi cha kwanza baada ya kocha huyo kuvutiwa na viwango vya Wayne Rooney na Dimitar Berbatov kucheza safu ya ushambuliaji. Berbatov amemshitua Ferguson baada ya Jumapili iliyopita kufunga mabao yote matatu katika mechi dhidi ya mahasimu wao Liverpool.
MSHAMBULIAJI nguli wa Manchester United, Michael Owena amemwangukia Sir Alex Ferguson akimtaka ampange katika michezo ya Ligi Kuu England msimu huu.
Owen ametoa kauli hiyo muda mfupi baada ya kufunga mabao mawili na kuchangia ushindi wa mabao 5-2 iliyopata United katika mchezo wake wa Kombe la Carling ilipovaana na Scunthorpe.
Mchezaji huyo wa zamani wa England, amerejea katika kiwango bora baada ya kuwa nje ya uwanja muda mrefu kutokana na kukabiliwa na majeraha ya nyonga, amecheza mechi tatu akitokea benchi tangu kuanza msimu huu.
Lakini, Jumatano iliyopita Owen alikuwa nyota wa mchezo baada ya kucheza kwa kiwango bora dakika 90 ingawa Ferguson hakuwepo uwanjani na inadaiwa alikwenda Hispania kuipepeleza Valencia ambayo watakutana nayo wiki ijayo katika mchezo wa ligi ya mabingwa Ulaya.
Baada ya kung'ara katika mchezo huo, mshambuliaji huyo wa zamani wa klabu za Liverpool, Real Madrid na Newcastle United, ana imani ataonyesha soka ya kuvutia msimu huu baada ya kupona.
"Ilikuwa mechi nzuri kwangu dhidi ya Scunthorpe, nipo katika kipindi cha mpito kwenye michuano ijayo ya ligi ya mabingwa Ulaya na Kombe la Carling. Nina uhakika nitacheza mechi nyingi zaidi," alisema Owen mwenye miaka 30.
Mchezaji huyo anatakiwa kufanya kazi ya ziada kumshawishi Ferguson kumpa nafasi ya kikosi cha kwanza baada ya kocha huyo kuvutiwa na viwango vya Wayne Rooney na Dimitar Berbatov kucheza safu ya ushambuliaji. Berbatov amemshitua Ferguson baada ya Jumapili iliyopita kufunga mabao yote matatu katika mechi dhidi ya mahasimu wao Liverpool.
Thursday, September 23, 2010
"TWIGA STARS ITAFANYA VIZURI." - KAIJAGE.
PAMOJA na kuingia katika michuano hiyo kwa mara ya kwanza katika michuano ya Mataifa ya Afrika kwa wanawake, Shirikisho la Soka nchini (TFF) limesema timu hiyo iko tayari na itakwenda kushindana na sio kushiriki.
Ofisa Habari wa TFF, Florian Kaijage alisema Jumatano kuwa uongozi una imani na Twiga Stars kuwa itafanya vizuri pamoja na kupangwa katika kundi gumu na timu za South Afrika na Nigeria.
Kaijage alisema ukiangalia jinsi gani Twiga walivyofuzu basi hutakuwa na mashaka kwamba vijana wako fiti tayari kwa ajili ya mashindano hayo.
"Twiga Stars kuwekwa katika kundi moja na Nigeria ambao ni mabingwa mara tano pamoja na wenyeji Afrika Kusini haimaanishi kuwa tayari wameshatolewa katika mashindano. Vijana wako tayari kushindana." alisema Kaijage.
Aliendelea kusema kuwa kuna mipango ya kuwaandalia mechi za kirafiki za ndani na za kimataifa kabla ya michuano hiyo itakayomwezesha kocha kurkebisha makosa yatayojitokeza.
Ofisa Habari wa TFF, Florian Kaijage alisema Jumatano kuwa uongozi una imani na Twiga Stars kuwa itafanya vizuri pamoja na kupangwa katika kundi gumu na timu za South Afrika na Nigeria.
Kaijage alisema ukiangalia jinsi gani Twiga walivyofuzu basi hutakuwa na mashaka kwamba vijana wako fiti tayari kwa ajili ya mashindano hayo.
"Twiga Stars kuwekwa katika kundi moja na Nigeria ambao ni mabingwa mara tano pamoja na wenyeji Afrika Kusini haimaanishi kuwa tayari wameshatolewa katika mashindano. Vijana wako tayari kushindana." alisema Kaijage.
Aliendelea kusema kuwa kuna mipango ya kuwaandalia mechi za kirafiki za ndani na za kimataifa kabla ya michuano hiyo itakayomwezesha kocha kurkebisha makosa yatayojitokeza.
"SIZITAKI MBICHI HIZI," ANCELOTTI.
KOCHA wa Chelsea Carlo Ancelotti amesema Kombe la Ligi (Carling Cup) halikuwa katika mipango yao baada ya kutolewa na Newcastle United kwa mabao 4-3 nyumbani kwao.
Ancelotti alichezesha kikosi dhaifu wakiwemo wachezaji watatu chipukizi na wengine wanne wakiwa waakiba. Beki John Terry naye alitolewa baada ya mapumziko ikiwa ni sehemu ya maandalizi na mchezo wao wa Jumamosi dhidi ya Manchester City.
"Halikuwa katika mipango yetu" alikaririwa Ancelotti katika mkutano na waandishi wa habari. "Nilitaka tushinde lakini sijashtuka. Nina furaha sio kwa matokeo bali kiwango walichoonyesha.
"Tulionyesha kiwango kizuri tulivyokuwa nyuma kwa mabao 3-1. Tulikuwa tuko 10 wao walikuwa 11 na tulionyesha mshikamano mzuri kitu ambacho ni muhimu kwetu."
Ancelotti alichezesha kikosi dhaifu wakiwemo wachezaji watatu chipukizi na wengine wanne wakiwa waakiba. Beki John Terry naye alitolewa baada ya mapumziko ikiwa ni sehemu ya maandalizi na mchezo wao wa Jumamosi dhidi ya Manchester City.
"Halikuwa katika mipango yetu" alikaririwa Ancelotti katika mkutano na waandishi wa habari. "Nilitaka tushinde lakini sijashtuka. Nina furaha sio kwa matokeo bali kiwango walichoonyesha.
"Tulionyesha kiwango kizuri tulivyokuwa nyuma kwa mabao 3-1. Tulikuwa tuko 10 wao walikuwa 11 na tulionyesha mshikamano mzuri kitu ambacho ni muhimu kwetu."
CARLOS VELA AFUNGIWA MIEZI SITA MEXICO.
MEXICO CITY, Mexico.
SHIRIKISHO la Soka la Mexico limewafungia wachezaji Carlos Vela na Efrain Juarez kwa muda wa miezi sita na kuwapiga faini wachezaji wengine 11 wa timu hiyo kwa kuvunja sheria.
Wachezaji hao waliandaa sherehe katika hotel waliofikia timu hiyo ya Monterrey baada ya mchezo dhidi ya Colombia uliochezwa Septemba 7 mwaka huu.
Taarifa ilitolewa Jumanne kwa waandishi wa habari na Nestor de La Torre, Mkurugenzi anayeshughulika na uchaguzi wa kikosi cha timu ya Taifa ya nchi hiyo. alisema Vela ambaye anacheza katika klabu ya Arsenal ya Uingereza na Juarez ambaye anacheza klabu ya Celtic ya Scotland walikiuka sheria nne za soka za nchi hiyo.
Wachezaji waliopigwa faini ni pamoja na Rafael Marquez, Javier Hernandez, Giovanni dos Santos, Guillermo Ochoa, Francisco Rodriguez, Carlos Salcido, Andres Guardado, Gerard Torrado, Pablo Barrera, Hector Esqueda na Hector Moreno.
SHIRIKISHO la Soka la Mexico limewafungia wachezaji Carlos Vela na Efrain Juarez kwa muda wa miezi sita na kuwapiga faini wachezaji wengine 11 wa timu hiyo kwa kuvunja sheria.
Wachezaji hao waliandaa sherehe katika hotel waliofikia timu hiyo ya Monterrey baada ya mchezo dhidi ya Colombia uliochezwa Septemba 7 mwaka huu.
Taarifa ilitolewa Jumanne kwa waandishi wa habari na Nestor de La Torre, Mkurugenzi anayeshughulika na uchaguzi wa kikosi cha timu ya Taifa ya nchi hiyo. alisema Vela ambaye anacheza katika klabu ya Arsenal ya Uingereza na Juarez ambaye anacheza klabu ya Celtic ya Scotland walikiuka sheria nne za soka za nchi hiyo.
Wachezaji waliopigwa faini ni pamoja na Rafael Marquez, Javier Hernandez, Giovanni dos Santos, Guillermo Ochoa, Francisco Rodriguez, Carlos Salcido, Andres Guardado, Gerard Torrado, Pablo Barrera, Hector Esqueda na Hector Moreno.
Wednesday, September 22, 2010
ARSENAL YAUA.
LONDON, England
KIUNGO Samir Nasri, juzi aliongoza mauaji ya Arsenal baada ya kufunga mabao mawili na kuchangia ushindi wa mabao 4-1 iliyopata timu hiyo dhidi ya Tottenham Hotspurs katika mchezo wa Kombe la Carling uliochezwa Uwanja wa Emirates, London.
Nasri alifunga mabao hayo kwa mkwaju wa penalti 92 na 96 katika muda wa niongeza baada ya miamba hiyo kutoka sare bao 1-1 dakika 90. Arsenal ilianza kumpa presha kocha wa Spurs, Harry Redknapp baada ya kufunga bao dakika 15 kupitia kwa Henri Lansbury kabla ya Andrey Arshavin kufunga la nne dakika 105.
Spurs ilizidisha mashambulizi langoni mwa Arsenal kutaka kusawazisha na juhudi zao zilizaa matunda baada ya mchezaji nguli, Robbie Keane kupachika bao dakika 49 akifunga kwa umbali wa yadi 18. Mashabiki wa Spurs, waliondoka mapema uwanjani kabla ya mchezo huo kumalizika.
Katika mechi zingine, Birmingham ilishinda mabao 3-1 dhidi ya MK Dons, Brentford ilitoka sare bao 1-1 ilipovaana na Everton, timu hiyo ilisonga mbele kwa jumla ya ushindi wa mabao 4-3 kwa mikwaju ya penalti. Burnley ilipata ushindi wa bao 1-0 ilipomenyana na Bolton.
Millwall ilikiona cha moto baada ya kulambwa mabao 2-1 ilipomenyana na Ipswich Town, Peterborough ilinyukwa mabao 3-1 ilipochuana na Swansea, Portsmouth ilifungwa 2-1 na Leicester wakati Stoke City iliichapa Fulham 2-0. West Ham ilishinda 2-1 dhidi ya Sunderland na Wolves ilishinda 4-2 ilipovaana na Notts County.
KIUNGO Samir Nasri, juzi aliongoza mauaji ya Arsenal baada ya kufunga mabao mawili na kuchangia ushindi wa mabao 4-1 iliyopata timu hiyo dhidi ya Tottenham Hotspurs katika mchezo wa Kombe la Carling uliochezwa Uwanja wa Emirates, London.
Nasri alifunga mabao hayo kwa mkwaju wa penalti 92 na 96 katika muda wa niongeza baada ya miamba hiyo kutoka sare bao 1-1 dakika 90. Arsenal ilianza kumpa presha kocha wa Spurs, Harry Redknapp baada ya kufunga bao dakika 15 kupitia kwa Henri Lansbury kabla ya Andrey Arshavin kufunga la nne dakika 105.
Spurs ilizidisha mashambulizi langoni mwa Arsenal kutaka kusawazisha na juhudi zao zilizaa matunda baada ya mchezaji nguli, Robbie Keane kupachika bao dakika 49 akifunga kwa umbali wa yadi 18. Mashabiki wa Spurs, waliondoka mapema uwanjani kabla ya mchezo huo kumalizika.
Katika mechi zingine, Birmingham ilishinda mabao 3-1 dhidi ya MK Dons, Brentford ilitoka sare bao 1-1 ilipovaana na Everton, timu hiyo ilisonga mbele kwa jumla ya ushindi wa mabao 4-3 kwa mikwaju ya penalti. Burnley ilipata ushindi wa bao 1-0 ilipomenyana na Bolton.
Millwall ilikiona cha moto baada ya kulambwa mabao 2-1 ilipomenyana na Ipswich Town, Peterborough ilinyukwa mabao 3-1 ilipochuana na Swansea, Portsmouth ilifungwa 2-1 na Leicester wakati Stoke City iliichapa Fulham 2-0. West Ham ilishinda 2-1 dhidi ya Sunderland na Wolves ilishinda 4-2 ilipovaana na Notts County.
MATTHAUS KUINOA BULGARIA.
BERLIN, Ujerumani
NAHODHA wa zamani wa Ujerumani, Lothar Matthaus (49) ametangazwa kocha mpya wa timu ya taifa ya Bulgaria baada ya kukubali kutia saini mkataba wa mwaka mmoja kuchukuwa nafasi ya Stanimir Stoilov.
Rais wa Shirikisho la Soka Bulgaria (BFU), Borislav Mihaylov alithibitisha kuwa nguli huyo wa zamani aliyecheza kwa mafanikio makubwa Ujerumani na klabu za Ulaya na walitaka kumpa mkataba wa muda mrefu kabla ya Matthaus kukubali kuinoa Bulgaria miezi 12.
Matthaus aliinoa Hungary mwaka 2004-2005, amewahi kuzifundisha klabu mbalimbali za Ulaya ikiwemo Rapid Vienna ya Austria. Mtihani wake wa kwanza utakuwa Oktoba 8, Bulgaria itakapovaana na Wales katika mchezo wa kufuzu fainali za Kombe la Ulaya 2012 ambapo imepangwa kundi G.
Bulgaria ilianza vibaya kampeni yake baada ya kukubali kipigo cha mabao 4-0 dhidi ya England Septemba 3 kabla ya kuchapwa bao 1-0 ikiwa nyumbani ilipovaana na Montenegro siku nne baadaye. Matokeo hayo yalimfanya Stoilov kutangaza kujiuzulu.
Rekodi ya mkongwe huyo inaonyesha alicheza mechi 150 za kimataifa na aliing'arisha Ujerumani katika fainali za Kombe la Dunia 1990, alikuwa mchezaji wa kwanza kutwaa tuzo ya mwanasoka bora wa dunia 1991.
Matthaus alistaafu soka akiwa na klabu ya Borussia Monchengladbach, lakini muda mrefu amekuwa mwakilishi wa Bayern Munich. Nguli huyo amewahi kuzinoa klabu za (Rapid Vienna, Austria), (Partizan Belgrade, Serbia), (Atletico Paranaense, Brazil), (Red Bull Salzburg, Austria) na Maccabi Netanya ya Israel.
NAHODHA wa zamani wa Ujerumani, Lothar Matthaus (49) ametangazwa kocha mpya wa timu ya taifa ya Bulgaria baada ya kukubali kutia saini mkataba wa mwaka mmoja kuchukuwa nafasi ya Stanimir Stoilov.
Rais wa Shirikisho la Soka Bulgaria (BFU), Borislav Mihaylov alithibitisha kuwa nguli huyo wa zamani aliyecheza kwa mafanikio makubwa Ujerumani na klabu za Ulaya na walitaka kumpa mkataba wa muda mrefu kabla ya Matthaus kukubali kuinoa Bulgaria miezi 12.
Matthaus aliinoa Hungary mwaka 2004-2005, amewahi kuzifundisha klabu mbalimbali za Ulaya ikiwemo Rapid Vienna ya Austria. Mtihani wake wa kwanza utakuwa Oktoba 8, Bulgaria itakapovaana na Wales katika mchezo wa kufuzu fainali za Kombe la Ulaya 2012 ambapo imepangwa kundi G.
Bulgaria ilianza vibaya kampeni yake baada ya kukubali kipigo cha mabao 4-0 dhidi ya England Septemba 3 kabla ya kuchapwa bao 1-0 ikiwa nyumbani ilipovaana na Montenegro siku nne baadaye. Matokeo hayo yalimfanya Stoilov kutangaza kujiuzulu.
Rekodi ya mkongwe huyo inaonyesha alicheza mechi 150 za kimataifa na aliing'arisha Ujerumani katika fainali za Kombe la Dunia 1990, alikuwa mchezaji wa kwanza kutwaa tuzo ya mwanasoka bora wa dunia 1991.
Matthaus alistaafu soka akiwa na klabu ya Borussia Monchengladbach, lakini muda mrefu amekuwa mwakilishi wa Bayern Munich. Nguli huyo amewahi kuzinoa klabu za (Rapid Vienna, Austria), (Partizan Belgrade, Serbia), (Atletico Paranaense, Brazil), (Red Bull Salzburg, Austria) na Maccabi Netanya ya Israel.
BENTO AMRITHI QUEIROZ URENO.
LISBON, Ureno
PAULO Bento ametangazwa kocha mpya wa Ureno kuchukuwa nafasi ya Carlos Queiroz aliyefungiwa miezi sita baada ya kupatikana na hatia ya kuwatolea lugha isiyofaa madaktari waliotaka kuwapima wachezaji wa timu hiyo dawa za kuongeza nguvu muda mfupi kabla ya kwenda Afrika Kusini kushiriki Kombe la Dunia 2010.
Nyota huyo wa zamani wa kimataifa wa Ureno mwenye miaka 41, ametia saini mkataba wa miaka miwili hadi Julai 2012. Kabla ya kustaafu soka, Bento alicheza mechi 35 akiwa na timu ya taifa. Bento jana alitambulishwa rasmi mbele ya waandishi wa habari makao makuu ya Shirikisho la Soka Ureno (PFF).
Bento atasaidiwa na Leonel Pontes, Joao Aroso atakuwa kocha wa viungo wakati Ricardo Peres ameteuliwa kufundisha makipa. Kabla ya kutwaa mikoba, benchi hilo la ufundi liliwahi kufanya kazi chini ya Bento kuinoa klabu ya Sporting Lisbon kati ya mwaka 2005 na 2009.
Kabla ya kutundika daluga, Bento alianza kung'ara katika mchezo wa soka akiwa na miaka 17 alipokuwa mchezaji tegemeo wa klabu za Sporting Lisbon na baadaye Benfica. Alikuwa miongoni mwa wachezaji waliocheza fainali za Kombe la Ulaya 2000 na Kombe la Dunia 2002.
"Paulo Bento na benchi la ufundi wametia saini mkataba wa hadi Julai 2012," ilisema sehemu ya mtandao wa Shirikisho hilo. Kocha huyo ataiongoza Ureno katika mechi za kufuzu fainali za Kombe la Ulaya 2012.
Queiroz alifukuzwa siku mbili baada ya kufungiwa miezi sita baada ya Ureno kuchapwa bao 1-0 na Norway katika mechi za kufuzu Kombe la Ulaya 2012.
Ureno ilianza kwa sare ya mabao 4-4 na Cyprus katika mechi za kufuzu fainali hizo. Ureno inashika mkia katika msimamo wa kundi H ikiwa tayari imezidiwa pointi tano na vinara Norway. Mtihani wa kwanza kwa Bento utakuwa Oktoba 8, Ureno itakapokuwa nyumbani kuvaana na Denmark kabla ya kuivaa Reykjavik siku nne baadaye.
PAULO Bento ametangazwa kocha mpya wa Ureno kuchukuwa nafasi ya Carlos Queiroz aliyefungiwa miezi sita baada ya kupatikana na hatia ya kuwatolea lugha isiyofaa madaktari waliotaka kuwapima wachezaji wa timu hiyo dawa za kuongeza nguvu muda mfupi kabla ya kwenda Afrika Kusini kushiriki Kombe la Dunia 2010.
Nyota huyo wa zamani wa kimataifa wa Ureno mwenye miaka 41, ametia saini mkataba wa miaka miwili hadi Julai 2012. Kabla ya kustaafu soka, Bento alicheza mechi 35 akiwa na timu ya taifa. Bento jana alitambulishwa rasmi mbele ya waandishi wa habari makao makuu ya Shirikisho la Soka Ureno (PFF).
Bento atasaidiwa na Leonel Pontes, Joao Aroso atakuwa kocha wa viungo wakati Ricardo Peres ameteuliwa kufundisha makipa. Kabla ya kutwaa mikoba, benchi hilo la ufundi liliwahi kufanya kazi chini ya Bento kuinoa klabu ya Sporting Lisbon kati ya mwaka 2005 na 2009.
Kabla ya kutundika daluga, Bento alianza kung'ara katika mchezo wa soka akiwa na miaka 17 alipokuwa mchezaji tegemeo wa klabu za Sporting Lisbon na baadaye Benfica. Alikuwa miongoni mwa wachezaji waliocheza fainali za Kombe la Ulaya 2000 na Kombe la Dunia 2002.
"Paulo Bento na benchi la ufundi wametia saini mkataba wa hadi Julai 2012," ilisema sehemu ya mtandao wa Shirikisho hilo. Kocha huyo ataiongoza Ureno katika mechi za kufuzu fainali za Kombe la Ulaya 2012.
Queiroz alifukuzwa siku mbili baada ya kufungiwa miezi sita baada ya Ureno kuchapwa bao 1-0 na Norway katika mechi za kufuzu Kombe la Ulaya 2012.
Ureno ilianza kwa sare ya mabao 4-4 na Cyprus katika mechi za kufuzu fainali hizo. Ureno inashika mkia katika msimamo wa kundi H ikiwa tayari imezidiwa pointi tano na vinara Norway. Mtihani wa kwanza kwa Bento utakuwa Oktoba 8, Ureno itakapokuwa nyumbani kuvaana na Denmark kabla ya kuivaa Reykjavik siku nne baadaye.
MWAMUZI ANAYECHUKIWA NCHINI ITALIA MBARONI KWA MADAWA YA KULEVYA.
MWAMUZI wa zamani anayechukiwa nchini Italia toka fainali za Kombe la Dunia zilizofanyika Japan na Korea Kusini 2002 amekamatwa katika Uwanja wa Ndege wa JF Kennedy kwa kukutwa na madawa ya kulevya aina ya heroin akiwa amejifunga mwilini mwake.
Maofisa wa Uhamiaji wa nchi hiyo pamoja na maofisa wa forodha walimkamata Byron Moreno Jumatatu baada ya kuwasili New York kwa ndege ya abiria akitokea Ecuador.
Wakati akikaguliwa, Moreno alionekana akitetemeka kwa mujibu wa maelezo ya mahakama ya Brooklyn.
Ofisa wa Forodha alihisi "kitu kigumu katika tumbo la Moreno, kwa nyuma na katika miguu yote miwili," alisema mwendesha mashitaka. Baada ya kumvua nguo na kumkagua walimkuta na mifuko kumi ya plastiki ambayo ilikuwa na madawa ya kulevya yanayokadiriwa kuwa kama kilo 10 hivi, alisema.
Jaji alimpeleka rumande Moreno bila ya dhamana kwa kosa la kukutwa na madawa hayo.
"Naangalia tukio lenyewe ilivyo ili nione ni jinsi gani naweza kumsaidia" alisema mwanasheria Michael Padden anayemwakilisha Moreno Jumanne.
Moreno aliwachanganya mashabiki wa Italia 2002 baada ya kumtoa Francesco Totti, kwa kumpa kadi ya pili ya njano kwa kujirusha katika eneo la hatari dakika 13 kabla ya mpira kumalizika ambapo Italia ilifungwa mabao 2-1 na South Korea katika raundi ya pili ya Kombe la Dunia.
Bao la dakika ya 111 lililofungwa na Damiano Tommasi ambalo lingeweza kuivusha Italia lilikataliwa kwa madai mchezaji huyo alikuwa ameotea, na South Korea walizawadiwa penati ambayo iliokolewa na golikipa Gianluigi Buffon kwa faulo ambayo ilichezwa na Christian Panucci dhidi ya Seol Ki-Hyeon.
"Nafikiri Moreno tayari alikuwa alikuwa na madawa ya kulevya 2002, lakini sio kwenye nguo yake ya ndani bali ndani ya mwili," alikaririwa Buffon akisema kwa utani, "watu wa kichezo wanapojiingiza katika biashara ya madawa ya kulevya wanapoteza maana ya michezo, ambayo pia inamaana ya kuokoa watoto wa mitaani kwenye hatari kama ya kujihusisha na utumiaji wa madawa ya kulevya.
Maofisa wa Uhamiaji wa nchi hiyo pamoja na maofisa wa forodha walimkamata Byron Moreno Jumatatu baada ya kuwasili New York kwa ndege ya abiria akitokea Ecuador.
Wakati akikaguliwa, Moreno alionekana akitetemeka kwa mujibu wa maelezo ya mahakama ya Brooklyn.
Ofisa wa Forodha alihisi "kitu kigumu katika tumbo la Moreno, kwa nyuma na katika miguu yote miwili," alisema mwendesha mashitaka. Baada ya kumvua nguo na kumkagua walimkuta na mifuko kumi ya plastiki ambayo ilikuwa na madawa ya kulevya yanayokadiriwa kuwa kama kilo 10 hivi, alisema.
Jaji alimpeleka rumande Moreno bila ya dhamana kwa kosa la kukutwa na madawa hayo.
"Naangalia tukio lenyewe ilivyo ili nione ni jinsi gani naweza kumsaidia" alisema mwanasheria Michael Padden anayemwakilisha Moreno Jumanne.
Moreno aliwachanganya mashabiki wa Italia 2002 baada ya kumtoa Francesco Totti, kwa kumpa kadi ya pili ya njano kwa kujirusha katika eneo la hatari dakika 13 kabla ya mpira kumalizika ambapo Italia ilifungwa mabao 2-1 na South Korea katika raundi ya pili ya Kombe la Dunia.
Bao la dakika ya 111 lililofungwa na Damiano Tommasi ambalo lingeweza kuivusha Italia lilikataliwa kwa madai mchezaji huyo alikuwa ameotea, na South Korea walizawadiwa penati ambayo iliokolewa na golikipa Gianluigi Buffon kwa faulo ambayo ilichezwa na Christian Panucci dhidi ya Seol Ki-Hyeon.
"Nafikiri Moreno tayari alikuwa alikuwa na madawa ya kulevya 2002, lakini sio kwenye nguo yake ya ndani bali ndani ya mwili," alikaririwa Buffon akisema kwa utani, "watu wa kichezo wanapojiingiza katika biashara ya madawa ya kulevya wanapoteza maana ya michezo, ambayo pia inamaana ya kuokoa watoto wa mitaani kwenye hatari kama ya kujihusisha na utumiaji wa madawa ya kulevya.
HENRY KUMKOSA BECKHAM.
MCHEZAJI Thierry Henry atakosa mchezo muhimu utaokaochezwa Ijumaa wakati timu yake ya New York Red Bulls itakapomenyana na timu anayocheza David Beckham ya Los Angeles Galaxy kufuatia kuumia mguu wake wa kulia.
Msemaji wa klabu hiyo alisema Jumanne kuwa mshambuliaji wa Ufaransa alifanyiwa vipimo kuangalia ni kiasi gani aliumia katika mchezo uliochezwa Septemba 4 dhidi ya Real Salt Lake ambao walipoteza.
Alicheza akiwa majeruhi wiki iliyopita na alitozwa faini ya dola 2,000 kwa kushangilia kwa kupiga mpira shuti baada ya mchezaji mwenzake Mehdi Ballouchy kufunga bao shuti hilo lilipelekea mpira mpira kumpiga golikipa wa Dallas Kevin Hartman na kumuumiza mguu.
"Tumeongea na Henry Jumatatu na tumeamua kwamba ni vizuri tukampumzisha kwa ajili ya afya yake," alisema Meneja wa Red Bulls Erik Soler. "Pamoja na mchezo unaotukabili Ijumaa, hatutaki kumuongezea maumivu zaidi ambayo amekuwa akicheza nayo karibu wiki mbili.
"Tunahitaji kuwa na uhakika kuhusu afya yake kwa ajili ya michezo yetu ya mwisho kwa kutarajia kuingia hatua ya mtoano, na kukaribia kutwaa kombe la (Major League Soccer [MLS]).
Mchezo wa Ijumaa utajumuisha wachezaji nyota wa ligi hiyo wakiwemo Landon Donovan wa Galax, Juan Pablo Angel na Rafael Marquez wote wa Red Bulls.
Msemaji wa klabu hiyo alisema Jumanne kuwa mshambuliaji wa Ufaransa alifanyiwa vipimo kuangalia ni kiasi gani aliumia katika mchezo uliochezwa Septemba 4 dhidi ya Real Salt Lake ambao walipoteza.
Alicheza akiwa majeruhi wiki iliyopita na alitozwa faini ya dola 2,000 kwa kushangilia kwa kupiga mpira shuti baada ya mchezaji mwenzake Mehdi Ballouchy kufunga bao shuti hilo lilipelekea mpira mpira kumpiga golikipa wa Dallas Kevin Hartman na kumuumiza mguu.
"Tumeongea na Henry Jumatatu na tumeamua kwamba ni vizuri tukampumzisha kwa ajili ya afya yake," alisema Meneja wa Red Bulls Erik Soler. "Pamoja na mchezo unaotukabili Ijumaa, hatutaki kumuongezea maumivu zaidi ambayo amekuwa akicheza nayo karibu wiki mbili.
"Tunahitaji kuwa na uhakika kuhusu afya yake kwa ajili ya michezo yetu ya mwisho kwa kutarajia kuingia hatua ya mtoano, na kukaribia kutwaa kombe la (Major League Soccer [MLS]).
Mchezo wa Ijumaa utajumuisha wachezaji nyota wa ligi hiyo wakiwemo Landon Donovan wa Galax, Juan Pablo Angel na Rafael Marquez wote wa Red Bulls.
ALIYEMJERUHI MESSI AFUNGIWA MECHI MBILI.
BEKI wa Atletico Madrid Tomas Ujfalusi amefungiwa kucheza mechi mbili kufuatia tukio lake la kumchezea vibaya nyota wa Barcelona Lionel Messi Jumapili iliyopita ambapo timu hiyo ilipoteza mchezo huo.
Beki wa huyo wa kimataifa wa Czech alifanya tukio hilo katika dakika za majeruhi na kupelekea kutolewa nje kwa kadi nyekundu na kumfanya Messi kuwa nje ya uwanja kwa wiki mbili.
Waandishi wa habari wa Hispania walikadiria kuwa beki huyo anaweza kufungiwa mechi kumi na mbili lakini Kamati ya Mashindano waliliona tukio hilo halikuwa la kukusudia hivyo kuamua atatumikia adhabu ya mechi mbili kama kawaida.
Ujfalusi ambaye tayari alishamuomba msamaha Messi kupitia ujumbe mfupi kwenye simu ya mchezaji mwenzake Kun Aguero atakosa michezo miwili wakati timu yake itakapopambana na valencia na Zaragoza.
Beki wa huyo wa kimataifa wa Czech alifanya tukio hilo katika dakika za majeruhi na kupelekea kutolewa nje kwa kadi nyekundu na kumfanya Messi kuwa nje ya uwanja kwa wiki mbili.
Waandishi wa habari wa Hispania walikadiria kuwa beki huyo anaweza kufungiwa mechi kumi na mbili lakini Kamati ya Mashindano waliliona tukio hilo halikuwa la kukusudia hivyo kuamua atatumikia adhabu ya mechi mbili kama kawaida.
Ujfalusi ambaye tayari alishamuomba msamaha Messi kupitia ujumbe mfupi kwenye simu ya mchezaji mwenzake Kun Aguero atakosa michezo miwili wakati timu yake itakapopambana na valencia na Zaragoza.
Tuesday, September 21, 2010
SHIRIKISHO LA SOKA TOGO LAMTUPIA LAWAMA KOCHA WAKE WA ZAMANI KUHUSU SAKATA LA KUPELEKA KIKOSI FEKI BAHRAIN.
LOME, TOGO
SHIRIKISHO la Soka la Togo limemtuhumu kocha wa zamani wa timu hiyo Tchanile Bana kuwa amehusika katika sakata la kupeleka kikosi cha uongo kucheza na Bahrain na wamemfungia kwa muda wa miaka mitatu.
Katika taarifa iliyotolewa Jumatatu, shirikisho hilo lilisema kuwa maandalizi ya timu na usimamizi wa mchezo huo vyete vilipangwa na Tchanile Bana.
Timu ilitengenezwa na wachezaji ambao hawajulikani na kupokea kipigo cha mabao 3-0 mchezo ulichezwa Septemba 7 mwaka huu.
Bana, ambaye alikuwa kocha wa Togo katika miaka ya 2000 na 2004, tayari alishafungiwa miaka miwili kwa kupeleka timu Misri bila ya ridhaa.
Mjumbe wa Kamati ya Nidhamu ya shirikisho hilo alisema uchunguzi zaidi unafanyika kuhusu tukio hilo ambapo kuna viongozi wengine wanaweza kuchukuliwa hatua.
"Tukio zima lililotokea Bahrain lazima lichunguzwe kwa kina ili kuwanasa walioshirikiana na Bana." alisema Ofisa huyo.
SHIRIKISHO la Soka la Togo limemtuhumu kocha wa zamani wa timu hiyo Tchanile Bana kuwa amehusika katika sakata la kupeleka kikosi cha uongo kucheza na Bahrain na wamemfungia kwa muda wa miaka mitatu.
Katika taarifa iliyotolewa Jumatatu, shirikisho hilo lilisema kuwa maandalizi ya timu na usimamizi wa mchezo huo vyete vilipangwa na Tchanile Bana.
Timu ilitengenezwa na wachezaji ambao hawajulikani na kupokea kipigo cha mabao 3-0 mchezo ulichezwa Septemba 7 mwaka huu.
Bana, ambaye alikuwa kocha wa Togo katika miaka ya 2000 na 2004, tayari alishafungiwa miaka miwili kwa kupeleka timu Misri bila ya ridhaa.
Mjumbe wa Kamati ya Nidhamu ya shirikisho hilo alisema uchunguzi zaidi unafanyika kuhusu tukio hilo ambapo kuna viongozi wengine wanaweza kuchukuliwa hatua.
"Tukio zima lililotokea Bahrain lazima lichunguzwe kwa kina ili kuwanasa walioshirikiana na Bana." alisema Ofisa huyo.
"NI RAHISI KUCHEZA MADRID KULIKO CHELSEA." - CARVALHO.
TAJI pekee alilobakiza Ricardo Carvalho akiwa na klabu ya Chelsea ni taji la Klabu Bingwa ya Ulaya. Beki huyo wa kushoto mwenye miaka 32 ameondoka katika klabu hiyo baada ya kuitumikia kwa miaka sita, na kwa kuhama kwake amekwenda kukutana tena na Jose Mourinho ambaye alimpeleka Chelsea mwaka 2004.
Lakini wakati Ligi Kuu ya Hispania ikitajwa kuwa ligi bora duniani, ikiwa na wachezaji nyota wa dunia kama Leonel Messi na Cristiano Ronaldo, Carvalho alisema ligi hiyo ni tofauti na ya Uingereza.
"Wakati nilipokwenda Chelsea nilipata wakati mgumu tofauti na nilivyokuja hapa. Nimekulia Ureno na soka huko halina tofauti na hapa. nafikiri ni vigumu kucheza Ligi Kuu ya Uingereza. Wachezaji wa Uingereza wana nguvu zaidi kwa maana hiyo ni ngumu kucheza Chelsea kuliko hapa Madrid. Na kucheza huko kumenikomaza kama mchezaji. Nilikuwa na furaha katika kipindi chote cha miaka sita niliyochezea klabu hiyo." alisema Carvalho.
Lakini wakati Ligi Kuu ya Hispania ikitajwa kuwa ligi bora duniani, ikiwa na wachezaji nyota wa dunia kama Leonel Messi na Cristiano Ronaldo, Carvalho alisema ligi hiyo ni tofauti na ya Uingereza.
"Wakati nilipokwenda Chelsea nilipata wakati mgumu tofauti na nilivyokuja hapa. Nimekulia Ureno na soka huko halina tofauti na hapa. nafikiri ni vigumu kucheza Ligi Kuu ya Uingereza. Wachezaji wa Uingereza wana nguvu zaidi kwa maana hiyo ni ngumu kucheza Chelsea kuliko hapa Madrid. Na kucheza huko kumenikomaza kama mchezaji. Nilikuwa na furaha katika kipindi chote cha miaka sita niliyochezea klabu hiyo." alisema Carvalho.
GHANA 'THE BLACK STARS' KUPEWA TUZO.
TIMU ya Ghana ambayo ilifika hatua ya robo fainali katika Kombe la Dunia lilifanyika Afrika Kusini mwaka huu wanatarajiwa kutunukiwa tuzo katika shrehe zinazotarajiwa kufanyika mwezi ujao London, Uingereza.
Timu inakuwa ni timu ya tatu kwa Afrika kufikia hatua hiyo katika historia ya Kombe la Dunia, lakini walitolewa kwa matuta na timu ya Uruguay.
Walijizolea wapenzi wengi wakiwa huko kutokana na jinsi walivyocheza kwa kujitolea na morali walionyesha, na kuzipita timu kama Uingereza, Ufaransa na Italia ambazo hazikufanya vizuri katika mashindano hayo.
Sasa timu hiyo ambayo imeshawahi kuwa mabingwa wa Kombe la Mataifa ya Afrika watajipanga kupokea tuzo yao hiyo kutokana na mafanikio waliyopata inayoitwa [Ghana UK Based Achievement (GUBA) awards] inayotarajiwa kufanyika London on October 24 mwaka huu.
Mojawapo watakaohudhuria hafla hiyo ni pamoja na nahodha wa timu hiyo John Mensah, ambaye anacheza kwa mkopo katika klabu ya Sunderland akitokea klabu ya Lyon, na Asamoah Gyan ambaye amejiunga katika klabu hiyo na alifunga magoli matatu katika michuano hiyo.
Mchezaji wa Fulham John Painstil na Michael Essien wa Chelsea ambaye alikosa michuano hiyo kutokana na majeruhi yanayokuwa yakimkabili nao watahudhuria tuzo hizo.
'Hii ni habari nzuri inatufanya kama timu kuona kuwa tunathaminiwa kitu tulicholifanyia taifa letu, si mara nyingi tunapata tuzo Ghana." alisema Mensah
'Ni heshima kubwa kuona ni jinsi gani tuzo za GUBA zitakavyotutia moyo.
Mtangazaji wa luninga wa huko Ghana Denta Sumpa ambaye pia ni mmoja wa wandaaji wa tuzo hiyo alisema timu hiyo inastahili tuzo hiyo kwa kuiweka nchi hiyo katika ramani ya dunia kwani katika michuano hiyo haikushangiliwa na waafrika pekee bali dunia nzima.
Timu inakuwa ni timu ya tatu kwa Afrika kufikia hatua hiyo katika historia ya Kombe la Dunia, lakini walitolewa kwa matuta na timu ya Uruguay.
Walijizolea wapenzi wengi wakiwa huko kutokana na jinsi walivyocheza kwa kujitolea na morali walionyesha, na kuzipita timu kama Uingereza, Ufaransa na Italia ambazo hazikufanya vizuri katika mashindano hayo.
Sasa timu hiyo ambayo imeshawahi kuwa mabingwa wa Kombe la Mataifa ya Afrika watajipanga kupokea tuzo yao hiyo kutokana na mafanikio waliyopata inayoitwa [Ghana UK Based Achievement (GUBA) awards] inayotarajiwa kufanyika London on October 24 mwaka huu.
Mojawapo watakaohudhuria hafla hiyo ni pamoja na nahodha wa timu hiyo John Mensah, ambaye anacheza kwa mkopo katika klabu ya Sunderland akitokea klabu ya Lyon, na Asamoah Gyan ambaye amejiunga katika klabu hiyo na alifunga magoli matatu katika michuano hiyo.
Mchezaji wa Fulham John Painstil na Michael Essien wa Chelsea ambaye alikosa michuano hiyo kutokana na majeruhi yanayokuwa yakimkabili nao watahudhuria tuzo hizo.
'Hii ni habari nzuri inatufanya kama timu kuona kuwa tunathaminiwa kitu tulicholifanyia taifa letu, si mara nyingi tunapata tuzo Ghana." alisema Mensah
'Ni heshima kubwa kuona ni jinsi gani tuzo za GUBA zitakavyotutia moyo.
Mtangazaji wa luninga wa huko Ghana Denta Sumpa ambaye pia ni mmoja wa wandaaji wa tuzo hiyo alisema timu hiyo inastahili tuzo hiyo kwa kuiweka nchi hiyo katika ramani ya dunia kwani katika michuano hiyo haikushangiliwa na waafrika pekee bali dunia nzima.
"NAJISIKIA KAMA NIMEFIKA MWEZINI HAPA MADRID." MOURINHO
KOCHA wa Real Madrid Jose Mourinho ametamba kwamba anajisikia furaha katika klabu hiyo akilinganisha kama kufika mwezini.
Akiongea Jumatatu kuhusu mchezo wao ujao dhidi ya timu ya Espanyol katika Uwanja wa Bernabeu, Mourinho alifafanua kuwa hawachukulii kiwango cha timu hiyo kirahisi na pia alionyesha jinsi gani anavyojivunia kufundisha mabingwa hao wa ulaya mara tisa.
"Espanyol ni timu yenye vipaji na inacheza soka la kuvutia," "watakuja hapa kushinda kama timu nyingine. hatuongozi ligi, lakini tunakaribia kufikia pale." alisema Mourinho kwenye tovuti ya klabu hiyo.
"Kuna timu nyingi ambazo ziko chini yetu na chache zilizotupita. Hivyo tunahitaji kuendelea kushinda ili kujiweka katika nafasi nzuri."
Kocha huyo Mreno aliendelea kusema kuwa kufundisha klabu hiyo ni sawa na kutua mwezini.
"Kwa jinsi ninavyijisikia, kuwa kocha wa Madrid ni sawa na kufika mwezini. Ni moja ya muhimu zaidi duniani.
"Hiyo inamaanisha nimejifunga hapa, lakini bado hatujashinda chochote. Tutaangalia kama tunaweza kuweka historia.
"Miaka kumi imepita haraka sana. Sasa nina furaha kama nilivyokuwa naanza kazi hii, na sidhani kama kuna kinaweza kubadilika katika miaka kumi ijayo.
"Natarajia kuwa kama Ferguson (Kocha wa Manchester United). Nitakuwa na miaka 70 lakini nitakuwa na morali wa kufundisha kama nilivyo sasa."
Mourinho alimalizia kwa kuonyesha kumwamini nyota wake Cristiano Ronaldo.
"Huwa anafanya kazi kubwa kila siku wakati wa mazoezi na awapo uwanjani. Huwa anasaidiana vizuri na wachezaji wenzake. Ni mchezaji bora." alimalizia Mourinho.
Akiongea Jumatatu kuhusu mchezo wao ujao dhidi ya timu ya Espanyol katika Uwanja wa Bernabeu, Mourinho alifafanua kuwa hawachukulii kiwango cha timu hiyo kirahisi na pia alionyesha jinsi gani anavyojivunia kufundisha mabingwa hao wa ulaya mara tisa.
"Espanyol ni timu yenye vipaji na inacheza soka la kuvutia," "watakuja hapa kushinda kama timu nyingine. hatuongozi ligi, lakini tunakaribia kufikia pale." alisema Mourinho kwenye tovuti ya klabu hiyo.
"Kuna timu nyingi ambazo ziko chini yetu na chache zilizotupita. Hivyo tunahitaji kuendelea kushinda ili kujiweka katika nafasi nzuri."
Kocha huyo Mreno aliendelea kusema kuwa kufundisha klabu hiyo ni sawa na kutua mwezini.
"Kwa jinsi ninavyijisikia, kuwa kocha wa Madrid ni sawa na kufika mwezini. Ni moja ya muhimu zaidi duniani.
"Hiyo inamaanisha nimejifunga hapa, lakini bado hatujashinda chochote. Tutaangalia kama tunaweza kuweka historia.
"Miaka kumi imepita haraka sana. Sasa nina furaha kama nilivyokuwa naanza kazi hii, na sidhani kama kuna kinaweza kubadilika katika miaka kumi ijayo.
"Natarajia kuwa kama Ferguson (Kocha wa Manchester United). Nitakuwa na miaka 70 lakini nitakuwa na morali wa kufundisha kama nilivyo sasa."
Mourinho alimalizia kwa kuonyesha kumwamini nyota wake Cristiano Ronaldo.
"Huwa anafanya kazi kubwa kila siku wakati wa mazoezi na awapo uwanjani. Huwa anasaidiana vizuri na wachezaji wenzake. Ni mchezaji bora." alimalizia Mourinho.
"MASHABIKI WA ARSENAL MSIMLAUMU GALLAS" - WENGER.
KABLA ya mchezo wao wa Jumanne wa Kombe la Ligi dhidi ya Tottenham, kocha wa Arsenal Arsenal Wenger amesema kuwa mashabiki wa klabu hiyo wasimlaumu William Gallas kwa kujiunga na mahasimu wao hao wanaotoka Kaskazini mwa London.
"Naamini kuwa majukumu yake ni kujitolea kwa nguvu zote katika klabu ambayo unachezea na alifanya hivyo alivyokuwa nasi." alisema Wenger.
"Unaweza kuwaelewa watu kutofurahia kama hujafanya hivyo lakini huwezi kuwaliza watu kama huna mkataba ulisainiwa na klabu na hicho ndicho kitu muhimu."
Wakati timu hiyo ikikabiliwa na mchezo huo dhidi ya Spurs, Wenger anatarajia kutumia nafasi hiyo kuwachezesha makinda wake ili wapate uzoefu.
Kipa Lukasz Fabianski, Johan Djourou, Emmanuel Eboue, Kieran Gibbs na mshambuliaji wa Mexico Carlos Vela ambao walikuwa benchi wakati wa mchezo dhidi ya Sunderland wataanza katika kikosi hicho, lakini hiyo pia itakuwa ni nafasi kwa wachezaji chipukizi Jay Emmanuel-Thomas, Bekin Afobe, Chuks Aneke na Henri Lansbury.
"Naamini kuwa majukumu yake ni kujitolea kwa nguvu zote katika klabu ambayo unachezea na alifanya hivyo alivyokuwa nasi." alisema Wenger.
"Unaweza kuwaelewa watu kutofurahia kama hujafanya hivyo lakini huwezi kuwaliza watu kama huna mkataba ulisainiwa na klabu na hicho ndicho kitu muhimu."
Wakati timu hiyo ikikabiliwa na mchezo huo dhidi ya Spurs, Wenger anatarajia kutumia nafasi hiyo kuwachezesha makinda wake ili wapate uzoefu.
Kipa Lukasz Fabianski, Johan Djourou, Emmanuel Eboue, Kieran Gibbs na mshambuliaji wa Mexico Carlos Vela ambao walikuwa benchi wakati wa mchezo dhidi ya Sunderland wataanza katika kikosi hicho, lakini hiyo pia itakuwa ni nafasi kwa wachezaji chipukizi Jay Emmanuel-Thomas, Bekin Afobe, Chuks Aneke na Henri Lansbury.
Monday, September 20, 2010
"TUNAHITAJI MABAO ZAIDI," - DROGBA.
MSHAMBULIAJI wa Chelsea Didier Drogba amesifu ushindi waliopata wa mabao 4-0 dhidi ya Blackpool na kuendeleza mwanzo mzuri toka walivyoanza ligi mwaka huu.
Pamoja na kutengeneza nafasi nafasi nyingi katika kipindi cha pili, na magoli yote yaliyofungwa katika kipindi cha kwanza na Salomon Kalou, Drogba na Florent Maluda lakini Drgba anaamini kuwa wangefunga magoli mengi zaidi.
"Ulikuwa mchezo mzuri nafikiri tulionyesha uwezo na tulijaribu kushinda magoli mengi kadri tulivyoweza na tukapata mabao manne kipindi cha kwanza nadhani kipindi cha pili tulipata nafasi saba lakini hatukuzitumia vizuri," alisema Drogba baada ya mchezo huo.
"Nafikiri kidogo hatukuwa makini kwa kutokushinda magoli mengine zaidi, kutokuwa sehemu muafaka wakati pasi inapokufikia na hichi ni kitu ambapo inabidi tukifanyie kazi hata kama tulipata ushindi mnono.
Kukosekana kwa nahodha John Terry na msaidizi wake Frank Lampard kufuatia kuwa majeruhi majukumu ya kuiongoza timu hiyo alikabidhiwa Drogba ambapo alisema kuwa ni heshima kubwa kwake lakini alikuwa akiwaombea wachezaji wenzake hao kupata nafuu mapema.
"Najisikia furaha, nimekuwa hapa kipindi cha miaka sita. Lakini imekuwa ni vizuri kuwa pamoja nao. Nahitaji warudi uwanjani haraka lakini ni heshima kubwa kwangu kuwa nahodha wa kikosi hiki leo," alimalizia Drogba.
Pamoja na kutengeneza nafasi nafasi nyingi katika kipindi cha pili, na magoli yote yaliyofungwa katika kipindi cha kwanza na Salomon Kalou, Drogba na Florent Maluda lakini Drgba anaamini kuwa wangefunga magoli mengi zaidi.
"Ulikuwa mchezo mzuri nafikiri tulionyesha uwezo na tulijaribu kushinda magoli mengi kadri tulivyoweza na tukapata mabao manne kipindi cha kwanza nadhani kipindi cha pili tulipata nafasi saba lakini hatukuzitumia vizuri," alisema Drogba baada ya mchezo huo.
"Nafikiri kidogo hatukuwa makini kwa kutokushinda magoli mengine zaidi, kutokuwa sehemu muafaka wakati pasi inapokufikia na hichi ni kitu ambapo inabidi tukifanyie kazi hata kama tulipata ushindi mnono.
Kukosekana kwa nahodha John Terry na msaidizi wake Frank Lampard kufuatia kuwa majeruhi majukumu ya kuiongoza timu hiyo alikabidhiwa Drogba ambapo alisema kuwa ni heshima kubwa kwake lakini alikuwa akiwaombea wachezaji wenzake hao kupata nafuu mapema.
"Najisikia furaha, nimekuwa hapa kipindi cha miaka sita. Lakini imekuwa ni vizuri kuwa pamoja nao. Nahitaji warudi uwanjani haraka lakini ni heshima kubwa kwangu kuwa nahodha wa kikosi hiki leo," alimalizia Drogba.
MESSI NJE WIKI MBILI.
MSHAMBULIAJI wa Barcelona Lionel Messi atakuwa nje ya uwanja kwa muda wa siku kumi tano baada ya kuumia kifundo cha mguu wakati yimu yake ilipoibuka na ushindiwa mabao 2-1 nyumbani kwa timu ya Atletico Madrid.
Kocha wa Barca Pep Guardiola alihakikishiwa kwamba Muargentina huyo hakuvunjika kifundo hicho cha mguu baada ya kuchezewa vibaya na Tomas Ujfalusi lakini ripoti ya waandishi wa habari ilisema kuwa atakosa kuitumikia timu hiyo kwa muda wa wiki mbili au zaidi.
Barca walikuwa wanaongoza baada ya beki huyo wa kimataifa Czech alipanda kadi nyekundu ya moja kwa moja ingawa tayari alikuwa na kadi ya njano kwa kumkwatua Muargenitiana huyo.
Messi alitolewa kwa machela akionekana akiwa katika maumivu makali, lakini Guardiola alisema kuwa nyota wake huyo hakuwa amepata maumivu makubwa sana kama alivyokuwa akihofu hapo mwanzo.
"Tumefurahi kushinda mchezo huu lakini pia tuna majonzi kwa kuumia kwa Leo (Messi)," aliwaambia waandishi wa habari katika mkutano.
Kocha wa Barca Pep Guardiola alihakikishiwa kwamba Muargentina huyo hakuvunjika kifundo hicho cha mguu baada ya kuchezewa vibaya na Tomas Ujfalusi lakini ripoti ya waandishi wa habari ilisema kuwa atakosa kuitumikia timu hiyo kwa muda wa wiki mbili au zaidi.
Barca walikuwa wanaongoza baada ya beki huyo wa kimataifa Czech alipanda kadi nyekundu ya moja kwa moja ingawa tayari alikuwa na kadi ya njano kwa kumkwatua Muargenitiana huyo.
Messi alitolewa kwa machela akionekana akiwa katika maumivu makali, lakini Guardiola alisema kuwa nyota wake huyo hakuwa amepata maumivu makubwa sana kama alivyokuwa akihofu hapo mwanzo.
"Tumefurahi kushinda mchezo huu lakini pia tuna majonzi kwa kuumia kwa Leo (Messi)," aliwaambia waandishi wa habari katika mkutano.
"TORRES NI MDANGANYIFU," - FERGUSON
KOCHA wa Manchester United Sir Alex Ferguson amemtuhumu mshambuliaji wa Liverpool Fernando Torres kwa kudanganya, akisema kuwa alikuza tukio akitaka John O'Shea atolewe nje.
Katika mchezo baina ya timu hizo ulipigwa katika Uwanja wa Old Trafford ulishuhdia mshambuliaji wa United Dimitar Berbatov akifanya tukio la kukumbukwa kwa kupachika wavuni mabao matatu peke yake (Hat-Trick) na kupelekea timu yake kuibuka na ushindi wa mabao 3-2.
Lakini tukiachana na ushindi huo kuna tukio ambalo O'Shea alimuanguasha Torres tukio ambalo lilizaa adhabu ndogo ambayo ilipigwa na Steven Gerrard kushinda bao la pili katika mchezo huo.
"Nililitizama mara ya pili tukio lile na inabidi niseme kuwa Torres alidanganya," alisema Ferguson.
"Alilifanya tukio lile liwe kubwa kwa kutaka mchezaji wetu atolewe nje."
Katika mchezo baina ya timu hizo ulipigwa katika Uwanja wa Old Trafford ulishuhdia mshambuliaji wa United Dimitar Berbatov akifanya tukio la kukumbukwa kwa kupachika wavuni mabao matatu peke yake (Hat-Trick) na kupelekea timu yake kuibuka na ushindi wa mabao 3-2.
Lakini tukiachana na ushindi huo kuna tukio ambalo O'Shea alimuanguasha Torres tukio ambalo lilizaa adhabu ndogo ambayo ilipigwa na Steven Gerrard kushinda bao la pili katika mchezo huo.
"Nililitizama mara ya pili tukio lile na inabidi niseme kuwa Torres alidanganya," alisema Ferguson.
"Alilifanya tukio lile liwe kubwa kwa kutaka mchezaji wetu atolewe nje."
Saturday, September 18, 2010
"SITISHIKI NA MSUKUMO NINAOPATA BARCA" - VILLA.
MSHAMBULIAJI nyota wa Barcelona David Villa amesema kuwa ametulia katika klabu hiyo na anafurahia msukumo anaopata akichezea mabingwa hao.
"Msukumo ninaopata kuhusu matokeo huwa yananifurahisha," "timu nyingi huwa zinajaribu kutuiga sisi na hilo linatufanya kuringia kikosi chetu." alisema Villa katika mkutano na waandishi wa habari.
""Nimetulia na nafurahi kuwa kuwa hapa najiona mwenye bahati. Tayari nimeshajua na wachezaji wenzangu pamoja na malengo yetu, kitu ambacho kinanirahisishia mambo yangu."
"Kwa kifupi najivunia kuwa sehemu ya kizazi hiki cha wachezaji na hapa najisikia niko nyumbani kama mmoja wa familia,"
"Huwa tunapasiana mipira na kushambulia kwa staili ya kipekee. Kwa pamoja Barca na timu ya Taifa ya Hispania tunaweza kucheza na timu yoyote na kuonyesha uwezo wetu. Naamini muonekano wetu ni mfano wa kuigwa na nafurahia hilo."
Mchezaji huyo pia aliongelea kuhusu nahodha wa Arsenal Cesc Fabregas na anaamini kuwa atajiunga na klabu hiyo katika siku za mbeleni.
"Moyo wa Fabregas uko kwa Barca na katika kipindi kifupi au baadae ataiacha Arsenal na kujiunga na sisi," alimalizia Villa.
INTER KUMCHUKUA KAKA JANUARI LAKINI KWA MASHARTI.
KLABU ya Inter Milan inatarajia kufungua mazungumzo kuhusu uhamisho wa mchezaji wa kimataifa wa Brazil Kaka ifikapo Novemba mwaka huu baada ya Rais wa Inter Massimo Moratti kukubali uhamisho huo.
Tetesi kutoka gazeti moja la Italia zilisema kuwa Moratti tayari ameshaongea na bodi ya wakurugenzi ya klabu hiyo Ijumaa ambapo alitaka kutoa ruksa ya kumfukuzia mchezahi huyo. Lakini kama watafikia makubaliano wanayotaka.
Inter inamhitaji mchezaji huyto kwa mkopo lakini kwa makubaliano ya kumnunua mchezaji huyo moja kwa moja baada ya msimu mmoja, kama walivyomchukua Zlatan Ibrahimovic.
Klabu hiyo pia itatakiwa kulipa pesa za mchezaji huyo Real Madrid kwa vipindi tofauti kutokana na muda watakaokubaliana.
Hatahivyo, Inter itamchukua mchezaji huyo kipindi ambacho atakuwa fiti kwa asilimia mia moja.
Wanafanya hivyo kwa kuogopa yasije kutokea yaliyopita wakati Madrid walipowalaumu AC Milan kwa kuwauzia mchezaji huyo ambaye alikuwa majeruhi.
Friday, September 17, 2010
Monday, September 13, 2010
FERGUSON AFIKIRIA KUMTUMIA ROONEY DHIDI YA RANGERS.
MASHAMBULIAJI wa Manchester United Wayne Rooney ameanza mazoezi Jumatatu asubuhi hii kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wa Klabu Bingwa ya Ulaya dhidi ya mabingwa wa scottland Rangers utakaochezwa kesho.
Kocha wa United Sir Alex Ferguson alimuondoa Rooney katika kikosi kilichopambana na na Everton Jumamosi, akisema kuwa alitaka kumlinda dhidi ya mashabiki wanaoweza kumzomea kutokana na kashfa yake binafsi inayomkabili.
Rooney anatarajiwa kuanza katika kikosi hicho kesho wakati timu itakapojaribu kuondokana na jinamizi la Jumamosi ambapo walitoka sare ya mabao 3-3 katika mchezo wa ligi dhidi ya Everton.
Kocha wa United Sir Alex Ferguson alimuondoa Rooney katika kikosi kilichopambana na na Everton Jumamosi, akisema kuwa alitaka kumlinda dhidi ya mashabiki wanaoweza kumzomea kutokana na kashfa yake binafsi inayomkabili.
Rooney anatarajiwa kuanza katika kikosi hicho kesho wakati timu itakapojaribu kuondokana na jinamizi la Jumamosi ambapo walitoka sare ya mabao 3-3 katika mchezo wa ligi dhidi ya Everton.
MADRID WAMMEZEA MATE ROONEY.
WAKATI mshambuliaji wa Manchester United Wayne Rooney akiomba vyombo vya habari kutokushabikia kashfa ya maisha yake binafsi inayomkabili, kuna tetesi zimezagaa kuwa Real Madrid wameamua kuanza kumnyemelea mchezaji ili kuongeza nguvu katika kikosi chao.
Mourinho anajulikana kwa kuwazimia nyota wa Uingereza lakini kocha wa United Sir Alex Ferguson anamatumaini kuwa Mourinho hatataka kumnyakua mchezaji huyo kumpeleka Santiago Bernabeu.
Tayari Mourinho ameshamwambia Ferguson kuwa asijali kwani kumleta Rooney Madrid haitawezekana.
Kuna taarifa iliyotolewa kwa Mourinho na Rais wa Real Madrid Florentino Perez kuwa atatenga kiasi cha Euro milioni 65 kwa ajili ya mchezaji huyo.
"Uhamisho wa Rooney unawezekana" kilisema chanzo hicho cha habari.
"Kulikuwa na utata kuhusu uhamisho wa David Beckham na Cristiano Ronaldo lakini mwisho wa siku wote walitua Bernabeu."
Rooney aliachwa katika kikosi cha United kilichokwenda kucheza na Everton Ferguson akijaribu kumlinda na mashabiki ambao pengine wangemzomea kutokana na kashfa inayomkabili.
Kama hali ikiendelea kuwa mbaya kwa mchezaji huyo, basi atakuwa hana budi bali kuondoka Old Trafford.
Mourinho anajulikana kwa kuwazimia nyota wa Uingereza lakini kocha wa United Sir Alex Ferguson anamatumaini kuwa Mourinho hatataka kumnyakua mchezaji huyo kumpeleka Santiago Bernabeu.
Tayari Mourinho ameshamwambia Ferguson kuwa asijali kwani kumleta Rooney Madrid haitawezekana.
Kuna taarifa iliyotolewa kwa Mourinho na Rais wa Real Madrid Florentino Perez kuwa atatenga kiasi cha Euro milioni 65 kwa ajili ya mchezaji huyo.
"Uhamisho wa Rooney unawezekana" kilisema chanzo hicho cha habari.
"Kulikuwa na utata kuhusu uhamisho wa David Beckham na Cristiano Ronaldo lakini mwisho wa siku wote walitua Bernabeu."
Rooney aliachwa katika kikosi cha United kilichokwenda kucheza na Everton Ferguson akijaribu kumlinda na mashabiki ambao pengine wangemzomea kutokana na kashfa inayomkabili.
Kama hali ikiendelea kuwa mbaya kwa mchezaji huyo, basi atakuwa hana budi bali kuondoka Old Trafford.
BALLACK NJE WIKI SITA.
KIUNGO wa Bayern Leverkusen Michael Ballack atakuwa nje ya uwanja kwa muda wa wiki sita baada ya kuumia mfupa mkubwa wa ndani chini ya mguu wakati timu yake ilipotoka suluhu na timu ya Hanover 96 katika mchezo wa Ligi Kuu ya Ujerumani Jumamosi iliyopita.
Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 33 alifanyiwa uchunguzi wa afya na klabu yake ilikuwa inaamini kuwa mchezaji huyo hakupata majeraha makubwa lakini baada ya kufanyiwa uchunguzi iligundulika maeumia sana.
Habari hizo za kustusha inamaanisha kocha wa Leverkusen Jupp Heynckes atamkosa mchezaji huyo katika mechi muhimu za ligi pamoja na Ligi ya Ulaya (Europa League) na pia kuna uwezekano mkubwa wa kukosekana katika kikosi cha timu yake ya Taifa ya Ujerumani.
Ballack anatarajiwa kukosa mechi ambapo timu yake ya Taifa itacheza na Turkey na Kazakhstan katika kutafuta nafasi ya kuvuzu michuano ya Ulaya mwanzoni mwa Octoba, inamaanisha kuwa hawezi kurudishiwa unahodha wa kikosi hicho ambacho kocha Joachim Loew alimuahidi kumrudishia wakati atapokuwa fiti.
Ballack ameitwa katika kikosi hicho mara 98 tu baada kukosa fainali za Kombe la Dunia zilizofanyika mwaka huu kutokana na maumivu ya kifundo cha mguu, na pia hakuitwa katika kikosi cha Ujerumani kilichocheza na Azerbaijan na Belgium.
Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 33 alifanyiwa uchunguzi wa afya na klabu yake ilikuwa inaamini kuwa mchezaji huyo hakupata majeraha makubwa lakini baada ya kufanyiwa uchunguzi iligundulika maeumia sana.
Habari hizo za kustusha inamaanisha kocha wa Leverkusen Jupp Heynckes atamkosa mchezaji huyo katika mechi muhimu za ligi pamoja na Ligi ya Ulaya (Europa League) na pia kuna uwezekano mkubwa wa kukosekana katika kikosi cha timu yake ya Taifa ya Ujerumani.
Ballack anatarajiwa kukosa mechi ambapo timu yake ya Taifa itacheza na Turkey na Kazakhstan katika kutafuta nafasi ya kuvuzu michuano ya Ulaya mwanzoni mwa Octoba, inamaanisha kuwa hawezi kurudishiwa unahodha wa kikosi hicho ambacho kocha Joachim Loew alimuahidi kumrudishia wakati atapokuwa fiti.
Ballack ameitwa katika kikosi hicho mara 98 tu baada kukosa fainali za Kombe la Dunia zilizofanyika mwaka huu kutokana na maumivu ya kifundo cha mguu, na pia hakuitwa katika kikosi cha Ujerumani kilichocheza na Azerbaijan na Belgium.
Sunday, September 12, 2010
WENGER ATAMBA KUCHUKUA KOMBE LA KLABU BINGWA MSIMU HUU.
KOCHA wa Arsenal Mfaransa Arsen Wenger anaamini kuwa timu yake iko fiti hivi sasa kunyakua kombe la Klabu Bingwa ya Ulaya msimu huu.
Arsenal haijawahi kushinda kikombe chochote cha Ulaya katika kipindi chote cha historia ya timu hiyo, wakati Wenger hajawahi kushinda mashindano akiwa na klabu yoyote barani Ulaya.
Mafanikio ambayo iliwahi kupata klabu hiyo ilikuwa ni mwaka 2006 ambapo walifika fainali lakini walipoteza mchezo huo kwa klabu ya Barcelona.
Wenger naamini katika safari yake hiyo ya kukisaka kikombe hicho cha Ulaya kikwazo kikubwa kitakuwa klabu ya Barcelona.
"Kama kuna timu ya kuogopa basi ni Barcelona," alikaririwa Wenger akisema.
"Hakuna timu isiyofungika lakini kuna timu za kufunga.
"Tuna malengo ya kushinda Klabu Bingwa, ndio. Tuna kikosi ambacho ni kizuri kikiwa na mchanganyika bora na uzoefu. Wakati ukiona timu yetu ikicheza, hutakuwa na swali kuhusu hilo." alimalizia Wenger.
Arsenal inaanza safari yake katika michuano hiyo msimu huu kwa kukutana na klabu ya Sporting Braga ya Ureno, Jumatano inayokuja.
Arsenal haijawahi kushinda kikombe chochote cha Ulaya katika kipindi chote cha historia ya timu hiyo, wakati Wenger hajawahi kushinda mashindano akiwa na klabu yoyote barani Ulaya.
Mafanikio ambayo iliwahi kupata klabu hiyo ilikuwa ni mwaka 2006 ambapo walifika fainali lakini walipoteza mchezo huo kwa klabu ya Barcelona.
Wenger naamini katika safari yake hiyo ya kukisaka kikombe hicho cha Ulaya kikwazo kikubwa kitakuwa klabu ya Barcelona.
"Kama kuna timu ya kuogopa basi ni Barcelona," alikaririwa Wenger akisema.
"Hakuna timu isiyofungika lakini kuna timu za kufunga.
"Tuna malengo ya kushinda Klabu Bingwa, ndio. Tuna kikosi ambacho ni kizuri kikiwa na mchanganyika bora na uzoefu. Wakati ukiona timu yetu ikicheza, hutakuwa na swali kuhusu hilo." alimalizia Wenger.
Arsenal inaanza safari yake katika michuano hiyo msimu huu kwa kukutana na klabu ya Sporting Braga ya Ureno, Jumatano inayokuja.
BARCELONA YAONGOZA KWA MASHABIKI WENGI ULAYA.
KLABU ya Barcelona ndio klabu inyoongoza kwa mashabiki wengi Ulaya ikifuatiwa kwa mbali na klabu ya Real Madrid katika nafasi ya pili, wakati kuna klabu nne za Italia zinafuatia na klabu za Uingereza zikiwa mojawapo katika nafasi 20 za vilabu zenye washabiki wengi Ulaya kwa mujibu wa jarida moja michezo Ulaya.
Taarifa hiyo pia ilisema vigogo wa Ligi Kuu ya Uingereza Manchester United na Chelsea ndio zinazoongoza kwa mashabiki duniani lakini timu zimeshika nafasi ya tatu na ya nne mbele ya Bayern Munich ya Ujerumani.
Gazeti hilo ambalo hutoa tathmini ya vilabu 20 bora vyenye washabiki wengi utafiti wake ndani na nje katika nchi 17 za Ulaya (Ujerumani, Ufaransa, Uingereza, Italia, Hispania, Ureno, Uturuki, Uholanzi, Austria, Switzerland, Greece, Poland, Croatia, Bulgaria, Ukraine, Czech Republic na Russia).
Matokeo hayo yamepatikana baada ya kuwahoji mashabiki 10,200 wenye umri kati ya miaka 16 hadi 69 kutoka nchi mbalimbali zilizoorodheshwa hapo, kabla ya kuchapishwa.
Barcelona walipata asilimia 57.8 katika kura hizo wakati mahasimu wao Madrid walipata asilimia 31.3, Manchester United walikamata nafasi ya tatu kwa kuzoa asilimia 30.6. Chelsea, Arsenal na Liverpool walikamiliza listi hiyo kwa timu za Uingereza.
Italia imewakilishwa na timu nne katika listi hiyo ambapo AC Milan na Inter zipo katika nafasi ya saba na nane wakati Juventus ni ya kumi na Roma ya 19. Matokeo mengine ni kama yavyoonekana hapo chini na asilimia walizopata katika mabano.
Barcelona (57.8), Real Madrid (31.3), Manchester United (30.6), Chelsea (21.4), Bayern Munich (20.7), Arsenal (20.3), AC Milan (18.4), Inter (17.5), Liverpool (16.4), Juventus (13.1), Zenit St. Petersburg (12.6), CSKA Moscow (10.5), Spartak Moscow (9), Marseille (7.8), Ajax (7.1), Galatasaray (6.8), Lyon (6.6), Fenerbahce (6.1), Roma (6), Dynamo Kiev (5.3).
Taarifa hiyo pia ilisema vigogo wa Ligi Kuu ya Uingereza Manchester United na Chelsea ndio zinazoongoza kwa mashabiki duniani lakini timu zimeshika nafasi ya tatu na ya nne mbele ya Bayern Munich ya Ujerumani.
Gazeti hilo ambalo hutoa tathmini ya vilabu 20 bora vyenye washabiki wengi utafiti wake ndani na nje katika nchi 17 za Ulaya (Ujerumani, Ufaransa, Uingereza, Italia, Hispania, Ureno, Uturuki, Uholanzi, Austria, Switzerland, Greece, Poland, Croatia, Bulgaria, Ukraine, Czech Republic na Russia).
Matokeo hayo yamepatikana baada ya kuwahoji mashabiki 10,200 wenye umri kati ya miaka 16 hadi 69 kutoka nchi mbalimbali zilizoorodheshwa hapo, kabla ya kuchapishwa.
Barcelona walipata asilimia 57.8 katika kura hizo wakati mahasimu wao Madrid walipata asilimia 31.3, Manchester United walikamata nafasi ya tatu kwa kuzoa asilimia 30.6. Chelsea, Arsenal na Liverpool walikamiliza listi hiyo kwa timu za Uingereza.
Italia imewakilishwa na timu nne katika listi hiyo ambapo AC Milan na Inter zipo katika nafasi ya saba na nane wakati Juventus ni ya kumi na Roma ya 19. Matokeo mengine ni kama yavyoonekana hapo chini na asilimia walizopata katika mabano.
Barcelona (57.8), Real Madrid (31.3), Manchester United (30.6), Chelsea (21.4), Bayern Munich (20.7), Arsenal (20.3), AC Milan (18.4), Inter (17.5), Liverpool (16.4), Juventus (13.1), Zenit St. Petersburg (12.6), CSKA Moscow (10.5), Spartak Moscow (9), Marseille (7.8), Ajax (7.1), Galatasaray (6.8), Lyon (6.6), Fenerbahce (6.1), Roma (6), Dynamo Kiev (5.3).
HOFU ILITUFANYA KUPOTEZA MCHEZO - INIESTA
KIUNGO wa Barcelona Andres Iniesta amekiri kuwa timu yake ilikuwa na hofu kubwa wakati walipokubali kipigo cha mabao 2-0 wakiwa nyumbani Camp Nou dhidi ya timu ambayo imepanda daraja msimu huu ya Hercules.
Mabao mawili yaliyofungwa na mshambuliaji wa Paraguay Nelson Valdez yalitosha kuisaidia timu hiyo kuondoka na ushindi, ingawa barca walionekana kumiliki mchezo huo lakini hawakuweza mapigo.
Baada ya mchezo huo Iniesta alisema kuwa matokeo hayo yatawastua na kuwaamsha lakini wanatakiwa kuangalia mbele na sio kujilaumu kwa yaliyopita.
"Vikombe vyote tulivyoshinda kipindi cha nyuma haviwezi kutusaidia katika kipindi hichi. Ni matumaini yangu tutalifahamu hili na kuijindaa vyema kwa ajili ya mchezon ujao" alisema Iniesta
"Ni rahisi sana kuingiwa na woga, hakuna mtu ambaye anapenda kufungwa lakini tulijaribu na tulikuwa hatuna bahati tukifika golini kwao."
Barcelona watakuwa na nafasi ya kulipa kisasi katikati ya wiki wakati watakapocheza mchezo wao wa kwanza dhidi ya Panathinaikos, kabla ya kumenyana na Atletico Madrid.
Mabao mawili yaliyofungwa na mshambuliaji wa Paraguay Nelson Valdez yalitosha kuisaidia timu hiyo kuondoka na ushindi, ingawa barca walionekana kumiliki mchezo huo lakini hawakuweza mapigo.
Baada ya mchezo huo Iniesta alisema kuwa matokeo hayo yatawastua na kuwaamsha lakini wanatakiwa kuangalia mbele na sio kujilaumu kwa yaliyopita.
"Vikombe vyote tulivyoshinda kipindi cha nyuma haviwezi kutusaidia katika kipindi hichi. Ni matumaini yangu tutalifahamu hili na kuijindaa vyema kwa ajili ya mchezon ujao" alisema Iniesta
"Ni rahisi sana kuingiwa na woga, hakuna mtu ambaye anapenda kufungwa lakini tulijaribu na tulikuwa hatuna bahati tukifika golini kwao."
Barcelona watakuwa na nafasi ya kulipa kisasi katikati ya wiki wakati watakapocheza mchezo wao wa kwanza dhidi ya Panathinaikos, kabla ya kumenyana na Atletico Madrid.
Friday, September 10, 2010
BLATTER AFIKIRIA KURUDISHA SHERIA YA BAO LA DHAHABU.
RAIS wa Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) Sepp Blatter pamoja na kupokea malalamiko kibao kuhusiana na baadhi ya matukio yaliyokea katika fainali za Kombe la Dunia lililofanyika Afrika Kusini, lakini Rais huyo amefurahishwa na jinsi alivyoziona fainali hizo, ingawa amekiri kuwa anafikiria kubadilisha baadhi ya sheria.
"Kwa ukweli niliona fainali nzuri za Kombe la Dunia mwaka huu. Mpira umekuwa mchezo wa mipango, huku timu zikienda pamoja. Kitu ambacho kinaweza kuwa na muonekano mzuri. kipindi cha nyuma kulikuwa na mipango rahisi ambapo timu hushambulia na kisha kuzuia." ilisema taarifa yake aliyotuma katika tovuti ya FIFA.
"Lakini kuna baadhi ya mechi katika hatua ya makundi katika michuano ya mwaka huu, ambapo tumeshuhudia baadhi ya timu zikizuia kufungwa kwa mchezo wa kutafuta suluhu. Suala hili nataka kulizungumza na Kamati ya Ufundi katika mkutano unaokuja."
"Tutajaribu kutafuta njia ambayo itawezesha kila timu kucheza kwa kujiachia katika mashindano kama haya, wakitafuta ushindi.
"Tunapanga kuchukua nafasi hiyo kuangalia kuhusu suala la muda wa ziada pia. Hivi sasa utaona timu nyingi zipaki mabasi katika kipindi chote cha muda wa nyongeza kuzuia mabao kwa njia yoyote. Kwa kuzuia hili, tunaweza tukaenda katika matuta moja kwa moja baada ya muda wa kawaida au kurudisha sheria ya bao la dhahabu (golden goal rule).
"Tutaangalia itakavyokuwa katika mkutano huo." alimalizia Blatter.
"Kwa ukweli niliona fainali nzuri za Kombe la Dunia mwaka huu. Mpira umekuwa mchezo wa mipango, huku timu zikienda pamoja. Kitu ambacho kinaweza kuwa na muonekano mzuri. kipindi cha nyuma kulikuwa na mipango rahisi ambapo timu hushambulia na kisha kuzuia." ilisema taarifa yake aliyotuma katika tovuti ya FIFA.
"Lakini kuna baadhi ya mechi katika hatua ya makundi katika michuano ya mwaka huu, ambapo tumeshuhudia baadhi ya timu zikizuia kufungwa kwa mchezo wa kutafuta suluhu. Suala hili nataka kulizungumza na Kamati ya Ufundi katika mkutano unaokuja."
"Tutajaribu kutafuta njia ambayo itawezesha kila timu kucheza kwa kujiachia katika mashindano kama haya, wakitafuta ushindi.
"Tunapanga kuchukua nafasi hiyo kuangalia kuhusu suala la muda wa ziada pia. Hivi sasa utaona timu nyingi zipaki mabasi katika kipindi chote cha muda wa nyongeza kuzuia mabao kwa njia yoyote. Kwa kuzuia hili, tunaweza tukaenda katika matuta moja kwa moja baada ya muda wa kawaida au kurudisha sheria ya bao la dhahabu (golden goal rule).
"Tutaangalia itakavyokuwa katika mkutano huo." alimalizia Blatter.
RAIS GBABO WA IVORY COAST AMPIGIA MAGOTI DROGBA.
MFUNGAJI bora wa Ligi Kuu ya Uingereza Didier Drogba ambaye hivi karibuni alitangaza kujitoa kwa muda kuitumikia timu yake ya Taifa ya Ivory Coast ameamua kujiunga tena na timu hiyo baada ya kukutana na Rais Laurent Gbagbo wa nchi hiyo iliyopo Magharibi mwa bara la Afrika mwishoni mwa wiki iliyopita, kwa mujibu wa taarifa ya gazeti moja la michezo nchini humo.
Taarifa ya gazeti hilo iliendelea kusema kuwa Drogba hakuwa na mahusiano mazuri na baadhi ya wachezaji wenzake wa timu hiyo pamoja na viongozi wa Shirikisho la Soka la nchi hiyo . Lakini alihudhuria mchezo ambao timu yake iliirarua Rwanda mabao 3-0 katika kutafuta tiketi ya kucheza michuano ya Mataifa Afrika 2012 kama mshangiliaji.
Rais Gbagbo ni mpenzi mkubwa wa mpira ndio maana akaamua kuingilia kati suala hilo na kumrudisha shujaa huyo wa soka katika timu hiyo baada ya kufanya nae mazungumzo ya kina.
Mshambuliaji huyo wa Chelsea pia alikuna na wachezaji wa timu hiyo kabla ya kuondoka na kurudi katika vilabu vyao na kuwaomba kusahau yaliyopita kwa ajili ya maendeleo ya timu yao ya Taifa, na kuongeza kuwa yuko tayari kuitumikia timu hiyo atapoitwa siku zijazo.
Ivory Coast inatarajiwa kucheza na Burundi Octoba mwaka huu kwa mchezo wa raundi ya pili ya kufuzu michuano ya AFCON.
Taarifa ya gazeti hilo iliendelea kusema kuwa Drogba hakuwa na mahusiano mazuri na baadhi ya wachezaji wenzake wa timu hiyo pamoja na viongozi wa Shirikisho la Soka la nchi hiyo . Lakini alihudhuria mchezo ambao timu yake iliirarua Rwanda mabao 3-0 katika kutafuta tiketi ya kucheza michuano ya Mataifa Afrika 2012 kama mshangiliaji.
Rais Gbagbo ni mpenzi mkubwa wa mpira ndio maana akaamua kuingilia kati suala hilo na kumrudisha shujaa huyo wa soka katika timu hiyo baada ya kufanya nae mazungumzo ya kina.
Mshambuliaji huyo wa Chelsea pia alikuna na wachezaji wa timu hiyo kabla ya kuondoka na kurudi katika vilabu vyao na kuwaomba kusahau yaliyopita kwa ajili ya maendeleo ya timu yao ya Taifa, na kuongeza kuwa yuko tayari kuitumikia timu hiyo atapoitwa siku zijazo.
Ivory Coast inatarajiwa kucheza na Burundi Octoba mwaka huu kwa mchezo wa raundi ya pili ya kufuzu michuano ya AFCON.
Subscribe to:
Posts (Atom)